Vyamavingi
JF-Expert Member
- Oct 3, 2014
- 5,745
- 5,446
Jana nilitembelewa na Balozi wa nyumba 10 wa CCM ambaye ni jirani yangu. Amekuja na karatasi / fomu mkononi na kunikabidhi ati nijaze jina langu, namba ya kadi ya CCM, na namba ya kadi ya mpiga kura! Anasema chama kinachukua upya takwimu za wanachama wake. Hakujua kuwa mimi sio mwana CCM na nikatumia nafasi hiyo kumwambia kuwa mimi sio mwanachama wa Chama chochote cha siasa.
Ili kumsaidia malengo yake, nikampeleka kwenye nyumba nyingine zilizo ndani ya uzio tunaoishi pamoja.
Nyumba ya kwanza tumemkuta mke wa mpangaji ambaye akatuambia kuwa naye sio mtu wa siasa na hana kadi ya chama chochote. Nikamchokoza huyo dada, vipi kuhusu John (mumewe ), akasema John yeye ni Chadema! Nikampeleka Balozi nyumba ya tatu, akatoka house girl. Kwa kuwa ni mtu mzima, nikamtambulusha kwa Balozi, dada akasema kadi yake hajui iko wapi. Balozi akauliza kuhusu kipalata cha kupiga kura, dada akasema hajui kiko wapi, hatimaye akapata ujasiri wa kusema yeye sio CCM.
Basi sikutaka hata kumpleka Balozi nyumba ya mwisho, nikamwambia jamaa hayupo maana msela anayekaa hapo najua kwa uhakika kuwa ni Chadema damu.
Nilichojifunza na kumpa Balozi pongezi ni ile ari yake ya kutekeleza maagizo ya Chama chake; na kuwa kwa CCM, uchaguzi unapoisha, wanajiandaa kwa uchaguzi unaokuja.
Wapinzani, jifunzeni kupitia mikakati ya CCM, hapo ndipo wanawapiga bao.
Vv
Ili kumsaidia malengo yake, nikampeleka kwenye nyumba nyingine zilizo ndani ya uzio tunaoishi pamoja.
Nyumba ya kwanza tumemkuta mke wa mpangaji ambaye akatuambia kuwa naye sio mtu wa siasa na hana kadi ya chama chochote. Nikamchokoza huyo dada, vipi kuhusu John (mumewe ), akasema John yeye ni Chadema! Nikampeleka Balozi nyumba ya tatu, akatoka house girl. Kwa kuwa ni mtu mzima, nikamtambulusha kwa Balozi, dada akasema kadi yake hajui iko wapi. Balozi akauliza kuhusu kipalata cha kupiga kura, dada akasema hajui kiko wapi, hatimaye akapata ujasiri wa kusema yeye sio CCM.
Basi sikutaka hata kumpleka Balozi nyumba ya mwisho, nikamwambia jamaa hayupo maana msela anayekaa hapo najua kwa uhakika kuwa ni Chadema damu.
Nilichojifunza na kumpa Balozi pongezi ni ile ari yake ya kutekeleza maagizo ya Chama chake; na kuwa kwa CCM, uchaguzi unapoisha, wanajiandaa kwa uchaguzi unaokuja.
Wapinzani, jifunzeni kupitia mikakati ya CCM, hapo ndipo wanawapiga bao.
Vv