DOKEZO Wananchi hatumtaki Mjumbe wa Mbezi Msumi (Dar), anatumia madaraka yake vibaya

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Sisi Wananchi wa Mbezi Msumi Shina Namba 7 kuna Mjumbe anaitwa Michael Meshack Mnyeke, asilimia kubwa ya Wananchi wa huku hatumtaki kutokana na tabia yake ya kuonea watu na kutumia madaraka yake vibaya.

Alhamisi iliyopita tulifanya kikao cha Wananchi pamoja viongozi wa Mtaa pamoja na CCM ambao ndio wamempa nafasi hiyo, tumewasilisha malalamiko yetu na wakasema watayafanyia kazi lakini mpaka leo Machi 12, 2024 hakuna kilichojibiwa.

Baadhi ya manyanyaso ambayo amekuwa akituhumiwa ni kuingia ndani ya nyumba za watu bila utaratibu, anatamba hakuna wa kumfanya kitu chochote kwa kuwa yeye ndio Serikali, amekuwa akichukua mali za watu kwa nguvu, mfano hivi karibuni alimpora mtu pikipiki kwa kutumia cheo chake.

Malalamiko haya nyafikisha hapa kwa kuwa kama hatua hazitachukuliwa tumekubaliana kuwa tunaweza kurudisha kadi za Uanachama kwa kuwa CCM wakiendelea kumuacha inamanisha wanaridhia tuendelee kunyanyasika.


====== ==
JamiiForums ilipozungumza na Balozi wa Mbezi Msumi, Ismail Mbinda amesema “Kweli nimepata malalamiko ya Mjumbe huyo na Wananchi wameyawasilisha katika Ofisi ya CCM Mbezi Msumi ambayo ndio imemdhamini, wao huko ndio watatoa majibu na kujua hatua za kuchukua.”
 
Msumi mjumbe shina namba 5 ndiye aliyepaweza na bila shaka zamani mpaka namba 7 ilikuwa ni eneo lake. Alikuwa anaitwa mzee Beka, lakini leo hata makalvati yaliyoletwa enzi zake yamekwisha funikwa na mchanga wa mvua.

Barabara hazipitiki. Michango ya miundo mbinu yakusanywa haijulikani wapi inakwenda. Walianzisha michango ya ulinzi shirikishi, lakini udokozi kama kawsida, ipo siku manake vibaka twawajua.

Kuna daraja linalounganisha msumi na kisauke(madale)toka limezombwa na maji viongozi woote kimyaa halafu kura wanategemea zitatoka wapi?
 
Yaani badala ya kufanya maamuzi magumu mnajinadi kurejesha kadi! Huu ni upuuzi wa Hali ya juu! Mtu hamumtaki andamaneni kumkaraa na aachie ngazi mara moja.

CCM hatujui vikao! Kiongozi akipewa nafasi anatumia akili za hovyo na wanaendelea kumkumbatia usishangae akapewa nafasi ya juu zaidi.

Fanyeni maamuzi acheni uchawa!.
Ni hilo tu!
 
Mmezidi unyonge huko kwenu mahakama hakuna au nyie wanaume wazima mnamshindwa vipi mtu mmoja huo ni uzembe, yani unakubali vipi mtu anaingia nyumbani kwako kizembe huyo polisi mwenyewe tu akija kwangu aje amejipanga uje na nyaraka zote zinazokupa mamlaka ya kuingia nyumbani kwa mtu, hiyo ni haki yako ya msingi usikubali mtu aichukue.
 
Magufuli kutuita watanzania wanyonge hakukosea kabisa.

Yani mjumbe wa shina ujifanye unaingia kwangu bila taarifa kisa ujumbe wako, pumbavu, watu wataenda kumuokotea mochwari.

Kirahisi rahisi tu eti kisa mjumbe uchukue pikipiki yangu. Mungu saidia nisikutane na huo upumbavu.
 
Kwa mujibu wa sheria za Tanzania Mjumbe wa shina wa ccm hana mamlaka yoyote katika lolote lile popote pale , inakuwaje mnakubali huo ujinga nyie ?
Kwa Msumi mjumbe ni dili....haya ni makazi mapya....raia wako bize..kutoka alfajiri kurudi giza...unakutana na barua ya mchango wa barabara....mchango wa umeme....mchango wa maji....mchango wa ulinzi shirki..na kadhalika wa kadha
 
Magufuli kutuita watanzania wanyonge hakukosea kabisa.

Yani mjumbe wa shina ujifanye unaingia kwangu bila taarifa kisa ujumbe wako, pumbavu, watu wataenda kumuokotea mochwari.

Kirahisi rahisi tu eti kisa mjumbe uchukue pikipiki yangu. Mungu saidia nisikutane na huo upumbavu.
Kuna nyumba alichukua kuku kisa jamaa hana hela ya ulinzi shirki
 
Yaani Mbezi msumi ni sehemu iliyosahaulika hapa Dar-es-salaam. Ni zaidi ya mwezi toka daraja lenu linalounganisha madale na Msumi Kusombwa na maji ila hakuna ukarabati wowote uliofanywa.

Huduma za Maji ya Dawasco hakuna, mnaishia maji ya chumvi ambayo yanasambazwa na watu waliochimba visima.


Kero yenu kubwa ni barabara...aisee hiyo barabara yenu ni kiunganishi kikubwa kati ya Mbezi -Madale- wazo-Tegeta kibaoni ila serikali haina mpango wa kuiweka lami wala vifusi vya changarawe.

Wamiliki wa daladala hawataki kupeleka magari mbezi Msumi kutokana na ubovu wa barabara.

Ukifika hapo mbezi mwisho foleni ya wakazi wa msumi wanaongojea usafiri ni balaa ,unaweza kusema kuna halaiki ya watu. Ni njia yenye abiria wengi sana ila mabasi ni machache na nauli inapofika jioni watu hutozwa 1000....huku bajaji nauli ikifika mpaka 3000 kwa abiria mmoja.

Barabara ya kilometa 13 tu kutoka mbezi mwisho ambayo kama ikiwekwa lami itakuwa ni suluhisho la wakazi wengi wa Mbezi makabe,mbezi msumi,tegeta A,Madale,Mbopo,Goba na Tegeta.

Nilishawahi kufika huko kufanya mradi fulani ila adha ya usafiri niliyoiona si ya nchi hii. Mkazi wa msumi mpaka afike na kurudi kutoka kariakoo anatumia zaidi ya sh 5000 ya nauli kila siku.

Lieni na Mbunge wenu ili akaililie serikali ije kuweka lami hiyo barabara mpate kuepukana na adha ya usafiri.

Niliwahi kufika mwaka 2006 nikakuta usafiri wa huko mnapanda canter za chai maharage. Ikifika saa 12 jioni usafiri hakuna ...ilikuwa ni shida sana.
 
Sisi Wananchi wa Mbezi Msumi Shina Namba 7 kuna Mjumbe anaitwa Michael Meshack Mnyeke, asilimia kubwa ya Wananchi wa huku hatumtaki kutokana na tabia yake ya kuonea watu na kutumia madaraka yake vibaya.

Alhamisi iliyopita tulifanya kikao cha Wananchi pamoja viongozi wa Mtaa pamoja na CCM ambao ndio wamempa nafasi hiyo, tumewasilisha malalamiko yetu na wakasema watayafanyia kazi lakini mpaka leo Machi 12, 2024 hakuna kilichojibiwa.

Baadhi ya manyanyaso ambayo amekuwa akituhumiwa ni kuingia ndani ya nyumba za watu bila utaratibu, anatamba hakuna wa kumfanya kitu chochote kwa kuwa yeye ndio Serikali, amekuwa akichukua mali za watu kwa nguvu, mfano hivi karibuni alimpora mtu pikipiki kwa kutumia cheo chake.

Malalamiko haya nyafikisha hapa kwa kuwa kama hatua hazitachukuliwa tumekubaliana kuwa tunaweza kurudisha kadi za Uanachama kwa kuwa CCM wakiendelea kumuacha inamanisha wanaridhia tuendelee kunyanyasika.
Kuna mwaka nilisikia mtendaji wa Mbezi Msumi alikatwa shingo na kuuliwa ndani ya ofisi yake....sijui ile kesi iliishia wapi.
 
Sisi Wananchi wa Mbezi Msumi Shina Namba 7 kuna Mjumbe anaitwa Michael Meshack Mnyeke, asilimia kubwa ya Wananchi wa huku hatumtaki kutokana na tabia yake ya kuonea watu na kutumia madaraka yake vibaya.

Alhamisi iliyopita tulifanya kikao cha Wananchi pamoja viongozi wa Mtaa pamoja na CCM ambao ndio wamempa nafasi hiyo, tumewasilisha malalamiko yetu na wakasema watayafanyia kazi lakini mpaka leo Machi 12, 2024 hakuna kilichojibiwa.

Baadhi ya manyanyaso ambayo amekuwa akituhumiwa ni kuingia ndani ya nyumba za watu bila utaratibu, anatamba hakuna wa kumfanya kitu chochote kwa kuwa yeye ndio Serikali, amekuwa akichukua mali za watu kwa nguvu, mfano hivi karibuni alimpora mtu pikipiki kwa kutumia cheo chake.

Malalamiko haya nyafikisha hapa kwa kuwa kama hatua hazitachukuliwa tumekubaliana kuwa tunaweza kurudisha kadi za Uanachama kwa kuwa CCM wakiendelea kumuacha inamanisha wanaridhia tuendelee kunyanyasika.
Wewe unaishi mbezi Bado unaamini mjumbe wa shina wa CCM ni mtendaji wa selikali? Wewe na wenzako munaoamini hivyo ni wajinga sana
 
Magufuli aliiweka hiyo barabara ya Msumi katika mpango wa TANROAD ...ilitakiwa iwekwe lami kitambo kama wenzenu wa barabara ya Mbezi -Goba walivyowekewa lami na Tegeta-Madale-Goba njia nne walivyowekewa lami.

Maendeleo yanachelewa kuja msumi kutokana na ubovu wa barabara. GOBA sasa hivi viwanja havishikiki kutokana na maendeleo ya barabara na huduma nyingine za kijamii kuwa karibu na wananchi.
 
Back
Top Bottom