Vin24vin
Member
- Sep 2, 2014
- 75
- 67
Habari wanajamvi! Naomba niende moja kwa moja kwenye mada ili niweze pata ushauri toka kwenu.
Nimefahamiana na huyu binti tangu mwaka 2014, wakati huo akiwa bado ni mwanachuo na mimi nikiwa muajiriwa (kazini) tayari. Nilimpenda sana kiasi ya kuweza kupunguza idadi ya mabinti niliokuwa na urafiki nao wa kimapenzi kwa sababu tu huyu binti ndie alieuaminisha moyo wangu kuwa ndio "the one". Kwa kuwa nina kipato, hakika hakuwahi kukosa hizi huduma za mwanaume kwa mpenzi wake. Na hakika katika urafiki wetu wote amekuwa/alikuwa kweli ni binti sahihi kwangu!
Nia yangu ya dhati ya kumuoa aliifahamu kadiri siku zilivyokuwa zinasonga na ombi lake kwangu lilikuwa nimpe muda amalize chuo ndipo taratibu zingine zifuate.
Hakika mpaka naandika uzi huu ni kwamba siuelewi mwenendo wa mwenzangu.
Mwaka jana mwezi wa 06 niliweza kwenda kwao na kuchumbia rasmi na ilipofika mwezi wa 11 nikapeleka mahari kama ambavyo familia zote mbili zilikubaliana na ka-engagement party kalifanyika.
"November" hiyo hiyo familia yangu ikatangaza tarehe ya harusi kuwa ingekuwa ni mwezi wa tano 2020.
Kutokana na mambo makubwa mawili ya kifamilia ya upande wangu yanayonikabili na mimi ndio nikiwa "provider" wa yote hayo, sikuwa na budi ya kufanya kikao cha dharura na familia yangu mwanzoni mwa mwezi December mwaka jana, nadhima kuu ikiwa ni ku-review ila tarehe ya harusi ambayo tuliisema kule ukweni mwanzoni mwa mwezi wa 11 mwaka jana, 2019.
Familia yangu ilinielewa na kufikia maamuzi ya kuwajuza wakwe wetu kwa kuwaeleza kiundani zaidi, na kuwapa taarifa kuwa tutasogeza harusi kutoka mwezi wa 5,2020 uliopangwa awali na sasa harusi itakuwa ni mwezi wa 08,2020.
Sasa cha kushangaza ni kwamba nikashangaa ghafla mwenzangu akaanza kuninunia bila sababu ila baada ya kuongea nae kwa kirefu akanieleza sababu kuwa hana uhakika na mimi kama kweli nitamuoa na kwamba nimemdhalilisha kwao kuwa ataonekana ana mume mtarajiwa asiye na mipango na kwanini tulishatangaza mwezi wa ndoa ilhali tulikuwa tunajua tutakuja kuibadili (hapa ndio niliishiwa nguvu maana nafahamu matatizo huwa hayaji kwa taarifa).
Na hivi niandikapo uzi huu wanajamvi, ni kwamba tangu mwezi wa 12 katikati ya mwaka jana na mpaka leo hii, mwezi huu wa 2,2020, tumewasiliana kwenye simu mara mbili tu na ni kwa msg na ambazo wala hazihusu kwanini yeye amekuwa hajibu msg zangu na wala haihusu yeye kunijibu kuwa kwanini amekuwa hapokei simu zangu!
Wanajukwaa, naombeni ushauri wenu katika hili, nini nifanye? Pana mapenzi tena hapa?
Pana ndoa kweli hapa?
Nimefahamiana na huyu binti tangu mwaka 2014, wakati huo akiwa bado ni mwanachuo na mimi nikiwa muajiriwa (kazini) tayari. Nilimpenda sana kiasi ya kuweza kupunguza idadi ya mabinti niliokuwa na urafiki nao wa kimapenzi kwa sababu tu huyu binti ndie alieuaminisha moyo wangu kuwa ndio "the one". Kwa kuwa nina kipato, hakika hakuwahi kukosa hizi huduma za mwanaume kwa mpenzi wake. Na hakika katika urafiki wetu wote amekuwa/alikuwa kweli ni binti sahihi kwangu!
Nia yangu ya dhati ya kumuoa aliifahamu kadiri siku zilivyokuwa zinasonga na ombi lake kwangu lilikuwa nimpe muda amalize chuo ndipo taratibu zingine zifuate.
Hakika mpaka naandika uzi huu ni kwamba siuelewi mwenendo wa mwenzangu.
Mwaka jana mwezi wa 06 niliweza kwenda kwao na kuchumbia rasmi na ilipofika mwezi wa 11 nikapeleka mahari kama ambavyo familia zote mbili zilikubaliana na ka-engagement party kalifanyika.
"November" hiyo hiyo familia yangu ikatangaza tarehe ya harusi kuwa ingekuwa ni mwezi wa tano 2020.
Kutokana na mambo makubwa mawili ya kifamilia ya upande wangu yanayonikabili na mimi ndio nikiwa "provider" wa yote hayo, sikuwa na budi ya kufanya kikao cha dharura na familia yangu mwanzoni mwa mwezi December mwaka jana, nadhima kuu ikiwa ni ku-review ila tarehe ya harusi ambayo tuliisema kule ukweni mwanzoni mwa mwezi wa 11 mwaka jana, 2019.
Familia yangu ilinielewa na kufikia maamuzi ya kuwajuza wakwe wetu kwa kuwaeleza kiundani zaidi, na kuwapa taarifa kuwa tutasogeza harusi kutoka mwezi wa 5,2020 uliopangwa awali na sasa harusi itakuwa ni mwezi wa 08,2020.
Sasa cha kushangaza ni kwamba nikashangaa ghafla mwenzangu akaanza kuninunia bila sababu ila baada ya kuongea nae kwa kirefu akanieleza sababu kuwa hana uhakika na mimi kama kweli nitamuoa na kwamba nimemdhalilisha kwao kuwa ataonekana ana mume mtarajiwa asiye na mipango na kwanini tulishatangaza mwezi wa ndoa ilhali tulikuwa tunajua tutakuja kuibadili (hapa ndio niliishiwa nguvu maana nafahamu matatizo huwa hayaji kwa taarifa).
Na hivi niandikapo uzi huu wanajamvi, ni kwamba tangu mwezi wa 12 katikati ya mwaka jana na mpaka leo hii, mwezi huu wa 2,2020, tumewasiliana kwenye simu mara mbili tu na ni kwa msg na ambazo wala hazihusu kwanini yeye amekuwa hajibu msg zangu na wala haihusu yeye kunijibu kuwa kwanini amekuwa hapokei simu zangu!
Wanajukwaa, naombeni ushauri wenu katika hili, nini nifanye? Pana mapenzi tena hapa?
Pana ndoa kweli hapa?