Kweli watanzania mwaka huu wa uchaguzi wameburudika sana na matamasha ya bure ya fiesta kutoka kwa chama tawala. Badala ya kusubiri matamasha ya Kilimanjaro na Serengeti fiesta ambapo wanalipia kuanzia buku tano hadi kumi. Imekuwa ni bure kabisa na bado unasafirishwa kwenda kwenye matamasha. Huko kwenye matamasha wamefanikiwa kuwaona akina diamond, wema, ze comedy, mr blue, mwanafa, khadija kopa na wasanii wengine wa fani ya kupiga push up kama mapadlock. Hata kama ni mimi lazima ningekwenda kuwaona kwani burudani inaondoa stress. Sasa waTz mmepunguza stress kwa kuwaona wasanii na watoa burudani za push ups kilishobaki ni kuondoa stress kabisa kwa kuikataa CCM. Peeeeeeeoooooooooooooooooples!