Urafiki si kuungana mkono hata penye ubaya. Kumuunga mkono rafiki hata anapokosea huo ndio unafiki hasa!!!!!!
Kumlaumu mtu anapokosea siyo uadui. Wewe ulitaka aue raia wasio na hatia kwa sumu haalfu dunia nzima ichekelee tu?
Kuungana na adui katika jambo jema ni dalili ya ukweli na nia thabiti. Adui anakuwa adui anapofanya jambo la kukudhuru. Lakini binadamu wa kawaida anapoonyesha roho ya kumsaidia huyo unayemwita adui, kumtoa kwenye mkwamo, kwa nini wewe ulazimishe ashikilie ubaya, aache kusaidia? Wewe ndiye unaroho ya shetani isiyokuwa na suluhu.
Kwa hiyo wewe ungemwona mmarekani si mnafiki, kama angeacha raia wasio na hatia wa syria wanaendelea kumalizika kwa hili shetani ISIS? Huoni tu kwamba bado yuko katika mtiririko ule ule wa kuwatetea raia wa syria? Raisi wao alipokuwa anawaua kwa sumu, America ilipiga kelele kulaani mauaji yale. Kosa liko wapi katika hoja hii?
Leo ISIS inachinja raia wa syria kama vile mulima asafishavyo mbigiri shambani, raisi wa syria amezidiwa, America inaamua kumsaida, ubaya au kosa la Americaliko wapi hapa?
My dear, is good you learn when to cast a stone. Si kila kitu unalaumu maadam, America ilishakuwa shamba lenu la bibi la kulaumu.
Please, wish you a peaceful weekend.