Nyakijooga
Senior Member
- Dec 9, 2018
- 123
- 202
Imeelezwa kuwa moja ya changamoto ambayo inawakumba Wastaafu wengi Nchini ni kukwama kwenye biashara sababu ya kukosa uzoefu.
Hayo yameelezwa na Meneja Masoko wa Benki ya Mwalimu (MCB), Hannah Mbajo wakati wa uzinduzi wa Kapu la MwalimuSanta, ambapo ameeleza kuwa kwa kutambua changamoto hiyo MCB imebuni njia itakayotumika kuwa suluhu la mafao ya kustaafu ili kuwasaidia wanaostaafu.
Amesema taasisi hiyo ni sehemu salama kwa Wastaafu kuwekeza ambao wanaweza kuchukua fedha zao wakati wowote huku wakijihakikishia usalama wa mali zao kwa kupatiwa bima.
Ameongeza kuwa Kapu la MwalimuSanta linamruhusu mstaafu aliyewekeza fedha zake MCB kukopa Asilimia 80 ya fedha alizowekeza kupitia mkopo wa 'Mlinde Mstaafu'.
Mbajo alisema Kapu la MwalimuSanta limebeba bidhaa muhimu kwa wastaafu watarajiwa na waliostaafu tayari ambao watawekeza fedha zao kwa faida ya asilimia 12 kwa mwaka na kupata bila malipo bima ya nyumba na samani za ndani.
“Watuamini tuwawekee fedha hizo wakiwa na uhakika wa kupata faida kila mwisho wa mwezi au mwisho wa mwaka,” amesema Mbajo na kuongeza kuwa MCB imezindua Kampeni ya Kapu la MwalimuSanta ili kusherehekea sikukuu za mwisho wa mwaka na kugawa zawadi mbalimbali kwa wateja wake.
"...Kapu la MwalimuSanta halikuishia hapo likaendelea kwa kuwalipia wastaafu bima ya nyumba kama anayo ama samani zote za ndani.
"Sote tunaona hivi sasa majanga mbalimbali yameongezeka kuna moto, mafuriko kama kule Manyara na hii ni kwasababu ya mabadiliko ya tabianchi hivyo tunamkinga mstaafu wetu na majanga ya aina yoyote," amesema Mbajo.
Akizungumzia bidhaa nyingine iliyopo kwenye Kapu la MwalimuSanta, Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Kidigitali cha MCB, Elilumba Kinyau alisema kapu hilo pia linagawa zawadi hadi sh. 50,000 kwa wateja wake watakaofanya muamala wa kiwango chochote bila kadi kupitia kwa wakala.
"Hii ni zawadi kwa wateja wetu watano kila wiki kipindi hiki cha sikukuu za mwisho wa mwaka mteja akitoa hela bila kadi kwa wakala wa MCB popote alipo atajipatia fedha taslim hadi sh 50,000 hapohapo," alisema Kinyau na kuongeza kuwa MCB ina mawakala zaidi ya 500 nchi nzima na huduma za benki kiganjani.
Hayo yameelezwa na Meneja Masoko wa Benki ya Mwalimu (MCB), Hannah Mbajo wakati wa uzinduzi wa Kapu la MwalimuSanta, ambapo ameeleza kuwa kwa kutambua changamoto hiyo MCB imebuni njia itakayotumika kuwa suluhu la mafao ya kustaafu ili kuwasaidia wanaostaafu.
Amesema taasisi hiyo ni sehemu salama kwa Wastaafu kuwekeza ambao wanaweza kuchukua fedha zao wakati wowote huku wakijihakikishia usalama wa mali zao kwa kupatiwa bima.
Mbajo alisema Kapu la MwalimuSanta limebeba bidhaa muhimu kwa wastaafu watarajiwa na waliostaafu tayari ambao watawekeza fedha zao kwa faida ya asilimia 12 kwa mwaka na kupata bila malipo bima ya nyumba na samani za ndani.
“Watuamini tuwawekee fedha hizo wakiwa na uhakika wa kupata faida kila mwisho wa mwezi au mwisho wa mwaka,” amesema Mbajo na kuongeza kuwa MCB imezindua Kampeni ya Kapu la MwalimuSanta ili kusherehekea sikukuu za mwisho wa mwaka na kugawa zawadi mbalimbali kwa wateja wake.
"...Kapu la MwalimuSanta halikuishia hapo likaendelea kwa kuwalipia wastaafu bima ya nyumba kama anayo ama samani zote za ndani.
"Sote tunaona hivi sasa majanga mbalimbali yameongezeka kuna moto, mafuriko kama kule Manyara na hii ni kwasababu ya mabadiliko ya tabianchi hivyo tunamkinga mstaafu wetu na majanga ya aina yoyote," amesema Mbajo.
Akizungumzia bidhaa nyingine iliyopo kwenye Kapu la MwalimuSanta, Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Kidigitali cha MCB, Elilumba Kinyau alisema kapu hilo pia linagawa zawadi hadi sh. 50,000 kwa wateja wake watakaofanya muamala wa kiwango chochote bila kadi kupitia kwa wakala.
"Hii ni zawadi kwa wateja wetu watano kila wiki kipindi hiki cha sikukuu za mwisho wa mwaka mteja akitoa hela bila kadi kwa wakala wa MCB popote alipo atajipatia fedha taslim hadi sh 50,000 hapohapo," alisema Kinyau na kuongeza kuwa MCB ina mawakala zaidi ya 500 nchi nzima na huduma za benki kiganjani.