Hangaikeni naye vizuri..

Hangaikeni naye vizuri..

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,102
Reaction score
828,977
Ni mzalendo wa kweli
Ni mpenda haki
Ni mcha Mungu wa kweli... Lakini ni mzee wa rula.. Hapendi konakona
Hangaikeni naye vizuri, atawafaeni huko mbeleni.. Nyie na wana wenu na vizazi vyenu
Ni mtu mwema mwenye kibali machoni pa Muumba wetu.. Hangaikeni naye vizuri ni kizalia cha Ibrahim Troule

Msidanganywe na wanaomuogopa.. Wenye dhambi hukimbia hata vivuli vyao... Wana mashaka mengi juu ya machumo ya dhuluma wanayomiliki.. Wamevimbiwa na kuvimbilwa lakini bado wanakula
Hofu yao kubwa sio kutapika kwa hiari bali kutapishwa kwa nguvu...

Hangaikeni naye vema ni mlinzi imara na mpambanaji wa kweli wa maslahi yenu
Wa haki zenu
Wa utu wenu
Wa hatima zenu

Kamwe msikubali kugombanishwa naye... Hawako tayari kuwaona mnapatana naye.. Maana wanatambua fika.. Huo ndio utakuwa mwisho wao..
Hangaikeni naye vema mkitambua ya kwamba kuna kesho na kesho yenyewe haiko mbali
 
hangaikeni naye vzuri japo hata mwenye mamlaka na mlango mdogo kule pekini anatamani aufunge ili asiingie ila anahofia ugali wake.
1744422495382.jpg
 
CHAMA cha Wanasheria Tanganyika (TLS), kimetoa wito wa kuachiwa mara moja na bila masharti yoyote kwa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Wakili Tundu A. Lissu na kubainisha kuwa kukamatwa kwake kunadhoofisha heshima ya taaluma ya sheria na misingi ya haki.

Taarifa ya leo Aprili 12, 2025 iliyotolewa na Rais wa TLS, Wakiili Boniface Mwabukusi imeeleza kuwa kuendelea kushikiliwa kwake kunaashiria vitisho kwa Wanasheria na washiriki wa siasa nchini.

“Iwapo wito huo hautazingatiwa, TLS inahifadhi haki ya kupendekeza kusitishwa kwa huduma za uwakilishi wa kesi za msaada wa kisheria (dock brief) na huduma nyingine za kisheria za kujitolea zinazotolewa na TLS na Wanachama wake, kama njia ya amani ya kupinga vitendo vya unyanyasaji na mashtaka yenye mlengo wa kisiasa"——imesema taarifa hiyo

TLS imemtaka pia Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kuhakikisha kuwa mashtaka mazito kama ya uasi yanaungwa mkono na ushahidi madhubuti na hoja za kisheria na kwamba Uongozi wa kisiasa pekee hauwezi kuchukuliwa kuwa ni kitendo cha uasi kwa mujibu wa sheria zilizopo.

"Kukamatwa kwa Wanasiasa kinyume na sheria kunaweza kusababisha upinzani na machafuko, Mamlaka zinapaswa kuchukua hatua za kisheria na za tahadhari ili kudumisha amani na umoja wa kitaifa, na kuepusha hali ya hofu miongoni mwa wanasiasa kuelekea uchaguzi mkuu”

#KitengeUpdates
1744477106542.jpg
 
Back
Top Bottom