Hamad Rashid aapa kuimaliza CUF

Hamad R hata kama yuko sahihi lakini strategy anayotumia ya kupambana kwa nguvu aslani hatafika popote mbele ya Seif. Ingawa hadi sasa sielewi nani anatumiwa kati ya Hamadi na Seif lakini HR aelewe Seif ndiye kashika mpini hata kama CCM wanamtumia HR hawatamuacha mshirika wao mkuu Seif.



HAMAD RASHID anaweza kuwa yuko right,sishangai kabisa kinachompata,Hivi vyama vyenu vyote vinavyolilia demokrasia kiukweli ndio vimekua vya kwanza kuminya na kubaka demokrasia ndani ya vyama hasa katika chaguzi za ndani,ni jambo la kawaida sasa kwa wenyeviti wa vyama mbadala vya Tanzania kuiona nafasi ya uenyekiti kama ni taasisi yao binafsi,anapotokea mtu kutaka kuwapa challenge kwenye nafasi hiyo unapoitishwa uchaguzi kwa mujibu wa katiba za vyama hivyo wenyeviti wetu hawa hununa na kufanya hila za kuwazuia,hawapendi kuwa tested,wao wangependelea zaidi kuwa wenyeviti wa maisha;sizungumzi kwa majungu ipo mifano hai ambayo ndio hata imechangia wetu wengine kama mimi kutokua na vyama na kuamua kutofungamana na upande wowote kutokana na kutotaka kujiweka karibu na demokrasia za kinafiki,mifano ni kama ifuatayo:

Kila mtu aliona mutungirehi alivyonyanyasa na kugombana na mrema alipotangaza kugombea nafasi ya "mzee" kwenye uchaguzi mkuu wa tlp,mwanzoni walikua marafiki na mrema kumchulkulia kama kijana wake lkn aliposema mzee na mimi nataka nikupime ubavu akaonekana hana adabu!

Tukaja kuona jinsi profesa safari alivyodhalilishwa na cuf kisa kutaka kumpima ubavu Lipumba!wakasema eti kwa kutaka kuyumia haki yake ya kupigiwa kura ama kuchaguliwa ndani ya chama chake na wanachama wenzake eti ametumwa na adui(ccm)!!!!!!!

Pia kila mtu hapa anakumbukumbu ya kilichompata marehemu chacha wangwe pale alipojaribu kumpima ubavu "bwana mkubwa" wa chadema,kwanza alianza kwa kugombea nafasi ya makamu mwenyekiti,mwenyekiti mboe akafanya kila analolijua kumzuia asigombee akashindwa,then akatumia kila mbinu chafu na safi ili jamaa asipate kura za kutosha pia ikashindikana marehemu chacha akaibuka kidedea bwana mkubwa akanuna sana,hakuipenda demokrasia iliyotumika kumuweka madarakani rasta,alitaka aweke mtu wake wanachama wakamwambia no mzee kura yako ni moja tu ndio unatakiwa uitumie hiyo kumzuia kwenye sanduku la kura!kura yake haikutosha kumzuia chacha bahati mbaya!chacha wangwe hakuishia hapo akamwambia mwenyekiti sasa naitaka nafasi yako!mwnyekiti akaona hii sasa balala,akaanza mikakati ya kumzuia,this time akafanikiwa!kweli chacha wangwe hakugombea uenyekiti wa chadema na hatakuja kugombea milele nafasi hiyo!

Ikawadia zamu ya zitto kumpima ubavu mwenye kigoda,kilichotokea wengi tunajua,kwani wengi humu kipindi hiki mlikua mmeshaingia chadema...rejea nini kilitokea!

Rai yangu kwa wenyeviti wa vyama mbadala hapa wanacho angalau japo kidogo cha kujifunza kutoka magamba,japo nao wana kamchezo eti ka kumuachia mwenyekiti amalize muda wake! upuuzi mtupu,hakuna demokrasia ya namna hiyo,wenyeviti wakubali kuwa tested kwenye chaguzi za ndani.Nawasilisha.
 
Lipumba alikosea njia kuingia cuf,bora angebaki ccm,asingefanya pupa mkapa ilikua ampe uwaziri kumuandaa awe rais au waziri mkuu wa Tanzania,najua wengi mtashangaa lakini huu ndio ukweli,nitaumwaga hapa siku moja,mumjue lipumba alikotokea mpaka kufika hapo alipo,kiufupi akiwa chuo kikuu yeye alikua katibu wa TANU youth league wakati jk akiwa mwenyekiti wake,na ni hapo hapo chuo kikuu ndipo walikutana na kujuana na maalimu seif aliejiunga chuoni hapo katika mpango maalum wa kuwasukuma wazanzibar....
 
Kuna mtu mmoja aliwahi kusema kuwa Njaa Haina Mchakato, nikamdharau. Duh Maswahiba leo wanafarakana ama kweli hata Compaore alikuwa swahiba wa Thomas lakini ndiye aliyemuua na kuchukua nchi na hadi leo anatawala.

Msemo wa mapanga shaaaaaa umewageukia CUF wenyewe sasa wanacharangana mchana kweuuupe! CCM bwana safi sana, ukishaingia jumba jeupe tu basi jua kinachofuata ni kufarakana. Sijui nani atafuatia katika kufarakana kwa kuwa umeandikiwa ukisikia tetesi za vita mahala mahala jua mwana wa Adamu yu karibu kuja kuwanyakuwa walio wake. Leo NCCR tetesi za vita, CUF tetesi za vita anayefuata simjui ila naona kama maono vile!
 
Lipumba alikosea njia kuingia cuf,bora angebaki ccm,asingefanya pupa mkapa ilikua ampe uwaziri kumuandaa awe rais au waziri mkuu wa Tanzania,najua wengi mtashangaa lakini huu ndio ukweli,nitaumwaga hapa siku moja,mumjue lipumba alikotokea mpaka kufika hapo alipo,kiufupi akiwa chuo kikuu yeye alikua katibu wa TANU youth league wakati jk akiwa mwenyekiti wake,na ni hapo hapo chuo kikuu ndipo walikutana na kujuana na maalimu seif aliejiunga chuoni hapo katika mpango maalum wa kuwasukuma wazanzibar....

Mkuu kwenye wekundu hapo:
  1. Siku ni leo tumwagie
  2. Ina maana Maalim hakuwa na sifa au?
 
Hamad Rashid atamuweza seif kwa kuwa wanajuana vizuri mambo mengi wamefanya pamoja,naona hamad anaona kama seif kamuacha kwenye ufalme wake na kumkumbatia yule mhindi Ismail Jussa.
 
Shughuli pevu ilikuwa leo 13/12/2011 ambapo mbunge huyo wa wawi - Pemba alikuwa na ziara nyingine katika tawi la CHECHNIA lililoko kata ya mabibo. Baada ya walinzi wa taifa na wa wilaya kuzuia shughuli ya KOSOVO inaonekana hamad rashid na wenzie walijipanga zaidi na kukodi kundi kubwa la vijana wapatao 150 ili kulinda mkutano wake wa mabibo. Majira ya saa 8.00 mchana vijana kadhaa walianza kufika ukumbi wa mkutano wengine wakiwa na makoti na wengine wakiwa na kofia za mazoezi maarufu PAMA. Wengi wa vijana hao walionekana kuwa na nyuso nzito na baadhi yao walionekana kama wamepata kilaji kidogo.


Majira ya saa 9.00 walifika hapo ukumbini(ukumbi wa kukodi) wajumbe watatu wa baraza kuu la uongozi la CUF wakiambatana na baadhi ya wanachama wanaompinga MAALIM SEIF. Walipofika ukumbini wanachama na wananchi mbalimbali walianza kukusanyika. Wakati kusanyiko linaendelea ghafla gari ya ofisi kuu ya CUF ikapaki mita 100 hivi kutoka ukumbini. Baadaye walishuka walinzi wawili wa wilaya ya kinondoni na kwenda kwenye mlango wa ukumbi kuuliza kulikoni kikao hicho kifanyike bila wilaya kupewa taarifa?


Sijakuelewa.....tarehe 13/12/2011 saa 8 au 9 mchana bado haijafika! Na stori yako hii unaelezea kitu ambacho kimeshatokea...
 
Kama sikosei huyu Hamad Rashid aliwahi kuhojiwa na vyombo vya habari kuhusu ndoa yao na CCM kwamba hawaoni inauwa upinzani? nakumbuka jibu lake lilikuwa ni hili " Hatuwezi kuwaachia nguruwe shamba wale peke yao, ni lazima tule wote" mwisho wa kunukuru.

Inaonekana Hamad Rashid yeye amezaliwa ili awe mtu wa madaraka na ulaji tu maisha yake yote, kwa sababu ninavyofahamu mimi ukiongoza mageuzi ndani ya chama basi wewe usiwe mmoja wa wale frontliner, hapa ndipo alipoishiwa busara huyu Hamad Rashid, nadhani wangeongoza harakati hizi wengine halafu wangempendekeza yeye hiyo ingeingia akilini kidogo.
 
Kama sikosei huyu Hamad Rashid aliwahi kuhojiwa na vyombo vya habari kuhusu ndoa yao na CCM kwamba hawaoni inauwa upinzani? nakumbuka jibu lake lilikuwa ni hili " Hatuwezi kuwaachia nguruwe shamba wale peke yao, ni lazima tule wote" mwisho wa kunukuru.

Inaonekana Hamad Rashid yeye amezaliwa ili awe mtu wa madaraka na ulaji tu maisha yake yote, kwa sababu ninavyofahamu mimi ukiongoza mageuzi ndani ya chama basi wewe usiwe mmoja wa wale frontliner, hapa ndipo alipoishiwa busara huyu Hamad Rashid, nadhani wangeongoza harakati hizi wengine halafu wangempendekeza yeye hiyo ingeingia akilini kidogo.

madaraka matamu kaka asikuambie mtu. Mambo mawili makuu (1) PESA na (2) MADARAKA hupambanua bayana tabia na hulka ya M2
 
Kama sikosei huyu Hamad Rashid aliwahi kuhojiwa na vyombo vya habari kuhusu ndoa yao na CCM kwamba hawaoni inauwa upinzani? nakumbuka jibu lake lilikuwa ni hili " Hatuwezi kuwaachia nguruwe shamba wale peke yao, ni lazima tule wote" mwisho wa kunukuru.

Inaonekana Hamad Rashid yeye amezaliwa ili awe mtu wa madaraka na ulaji tu maisha yake yote, kwa sababu ninavyofahamu mimi ukiongoza mageuzi ndani ya chama basi wewe usiwe mmoja wa wale frontliner, hapa ndipo alipoishiwa busara huyu Hamad Rashid, nadhani wangeongoza harakati hizi wengine halafu wangempendekeza yeye hiyo ingeingia akilini kidogo.

Kama anavyofanya EL
 
waache si waliichekea ccm?
hiki chama kimehusika na kuwaangamiza makada wake kwa mbinu chafu ili kiendelee kuiba rasilimali za nchi sembuse sisimizi cuf?

mwaka huu wataisoma.
 
Uroho wa Madaraka kwa viongozi wetu utaviua vyama vya upinzani, CCM wanamamluki kila chama ili kuvibomoa.
 
Hizi pia ni mbinu za ccm kwa kutaka kugawa kura za upinzani. Wameona Seif wamempa ulaji hivyo hana nguvu tena ya kukijenga chama. Hivyo itakuwa vigumu kwao kwa mwaka 2015 bila cuf kuwepo kuwasaidia kugawa kura za wapinzani, ndio maana wanamchochea Hamad ili anzishe vurugu kwa minajili ya kukijenga cuf tbara. Inawezekana kweli kuna fungu ccm watakuwa wamemtengea Hamad kwa ajili ya hii kazi. Sio rahisi kwa Hamad kusema atatembelea ofisi zote za cuf tbara na kununua vifaa vya ofisi. Tujiulize kwa pesa gani alionao Hamad, na siku zote alikuwa wapi katika kujenga hizo ofisi aibuke tu sasa.
 
Kwa wazalendo hasa serikali ya muungano, ni lazima watafute namna ya kujipenyeza ktk huo ugomvi wao uendelee wasahau hoja ya kujitenga na kuvunja muungano. Zanzibar wakiwa na matatizo na migawanyiko ya dhahiri, Muungano huimarika maana wote hukimbilia bara kuomba kuungwa mkono!!
 
I concur with you, na on top of that Hamad Rashid ana uchu wa madaraka, kumbuka miaka yote huko nyuma alikua anamsapoti Maalim na wakati ana madaraka Bungeni mbona alikua kimya, na hata kuingia ktk serikali "anayoita Kuolewa' na yeye anahusika big time, mi nadhani anafanya haya yote sababu kwa kipindi hiki hana madaraka, so anataka madaraka kwa nguvu zote, ni mroho sana wa madaraka huyu jamaa, na ni kweli anaweza kufa kwa ajili ya madaraka km alivyonukuliwa!GOSH
 
hizi fujo hatuzitaki huku bara. Kama ni cuf wakapiganie huko visiwani. Hasira zenu nyie viongozi mliotoka visiwani zisitusababishie matatizo humu
 
Back
Top Bottom