Halotel janga jingine

Halotel janga jingine

92mtl

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2016
Posts
459
Reaction score
309
Wandugu baada ya kuujua huu mtandao hakika nilijua nimepata mkombozi ambaye atanifanya niwe kasi hasa kwenye issue zangu za mtandao. Hii ni wiki ya tano tangu halotel mahala nilipo imeanza kusumbua hakuna cha 3g iliyotulia.

Hili tatizo si kwangu tuu, karibia watu wangu wote wa karibu eneo nililopo wananiambia inazingua yaani bora hata kobe wangu voda ambaye nasikia huko mjini ana kasi ya ajabu.

Mwanzoni mwa mwezi huu niliamua kuwapigia watoa huduma nikaambia internet iko vizuri labda sehemu nilipo ndio kuna shida, nikaahidiwa kwa niaba ya wenzangu kuwa watashughulikia hadi leo kimya. Kinachoniuma zaidi nina bonge la bundle la mwezi sasa sielewi kama.

1. Walikuja na nguvu ya soda sasa wamezidiwa?

2. Kama ni tatizo la muda ndo liwe zaidi ya wiki 3?

3. Au wamekula kidogo kitu ili wapunguze ushindani ktk soko

Ni hayo tu.

Niko mkoa mpya wa Songwe wilaya ya Ileje.
 
kuhusu halotel we nyamaza tu huyo ndo mkombozi wetu kwenye internet, kawaambie mabosi wako wa ile mitandao chakavu waendelee tu kushusha mb wafanye hata mb 50 kwa sh 1000 maana naona wehu wenu ni wa kimwendokasi
 
Kwa hapa nilipo nafurahi na voda tuu speed hadi 7Mb/s. Lkn halotel ni janga. Nikiwek mb 350 hadi zina expire. Viva voda mmenifikia japo ni ghali....
 
  • Thanks
Reactions: 7ve
Sijui mikoani ila kwa Dar Halotel no suruhisho mm nimeshasahau mitandao mingine nilichofanya nikununua simu ya line 2 na kushare Internet kwa kutumia bundle murua za Halotel.
 
Niwe mkweri. Kwangu mim halotel kwenye internet ni zero kabsa. Naweza fungua page moja ukapita dakika mbili ndo page inafunguka. Kwenye kudowload speed yake huwa inachezea 0.2kb/s speed ambayo ni ndogo mno
 
  • Thanks
Reactions: 7ve
Hiyobhali imejitokeza kwa nusu saa tu..kwa sasa imerudi hewan..
 
Niwe mkweri. Kwangu mim halotel kwenye internet ni zero kabsa. Naweza fungua page moja ukapita dakika mbili ndo page inafunguka. Kwenye kudowload speed yake huwa inachezea 0.2kb/s speed ambayo ni ndogo mno
Mbona kwangu sio shida
 
  • Thanks
Reactions: dtj
Kwakweli mpaka nimesahau laini yangu ya tigo jinsi halotel inavyonipa raha mjini hapa, tena nikiwa na stream ndo usiseme naangalia movie tu hamna kudownload sasa nyie mnaosema mtandao umezidiwa pelekeni simu zenu kwa dr matelephone, Sijui mara ya mwisho kuweka vocha tigo ilikua lini kwanza.
 
  • Thanks
Reactions: dtj
Aah mkuu kumbe halotel imefika hadi ileje kwa bibi angu,vipi imefika hadi milimani kule maana nampango wa kurudi ileje nikalime siunajua mtukufu kasitisha ajira
huku ipo kote ilikuja juu sana kitu ilikua 3gH+ saiz saiv GE 3g ya kubahatisha
 
Mimi mwenyewe sio naongea kwa kubahatisha nimetumia mitandao yote kwenye internet ila nilicho kuja kugundua halotel speed yao sio kubwa ila nikwamba inapatikana maeneo mengi hasa vijijini na inakuwa ni full 3G network ila sio kwamba ina speed kubwa watu wanadanganyika.,,nilikuja kuhakikisha hilo nilipokuja kukaa eneo ambalo mitandao yote inashika 3G network nikaja kupima speed ya internet aise Halotel anakimbizwa vibaya sana na Vodacom.
 
hongeleni lakin nimesemea eneo nililopo
 
Back
Top Bottom