Halmashauri: Moja ya chanzo cha umasikini kwa taifa

Halmashauri: Moja ya chanzo cha umasikini kwa taifa

Hatulalamiki ila uwepo wa halmashauri nyingi kumerudisha maendeleo nyuma. Pamoja na wasomi hao ma DED kumbuka maafisa mipango, wachumi, mipango miji ni wale wale wasiojituma na wezi. Yaani kwa ufupi panahitajika kufumilwa tena hasa muundo wa utumishi wa halmashauri. Mfano si ajabu mchumi kuwa hajui miradi inayoendelea kwenye halmashauri yake. Si kama enzi zile siku hizi wachumi kazi yao ni kukaa tu ofisini wala hawafuatilii miradi unakuta miradi hewa kibao. Na kibaya zaidi wafanyakazi wengi wa halmashauri siyo wabunifu wana akili mgando. Mimi nasema hayo kwa sababu nawajua. Chukua mfano mwingi, halmashauri kwa asilimia kubwa au 100% hazina policy ya majengo/miji/ etc. Unakuta wanagawa viwanja then hata huduma za jamii hazipelekwi, kila mtu anajenga anavyotaka, kumbi za starehe hazijengwi kuzuia sauti kutoka nje, nyumba hazina mpangilio wa rangi, yaani ni ovyo ovyo. Na kwa kutegema hizi halmashauri hatutakuja kufikia ulaya standard zao
Hao wote ni makada wa ccm na wizi ni jadi yenu.
 
Haya mambo hayahitaji ushabiki wala siasa, sio wakati wakuongea na kuandika sana, halmashauri zetu zimejaa wezi na pia zimeibiwa sana,.. mfanyakazi wa halmashauri anamiliki mijengo 1,2,3.... tena ya kifahari kuanzia mil 100 kuendelea huku mtaani hana biashara hata ya vitumbua.. KUFILISIWA NA JELA VINAWAHUSU HAWA WATU..
 
mkitaka kushuhudia hilo njooni H/W ya Monduli iliyokuwa chini ya Lowassa sasa iko mikokoni mwa watiifu wake pitieni idara zote ziko mikononi mwa wezi wakubwa tena chini ya famiia moja miradi yote ipo chini ya kiwango
 
Hii hoja haihitaji maneno mengi wala ubishi, ukweli uko wazi kabisa.
TANZANIA kwa sasa ni moja ya nchi masikini sana duniani na watu wake wengi kwa asilimia kubwa huishi katika umasikini mkubwa.

Inatia uchungu sana kuambiwa eti nchi yenu ipo kundi la nchi masikini kabisa na ombaomba huku mkijua kabisa hali hii husababishwa na wapumbavu wachache kwa maslahi binafsi na vimada wao.

Kiukweli moja ya chanzo kikuu cha umasikini wa taifa hili ni halmashauri zetu, watendaji wa halmashauri zote wamechangia kwa kiasi kikubwa umasikini huu, sio wakati tena wakucheka na hawa wapumbavu bali ni wakati wakuwajaza kwenye jela zetu, kuwafilisi na mwisho kuwaua kabisa.

Maneno mengi hatuyahitaji tena na tuko nje ya muda, ni wakati sasa wakutoa adhabu na hakuna adhabu nyingine zaidi ya kuwafilisi, kuwafunga jela za pembezoni na adhabu kali.
Vyomba vyote vya usalama ni mali ya serikali, Mh Rais ndio mtoa amri, sasa nini tunashindwa kuadhibu asilimia ndogo ya wapumbavu wanaoleta huu mkwamo?, watu zaidi ya mil 45 tunashindwaje na hawa wapumbavu wachache mpaka Taifa linakuwa maskini hivi.

INAKERA, eti tunaitwa moja ya taifa masikini duniani nasi tumekaa tu tumeridhika, huku wengine eti wanajiita wasomi na videgree, vimasters, viphd na wengine maprofesa sasa sijui unajiitaje msomi huku taifa lako ni masikini.
Punguza POVU mama Chiku na sabuni yako ya family detergent?

Huko Halmashauri mnakofanyia siasa ndio tutegemee itoke tija? VIMASTAZ na VIPhD si ndio juzi hapa vimeongezewa UKADA na kupelekwa huko, sasa mbona makelele mapema au hii post ni ya mwaka 2011 mimi nimejichanganya?

Hao unaowaita 'wapumbavu' hawajajiweka hapo, wamewekwa. Halafu nikukumbushe kuwa, moja kati ya mambo yanayozikwamisha serikali za Afrika ni kutozingatia utawala wa sheria. Sasa unaposema '...ndio mtoa amri' unafikiri nchi inapaswa kuendeshwa kwa amri au katiba?

Kajipange, kama jana hukupata milo mitatu unawehuka basi jipe staha. Anza kuzoea mlo mmoja kwa siku, viwanda haviji bila jasho na machozi.
 
Hatulalamiki ila uwepo wa halmashauri nyingi kumerudisha maendeleo nyuma. Pamoja na wasomi hao ma DED kumbuka maafisa mipango, wachumi, mipango miji ni wale wale wasiojituma na wezi. Yaani kwa ufupi panahitajika kufumilwa tena hasa muundo wa utumishi wa halmashauri. Mfano si ajabu mchumi kuwa hajui miradi inayoendelea kwenye halmashauri yake. Si kama enzi zile siku hizi wachumi kazi yao ni kukaa tu ofisini wala hawafuatilii miradi unakuta miradi hewa kibao. Na kibaya zaidi wafanyakazi wengi wa halmashauri siyo wabunifu wana akili mgando. Mimi nasema hayo kwa sababu nawajua. Chukua mfano mwingi, halmashauri kwa asilimia kubwa au 100% hazina policy ya majengo/miji/ etc. Unakuta wanagawa viwanja then hata huduma za jamii hazipelekwi, kila mtu anajenga anavyotaka, kumbi za starehe hazijengwi kuzuia sauti kutoka nje, nyumba hazina mpangilio wa rangi, yaani ni ovyo ovyo. Na kwa kutegema hizi halmashauri hatutakuja kufikia ulaya standard zao
Kila hatua inaanza kwa kuzingatia UTAWALA WA SHERIA. Kama UKADA ndio ngazi ya DED, mtatoa sana mifano ya ajabu ajabu mitandaoni.

Siku hizi kutoa matamko ndio ubunifu.
 
Hatulalamiki ila uwepo wa halmashauri nyingi kumerudisha maendeleo nyuma. Pamoja na wasomi hao ma DED kumbuka maafisa mipango, wachumi, mipango miji ni wale wale wasiojituma na wezi. Yaani kwa ufupi panahitajika kufumilwa tena hasa muundo wa utumishi wa halmashauri. Mfano si ajabu mchumi kuwa hajui miradi inayoendelea kwenye halmashauri yake. Si kama enzi zile siku hizi wachumi kazi yao ni kukaa tu ofisini wala hawafuatilii miradi unakuta miradi hewa kibao. Na kibaya zaidi wafanyakazi wengi wa halmashauri siyo wabunifu wana akili mgando. Mimi nasema hayo kwa sababu nawajua. Chukua mfano mwingi, halmashauri kwa asilimia kubwa au 100% hazina policy ya majengo/miji/ etc. Unakuta wanagawa viwanja then hata huduma za jamii hazipelekwi, kila mtu anajenga anavyotaka, kumbi za starehe hazijengwi kuzuia sauti kutoka nje, nyumba hazina mpangilio wa rangi, yaani ni ovyo ovyo. Na kwa kutegema hizi halmashauri hatutakuja kufikia ulaya standard zao
Unaelekea kulifahamu tatizo, swali langu linaweza kuwa-je, kwa approach hii ya kupeleka maded, maras, na madc makada inaweza kusaidia kuleta hayo mabadiliko unayoyataka? Au nibadilishe swali kidogo-unafikiri kwa kuingiza siasa na kuwaza zaidi kudhibiti wapinzani kwenye maeneo husika tunapotafuta wasimamizi wa shughuli kwenye halmashauri italeta tija?
 
Unaelekea kulifahamu tatizo, swali langu linaweza kuwa-je, kwa approach hii ya kupeleka maded, maras, na madc makada inaweza kusaidia kuleta hayo mabadiliko unayoyataka? Au nibadilishe swali kidogo-unafikiri kwa kuingiza siasa na kuwaza zaidi kudhibiti wapinzani kwenye maeneo husika tunapotafuta wasimamizi wa shughuli kwenye halmashauri italeta tija?
Tumuache rais afanye kezi
 
Kila hatua inaanza kwa kuzingatia UTAWALA WA SHERIA. Kama UKADA ndio ngazi ya DED, mtatoa sana mifano ya ajabu ajabu mitandaoni.

Siku hizi kutoa matamko ndio ubunifu.
DED lazima awe kada, kwani halmashauri zote na majiji zinatekeleza ilani ya CCM
 
DED lazima awe kada, kwani halmashauri zote na majiji zinatekeleza ilani ya CCM
Bi mdogo hebu tumia kichwa chako angalau mara moja kwa mwaka ubongo usioze. Ilani ya CCM haitekelezwi na chama peke yake. Uchaguzi ukiisha, ILANI inashika hatamu na utekelezaji wake haumaanishi watendaji wote wawe wanachama wa chama kilichoshinda.

Leo hii chama kingine kikishinda uchaguzi, wachaguliwe maDED nchi nzima (kama ilivyofanyika), nao maDED wakifika huko wilayani waanze kuondoa Maafisa Elimu wa Wilaya na Waganga Wakuu wawaweke makada wa chama chao, huo ni utendaji au upumbavu?

Shida ya kuzoea wizi wakati wa uchaguzi ndio inatupeleka huko. DED hana haja ya kuwa kada wa chama chochote kama walivyo polisi (kwenye nchi huru). Unaposema halmashauri zinatekeleza ilani ya CCM, vikao vya madiwani huwa vinapelekewa hiyo ilani? Haya tuone basi hiyo ilani ya CCM inavyotekelezwa Arusha na Dar...labda kwa matamko na kutumbua majipu madogo madogo.
 
Ukiacha report za CAG,mfano halisi injinia wa maji wa wilaya,wilaya labda inapakana na mto au ziwa au bahari lakini wilaya yake wananchi wanakosa maji,ameshindwaje kutumia elimu yake kuona tu kwamba kwa wananchi wanaweza kuchimba njia ya kulaza bomba la maji kutoka kwenye chanzo mpaka makao makuu ya wilaya na serikali ijenge mfumo wa kutakatisha ayo maji anashindwaje kutoa ata Ushauri wakuondoa kero ya maji kwa mbinu mbadala.

Kwa kifupi hili umaskini uondoke tz lazima wafanyakazi wa serikali mindset yao ibadilike hiwe kama ya wafanyakazi wa private sector na nivizuri serikali ijifunze sekta ya binafsi wafanyakazi wake wanafanyaje kazi na raslimali chache walizo nazo kuzalisha na pia mfanyakazi awe anapimwa kutokana na utendaji wake.Pia kuwe na tume huru ya ajira isiyo ingiliwa na vimemo au ukada kama mtu anauwezo anajiriwa kutokana na uwezo wake ukiambatanishwa na veting huru.
 
Mahakama zipo kwa ajili yetu mkuu,ni vema tukazitumia ipasavyo kuliko kuja na lawama,kusanya ushahidi,funga hayo majizi na ikibidi filisi majambazi yote ya mali ya umma ukizingatia kuwa Mahakama ya ufisadi imeshaanzishwa kwa tamko la Mkuu wa Kaya
 
chanzo cha umaskini wa taifa hili ni wale jamaa tu basi acheni kuzunguruka
 
Back
Top Bottom