kimatire
JF-Expert Member
- Nov 27, 2008
- 371
- 94
Katika hali isiyo ya kawaida Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam haina budi kuzuia magari kuingia katika eneo lote la maduka Kariakoo na Katikati ya Jiji –( City Centre) siku za mwisho wa wiki yaani Ijumaa,Jumamosi na Jumapili.Kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa 12 jioni kuwe na utaratibu wa kutokuruhusu magari au vyombo vyote vya moto kuingia katika maeneo hayo.
Hatua hii ni ya muhimu sana itasaidia kukabiliana na msongamano wa magari wakati wa shopping,Pia kupunguza walau kiasi cha hewa ukaa ndani ya Jiji.Pia itatoa fursa kwa waenda kwa miguu kuwa na wasaa mzuri wa kutembea na kutumia usafiri usio na uharibifu wa mazingira (Baiskeli na wala siyo pikipiki.)
Taratibu chache tu zitawekwa na zingine kubadilishwa.Naamini jambo hili linawezekana na litawajengea mazoea wakaazi wa Jiji kufanya mazoezi ya kutembea kwa miguu au hata kuendesha baiskeli.Kutapunguza matumizi ya kuwafanyisha askari wetu kazi za ziada.
Pia ni muhimu sana kwa mamlaka husika kuwadhibiti wafanya biashara ndogo ndogo ambao nao ni kero namba mbili wasipange bidhaa zao barabarani ili kutoa nafasi ya waenda kwa miguu kuwa na fursa nzuri ya kutembea.
Hatua hii ni ya muhimu sana itasaidia kukabiliana na msongamano wa magari wakati wa shopping,Pia kupunguza walau kiasi cha hewa ukaa ndani ya Jiji.Pia itatoa fursa kwa waenda kwa miguu kuwa na wasaa mzuri wa kutembea na kutumia usafiri usio na uharibifu wa mazingira (Baiskeli na wala siyo pikipiki.)
Taratibu chache tu zitawekwa na zingine kubadilishwa.Naamini jambo hili linawezekana na litawajengea mazoea wakaazi wa Jiji kufanya mazoezi ya kutembea kwa miguu au hata kuendesha baiskeli.Kutapunguza matumizi ya kuwafanyisha askari wetu kazi za ziada.
Pia ni muhimu sana kwa mamlaka husika kuwadhibiti wafanya biashara ndogo ndogo ambao nao ni kero namba mbili wasipange bidhaa zao barabarani ili kutoa nafasi ya waenda kwa miguu kuwa na fursa nzuri ya kutembea.