Mbunge wa kawe halima james mdee amesema kuwa chama chake na BAWACHA wanajiandaa kuingia msituni sio kupigana bali wanaingia msitu kwa msitu, poli kwa poli na kijiji kwa kijiji ili kwa muda wa Miezi miwili ili kuhakikisha CHADEMA inasonga mbele na kuenea Tanzania nzima ili kuitoa CCM madarakani.
Amesema kuwa wanawake na vijana wanamuamini hivyo atawaongoza Vizuri na hatawaangusha na wameshafanya kikao tayari na kupanga ratiba ya ziara ili kumkomboa mtanzania.
Chanzo: Habari ITV