Hali za hospitali zetu

Hali za hospitali zetu

measkron

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2011
Posts
3,782
Reaction score
2,418
Hospitali ya mkoa Ruvuma wodi ya wajawazito uwezo wake ni vitanda 70, kuna kina mama zaidi ya 200 wanalala nje, ndani hapatoshi na mvua ikinyesha wananyeshewa, jiko dogo wanapika nje, wengi hutokea jimbo la Namtumbo kwani hakuna huduma ya dharura kwa wajawazito... Source TBC News saa 2. My take: vipaumbele ni vipi kama twaweza kuadhimisha miaka 50 ya uhuru kwa pesa nyingi huku tukishindwa kujali huduma muhimu? Viongozi wetu wana mawazo gani ili kuboresha huduma za kijamii?
 
Kama nakumbuka vizuri kuna wakati Mwanakijiji alikuwa na effort ya kuongeza vitanda kwa wagonjwa. Sijui iliishaje. Sio lazima kila kitu kiachwe kwa serikali, especially kama serikali yenyewe hopeless.

Tunafanya nini kusaidia wagonjwa kama Watanzania?
 
Wabunge wao hawana habari nao.Wanafikiria kujiongezea posho tu.Sijui nini msimamo wa mbunge wa Namtumbo Vita Kawawa kuhusu posho wakati mama na dada zake wanajifungulia mavumbini kama panya!
 
Wabunge wao hawana habari nao.Wanafikiria kujiongezea posho tu.Sijui nini msimamo wa mbunge wa Namtumbo Vita Kawawa kuhusu posho wakati mama na dada zake wanajifungulia mavumbini kama panya!

Mkuu ninadhani hili hii sio kwa Namtumbo pekee, kule Simanjiro hawana hospitali ya wilaya kina mama wajawazito hulazimika kwenda Hospitali ya Mkoa Kilimanjaro, Mawenzi, kulingana na jiografia ya Simanjiro. Nina ndugu yangu anafanya kazi huko Mawenzi hospitali ananijuza chumba cha upasuaji kilifungwa tangu 27/12/2010, karibu mwaka sasa. Ingependeza kama wanahabari wengine wangeiga mfano wa Ruvuma na kuonyesha mikoa mingine hali ikoje. Serikali legelege, viongozi legelege, maamuzi legelege.
 
Kama nakumbuka vizuri kuna wakati Mwanakijiji alikuwa na effort ya kuongeza vitanda kwa wagonjwa. Sijui iliishaje. Sio lazima kila kitu kiachwe kwa serikali, especially kama serikali yenyewe hopeless.

Tunafanya nini kusaidia wagonjwa kama Watanzania?
Tunalipa kodi kwa serikali ambayo nayo hupaswa ku-provide better services kwa wananchi! Je ndicho kinachofanyika? Kodi hatulipi? Kama tunalipa, hazitoshi? Kama zinatosha, zinatumikaje? Jibu= kujiongezea posho, sherehe za 64bn/-, safari za nje zisizokuwa na tija nk nk.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Hospitali ya Mkoa Iringa imesimamisha huduma za kawaida kwani serikali (hazina) haijapeleka fedha MSD za kutosha kwa miezi mitatu mfululizo. Hospitali ilikuwa inapokea kiasi cha mil 33 kwa mwezi kwa ajili ya madawa , lakini tangu Sept 2011 imepeleka mil 28 tu. Hospitali imeshindwa kujiendesha kama kawaida. Huduma ni kwa zile za dharura tu. (Emergencies)
 
wabunge wasipolipwa posho for one day only ..vitanda vinanunuliwa na hospitali inaongezwa...nani wa kuwafunga kengele? ZITTO??
 
hospitali ya mkoa iringa imesimamisha huduma za kawaida kwani serikali (hazina) haijapeleka fedha msd za kutosha kwa miezi mitatu mfululizo. Hospitali ilikuwa inapokea kiasi cha mil 33 kwa mwezi kwa ajili ya madawa , lakini tangu sept 2011 imepeleka mil 28 tu. Hospitali imeshindwa kujiendesha kama kawaida. Huduma ni kwa zile za dharura tu. (emergencies)

kwani watu walikuwa wanatibiwa bure?
 
Upinzani Mi naona ni nzuri sana! Ntarudi baadae kidogo! Maana naona hp mtaani kama kuna kelele ambazo siyo!
 
Hospitali ya Mkoa Iringa imesimamisha huduma za kawaida kwani serikali (hazina) haijapeleka fedha MSD za kutosha kwa miezi mitatu mfululizo. Hospitali ilikuwa inapokea kiasi cha mil 33 kwa mwezi kwa ajili ya madawa , lakini tangu Sept 2011 imepeleka mil 28 tu. Hospitali imeshindwa kujiendesha kama kawaida. Huduma ni kwa zile za dharura tu. (Emergencies)

....Dah!!! Halafu wanaenda kuunguza bilioni 64 kwa sherehe tu!!!! Na kisha kuja na kauli potofu kwamba tumethubutu, tumeweza na tunasonga mbele!!!!!
 
Kumbe tunajua serikali yenyewe ni hopeless? Why do we keep voting it in? Mi nadhani sie wenyewe ndo tuna tatizo! Inafika wakati tuvune tulichopanda manake hatujifunzi kutokana na makosa. Hao wamama wanaojifungua nje kwenye mvua walimchagua rais wao,ndo anawatumikia hivyo!
Kama nakumbuka vizuri kuna wakati Mwanakijiji alikuwa na effort ya kuongeza vitanda kwa wagonjwa. Sijui iliishaje. Sio lazima kila kitu kiachwe kwa serikali, especially kama serikali yenyewe hopeless.

Tunafanya nini kusaidia wagonjwa kama Watanzania?
 
Kumbe tunajua serikali yenyewe ni hopeless? Why do we keep voting it in? Mi nadhani sie wenyewe ndo tuna tatizo! Inafika wakati tuvune tulichopanda manake hatujifunzi kutokana na makosa. Hao wamama wanaojifungua nje kwenye mvua walimchagua rais wao,ndo anawatumikia hivyo!


....Dr nakubaliana nawe lakini pia mimi nadhani katika uchaguzi uliopita hakushinda huyu ila walitumia vyombo vya dola kuchakachua uchaguzi kwa kiwango cha kutisha, kwenye uchaguzi wa Rais na Wabunge.
 
Jamani inabidi ifike kipindi tuanze kudeal na wabunge wetu hata kwa kuwapiga au hata kuharibu ili mradi wajue majukumu yao maana kila kitu tunalaumu serikali bila kuangalia ngazi ya serikali ya kuwajibisha.

 
Back
Top Bottom