Hali ya Usafiri na Wasafiri BRT ni mbaya mno. SUMATRA Mpo Wapi?

ibanezafrica

JF-Expert Member
Oct 23, 2014
7,261
6,543
Kwa hali niliyoshuhudia nilipopanda basi la Gerezani kuelekea Kimara ni ya kusikitisha sana, Kituoni Gerezani abiria waliosubiria gari kwa muda mrefu wamejazana pale miongoni mwao ni wa mama wenye watoto wadogo, wazee na wanafunzi, hatimaye linakuja basi kupakia ilihali ndani wamo abiria waliozunguka nalo!

Kwa vile watu wamechoka kusubiri kituoni wanaamua kuvamia hivyo hivyo basi linajaa kupita maelezo, basi linafika kituo cha msimbazi kundi lingine kubwa linavamia basi na mpaka milango kushindwa kufunga! Hii ni hatari sana, basi linafika kituo cha faya na vingine vifuatavyo kuna wanaolazimisha kuingia ndani wanashindwa na kuna wanaotaka kushuka wanashindwa! Watoto wadogo wanalia kwa kuminywa na tulisikia kuwa hivi karibuni kuna mama mwenye presha alianguka ktk kusukumana akakimbizwa muhimbili maana alianguka presha ikapanda.
Nachoshangaa Sumatra hawaoni shida hizi wao wakiwa wadhibiti na wasimamizi wa vyombo vya usafiri majini na nchi kama?

Au usafiri wa mwendo kasi hauwahusu? Tafadhali Sumatra hatua za haraka zitafutwe kuondoa usumbufu huu.
IMG_20180703_161543.jpg
 
Kwani hvi magari ya mwendokasi yapo Sita hv kwanini wasiongeze magari
 
Hamna mradi wowote ulioanzishwa na CCM ukawa Na matokeo mazuri.
1. Uwanja wa uko mekemeke hope hae, umekongoroka.
2. Ndege ni hasara Kila kukicha
3. Mwendokasi ni majanga
4. Hostel za UDSM Mlimani City ni full expansion joints
5. Standard Gauge imesha anza kuzingua Huko wilayani Bagamoyo
6. Barabara mpya zinafumuliwa na kuanza kujengwa upya
Yaani hakika TUNALALA KWA HUZUNI KAMA TULIVYOAMBIWA kwenye Isaya 50:11
 
Kwa hiyo picha mbona haionyeshi watu kuwa wengi au kuwa pamejaaa na wamechoka na hakuna msongamano unaodai.. bali hao wawili watatu wanasubiri kwa uamuzi kupanda basi lingine..

Utakuwa msafiri wa siku moja unalalamika ambacho haukielewi mwenyewe.. ndio ingekuwa imetokea jana juzi tungekusikia..

Ya huyo Mama ulisikia ukuona.. kumbuka watu wana magonjwa na popote lolote linatokea hata majumbani mwao

Unasema milango haifungi ila nasoma unaandika mnafika kituo kinachofata.. duh

Ungeona maisha ya nchi zilizoendelea wakati wa mida ya kukimbizana basi ungelala kituoni kabisa weye au kurudi ulipotoka.. na maisha yao yanasonga mbele.. hicho kipicha chako kinatia aibu kuandika malalamiko
 
Back
Top Bottom