Rare Sapphire
JF-Expert Member
- Jul 24, 2021
- 576
- 1,626
Wakuu,
Naamini wote tunaenda saluni, iwe kusuka au kunyoa, na huduma hii sio kwa watu watu wazima pekee hata watoto pia huenda saluni kutengenezwa nywele, sasa swali ni kwamba hali ya usafi ikoje kwenye saluni unayoenda kupata huduma?
Wanaume, mataulo yanayohudumia wateja yanasafishwa baada ya muda gani? Au ni mwendo wa kukung'uta tu baada ya kumhudumia mteja halafu mwengine anatumia hilohilo? Kwenye vifaa angalau upande wa wanaume wanasafisha na spirit ama sanitaiza japo nayo sijui inaondoa wadudu/uchafu kwa kiasi gani.
Machanuo, mikasi, taulo, sindano nk, kwenye saluni za kike zinasafishwa kabla hajatumia mtu mwingine? Tukumbuke vifaa vinavyotumika vina ncha kali na ni rahisi sana kumuambukiza mtu ugonjwa.
Saluni yako vipi, usafi ni wa hali ya juu au tunamuachia Mungu?
Naamini wote tunaenda saluni, iwe kusuka au kunyoa, na huduma hii sio kwa watu watu wazima pekee hata watoto pia huenda saluni kutengenezwa nywele, sasa swali ni kwamba hali ya usafi ikoje kwenye saluni unayoenda kupata huduma?
Wanaume, mataulo yanayohudumia wateja yanasafishwa baada ya muda gani? Au ni mwendo wa kukung'uta tu baada ya kumhudumia mteja halafu mwengine anatumia hilohilo? Kwenye vifaa angalau upande wa wanaume wanasafisha na spirit ama sanitaiza japo nayo sijui inaondoa wadudu/uchafu kwa kiasi gani.
Machanuo, mikasi, taulo, sindano nk, kwenye saluni za kike zinasafishwa kabla hajatumia mtu mwingine? Tukumbuke vifaa vinavyotumika vina ncha kali na ni rahisi sana kumuambukiza mtu ugonjwa.
Saluni yako vipi, usafi ni wa hali ya juu au tunamuachia Mungu?