Mangi wa Rombo
Senior Member
- Sep 25, 2014
- 172
- 104
Habari wana JF!
Nafahamu kumekuwa na ripoti nyingi za uharibifu wa miundombinu kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha, lakini leo ningependa nilete jukwaani hapa hali ya kiunga kati ya Mbopo na Bunju, kutoka kata ya Mabwepande, wilaya ya kinondoni.
Kwa sasa hakuna mawasiliano kabisa kufuatia kukatika kwa kiunga hichi kilichopo mbele kidogo baada ya mbopo center eneo maarufu "mabanda ya kuku"
Kibaya zaidi ni kwamba shule ya kata na zahanati zipo upande wa mbopo hivyo wagonjwa na watoto wanahatarisha maisha kwa kupita juu ya bomba la Dawasa kama inavyo onekana hapo kwenye video!
Juhudi za kupata hata daraja la muda la waenda kwa miguu zimegonga mwamba!
M-bunge wa jimbo la Kawe,Mh Josephat Gwajima amekuwa mwenye kukwepa kukutana na wananchi wa eneo hili, na amekuwa akitoa ahadi hewa bila utekelezaji! Hili ni jimbo ambalo yeye mwenyewe kupitia ukurasa wake wa Instagram alipost video ya Mh Makonda akitoa ahadi ya magreda 20 lakini mpaka leo hata greda moja halijaonekana.
Watoto wako hatarini, inapotokea wako shule na mvua ikanyesha bhasi wanakaa upande wa pili hadi maji yapungue kisha wanapita juu ya bomba!
Miaka 63 ya Uhuru bado kuna kata hapa Dar haina kiunganishi na watoto wanabebwa mabegani.
TARURA wanajua juu ya eneo hili ila hawajawahi kutoa majibu! Ofisi ya Mkuu wa Wilaya inayo taarifa!
Swali ni je, mnasubiri hadi mtu apoteze maisha au kuumia ndo mchukue hatua?
#Jamiiforums tusaidieni kupaza sauti
Nafahamu kumekuwa na ripoti nyingi za uharibifu wa miundombinu kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha, lakini leo ningependa nilete jukwaani hapa hali ya kiunga kati ya Mbopo na Bunju, kutoka kata ya Mabwepande, wilaya ya kinondoni.
Kwa sasa hakuna mawasiliano kabisa kufuatia kukatika kwa kiunga hichi kilichopo mbele kidogo baada ya mbopo center eneo maarufu "mabanda ya kuku"
Kibaya zaidi ni kwamba shule ya kata na zahanati zipo upande wa mbopo hivyo wagonjwa na watoto wanahatarisha maisha kwa kupita juu ya bomba la Dawasa kama inavyo onekana hapo kwenye video!
Juhudi za kupata hata daraja la muda la waenda kwa miguu zimegonga mwamba!
M-bunge wa jimbo la Kawe,Mh Josephat Gwajima amekuwa mwenye kukwepa kukutana na wananchi wa eneo hili, na amekuwa akitoa ahadi hewa bila utekelezaji! Hili ni jimbo ambalo yeye mwenyewe kupitia ukurasa wake wa Instagram alipost video ya Mh Makonda akitoa ahadi ya magreda 20 lakini mpaka leo hata greda moja halijaonekana.
Watoto wako hatarini, inapotokea wako shule na mvua ikanyesha bhasi wanakaa upande wa pili hadi maji yapungue kisha wanapita juu ya bomba!
Miaka 63 ya Uhuru bado kuna kata hapa Dar haina kiunganishi na watoto wanabebwa mabegani.
TARURA wanajua juu ya eneo hili ila hawajawahi kutoa majibu! Ofisi ya Mkuu wa Wilaya inayo taarifa!
Swali ni je, mnasubiri hadi mtu apoteze maisha au kuumia ndo mchukue hatua?
#Jamiiforums tusaidieni kupaza sauti