Hali ya kisiasa mkoani Kigoma

Hali ya kisiasa mkoani Kigoma

si huyo ndo mnataka awe rais wa tanzania wakati kwake tu kumemshinda? maslia naomba waseme kitu hapa
 
Fahamu kuwa muda ni kitu kizuri kukitumi, na fikiri umesoma vema mada husika kama muwasilisha mada alivyo elezea, lakini ni kweli watanzania wa leo tunahitaji kujua kuna ofisi ngapi kwenye jimbo la zitto kabwe? na kwanini zitto kabwe wakati hapa nilipo Iringa kwa Msigwa hakuna hata hizo ofisi pia za chadema.

Nafikiri tusiwe tunapoteza dhana ya kujenga taifa hili kwenye mambo ya siyo na msingi ccm wana ofisi kila mtaa, kila kijiji kila kata, wilaya na mikoa lakini still ndani ya miaka hamsini ya utawala wao hakuna jambo lolote la msingi walilo lifanya zaidi ya kutuibia bila sababu za msingi.

Pia na fikiri mtoa mada si mfatiliaji wa sera za chadema kuwa mbunge wa chadema ni muwakilishi wa watanzania wote hivyo kama ofisi haipo kigoma kaskazini basi hizo nyingine zinatosha, chama kichanga kama chadema hakiwezi kwa muda huu kuwa kila lipa gharama kwa wahudumi wake wote nchi nzima.

Mwisho nafikiri unafahamu kuna kitu kinaitwa M4C je umesha fatilia dhumuni lake? kama hujafanikiwa kufanya hilo then ni vema ukafatilia sasa, lakini kukuhabarisha tuu chadema kuanzia makao makuu hawana jengo lao kama chama ndio maana wanapita kuchangisha michango Tanzania nzima kuweza kupata pesa za kujenga chama kutoka kwenye mashina mpaka ngazi ya taifa so kuliko kuongea kwa kejeli kuhusu mtu toa mchango wako kujenga chama hiki kwa ajili ya kizazi hiki na kinacho kuja na si kupiga soga na majungu this is what we shall do kwa maendeleo ya nchi hii.

Hope umenisoma
 
maana yake nini sasa tupe mwongozo mkuu

Wadau;
Mnahitaji nini hapa kujua mada hii inamhusu nani wakati mimi kwa uelewa wangu hapa anayezungumziwa ni Zitto Z Kabwe. Kiukweli ni kwamba Chadema kanda ya Kigoma, Tabora na Rukwa iko hoi sana wakati jamaa kwa nafasi yake na ushawishi alionao kama kweli angekuwa anafanya kazi kama inayofanywa na Godbless Lema, Vincent Nyerere n.k sasa hivi Kanada hiyo kusingekuwa na ccm kabisa.

Kwa kweli hapo kuna jambo na yangu ni masikio na macho kuzidi kusikia na kuona mengi hasa yaliyomo katika undani wa jamaa huyu tunapoelekea 2015.

Naomba kuwasilisha.
 
Bora 2015 Chadema iwe haina jimbo Kigoma ili tuzungumze mengine
 
duh..unataka kuxema hata urais tutapata taabu xana hata huko nyumbani kwa rais kijana tarajiwa?
 
Habar ya mkuu PREZZO! unasema hivyo kwakuwa umetangaza kutokugombea ubunge 2015, ?

prezzo ni latin au greek word

pia inaweza kuwa muundaji wa hili jina prezzo alijaribu kumaanisha ufanana na neno president
 
<b>wabunge</b> (NCCR-4,CCM-3,CHADEMA-1 (Kigoma Kaskazini))<br />
<br />
<b>kigoma kaskazini</b><br />
<br />
1. Hakuna ofisi ya jimbo, inafunguliwa uchaguzi ukikaribia na inafungwa uchaguzi ukiisha.<br />
2. Chadema ina madiwani 2 kati ya 10
so what?
labda kuna kitu ulitaka kusema, hilo kila mtu analifahamu, naweza kusema kajipange upya
 
Jamaa ananafsi za kibinafsi sana anashindwa hata na kgm manispaa chadema inaongoza kwa miaka 15 sasa,
 
Mi sijakuelewa mkuu,unazungumzia hali ya kisiasa kigoma (kama mkoa),au unazungumzia hali ya kisiasa ya CDM kigoma,au unazungumzia hali ya kisiasa kigoma kaskazini???
Yawezekana unahoja lakini hiyo mistari miwili haijabeba content ya kile unachoazimia kusema.
Funguka zaidi tukuelewe vizuri.
 
hata matokeo ya 2010 yenyewe mbona Zito aliponea tundu la sindano?huyu jamaa hakubaliki hata kwao.
 
Hoja dhaifu kama hizi huwa hazina nguvu yoyote huko kigoma kaskazini hata kama zitto asifike kwa miaka yote yeye ataendelea kuwa mbunge mpaka achoke yeye.

Hivyo kuwe na ofisi ya chadema au kusiwe na ofisi yeye si shida na fikiri mtoa mada bado hujaweza kutengeneza hoja yako vema.

Ni vema kwa mtanzania kuongea mambo muhimu ya kujenga nchi hii na si kuwa na hoja za kwenye vijiwe vya kahawa kisha unaleta kwenye kadamnasi hii.

Kama anazuia kukuwa kwa chama Kigoma Kasikazini huyu prezzo anathibitisha ni mbunge aliyeshuka kwa kura nyingi toka uchaguzi wa 2005 kumbe anaua chama hata anakotoka uchawi wake umejikita kwenye roho mbaya
 
Bora 2015 Chadema iwe haina jimbo Kigoma ili tuzungumze mengine

Kwani itakuwa ajabu si utakuwa unaendeleza yale ya 2010 lakini 2015 hata hao wa kwenu wamekujua ndio maana hata akina machali walikugomea kila mtu amekujua hata huko kwenu kwamba wewe ni malaya wa kisiasa
 
Huwa ninacheka sana nikiona hali ya kisiasa ya Chadema kwenye jimbo la Kigoma Kaskazini.

Mara nyingi ninajaribu kulinganisha na uimara wa Chadema kwenye majimbo ya Arusha Mjini,Musoma mjini,Karatu,Hai na Ubungo.

Haya mambo ndiyo maana wakati mwingine yanatupa wasiwasi na tunashindwa kuaminiana.

Mkuu Molemo karibu jamvini.Wakati wa Mjadala wa Mnafiq Zitto nilikuona uko kwenye list ya guest ukifuatilia mjadala kwa umakini. Zitto ameiua Chadema Kigoma
 
Last edited by a moderator:
Kata yake sasa hivi bendera za ADC tu; honestly CDM ni kama imekufa KGM sasa hivi. Huenda mkakati uliokuwa unaendelea ni issue ya CHAUMMA, nashindwa kufuatilia bila kujiexpose sijaaga kwetu mwenzenu.
 
Hoja dhaifu kama hizi huwa hazina nguvu yoyote huko kigoma kaskazini hata kama zitto asifike kwa miaka yote yeye ataendelea kuwa mbunge mpaka achoke yeye.

Hivyo kuwe na ofisi ya chadema au kusiwe na ofisi yeye si shida na fikiri mtoa mada bado hujaweza kutengeneza hoja yako vema.

Kisha kuna mbunge mmoja wa chadema na ndio yeye peke yake kwenda kwake kuna barabara safi na bora sifahamu hao wengine walio wengi wamefanya nini kwenye majimbo yao.

Ni vema kwa mtanzania kuongea mambo muhimu ya kujenga nchi hii na si kuwa na hoja za kwenye vijiwe vya kahawa kisha unaleta kwenye kadamnasi hii.

Tayseer
Maoni yako ni yako. Lakini nimeguswa na vitu viwili:

Kwanza ni dharau kwa wapiga kura wa Kigoma Kaskazini kwamba umeshawachagulia mfalme - maana sidhani Kama ni mawazo yao!

Pili kwamba barabara zuri tu linakwenda jimboni kwake Kigoma nzima ambayo imejengwa na Serkali ilipaswa kuibua hisia za upendeleo, kwani Kigoma siyo wa jimbo hilo tu wanaolipa kodi.

lakini pia Cilicia katika mgawanyo huo wa wabunge na madiwani wanaowakilisha wananchi wa Kigoma ni yupi ana nguvu na anaweza kujitapa kuwakilisha wananchi wa Kigoma?
 
Back
Top Bottom