EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,483
- 15,308
Yamekuwa yakisemwa hapa kwa muda mrefu lakini baadhi ya watu wakawa wanapinga. Katika ripoti yake CAG amedhibitisha kuwa kutolewa kwa fedha pungufu ya bajeti iliyoidhinishwa kumesababisha matatizo makubwa kwa balozi zetu katika kumudu gharama za uendeshaji ikiwa ni pamoja na kushindwa kutekeleza majukumu ya kufanikisha shughuli za diplomasia ya uchumi.
CAG ametoa mfano kuwa wakati wa ukaguzi walikuta baadhi ya maofisa wa balozi za Tanzania katika nchi za China na Italia ambao hawajarejea nchini kutokana na ukosefu wa fedha, licha ya kumalizika kwa muda wao wa kazi vituoni.
Pia CAG amesema baadhi ya balozi zimeshindwa kuendeleza viwanja kutokana na uhaba wa fedha. Tatizo hili limekuwepo kwa muda mrefu sasa licha ya kulitolea taarifa kwenye ripoti yangu ya mwaka jana, alisema na kutaja baadhi ya vituo hivyo kuwa ni London, Dubai, Kigali na Msumbiji.
Aidha, amesema matumizi ya ziada kupitia maduhuli yaliyokusanywa na ofisi za balozi zinazokusanywa katika balozi za Tanzania hazisimamiwi kwa ufanisi. Amesema mlipaji mkuu wa serikali anatakiwa kusimamia fedha hizo ambazo zinasababisha kuwepo kwa matumizi ya ziada na yasiyoridhisha.
Kutokana na kasoro hizo, Sh. 3,013,732,776 zimetumika nje ya bajeti iliyoidhinishwa na Bunge.
CAG ametoa mfano kuwa wakati wa ukaguzi walikuta baadhi ya maofisa wa balozi za Tanzania katika nchi za China na Italia ambao hawajarejea nchini kutokana na ukosefu wa fedha, licha ya kumalizika kwa muda wao wa kazi vituoni.
Pia CAG amesema baadhi ya balozi zimeshindwa kuendeleza viwanja kutokana na uhaba wa fedha. Tatizo hili limekuwepo kwa muda mrefu sasa licha ya kulitolea taarifa kwenye ripoti yangu ya mwaka jana, alisema na kutaja baadhi ya vituo hivyo kuwa ni London, Dubai, Kigali na Msumbiji.
Aidha, amesema matumizi ya ziada kupitia maduhuli yaliyokusanywa na ofisi za balozi zinazokusanywa katika balozi za Tanzania hazisimamiwi kwa ufanisi. Amesema mlipaji mkuu wa serikali anatakiwa kusimamia fedha hizo ambazo zinasababisha kuwepo kwa matumizi ya ziada na yasiyoridhisha.
Kutokana na kasoro hizo, Sh. 3,013,732,776 zimetumika nje ya bajeti iliyoidhinishwa na Bunge.