Aliona balaa lililokuwa mbele yetu ndo maana alitulilia mpaka dakika ya mwisho ya uhai wake.
Aliona kuwa tangu vijana wake waamue kwenda Zenji kurekebisha azimio la arusha baas watanzania watateseka mno.
Lakini kwa umoja, udugu na ujasiri aliotupatia tutautumia kuamua hapo oktoba 31 kwamba tuendelee kuteseka au tubadili uongozi na kuweka wanaotujali zaidi.
Sio kazi rahisi kuuondoa mbuyu njia panda. lakini ukishaondoka njia inakuwa nyeupee kupitika
...alituambia ili Nchi iendelee inahitaji vitu vinne, WATU, ARDHI, SIASA SAFI na UTAWALA BORA.
..alisema kipindi cha Utawala wake adhabu waliopewa Mafisadi na Wala Rushwa ilikuwa ni mbali ya kwenda Jela lkn pia mtuhumiwa atachapwa viboko 12, 6 wakati anaingia Jela na 6 wakati anatoka akamuonyeshe Mkewe...
...alisema Mtu ambaye anajiandikisha kupiga kura halafu siku ya uchaguzi haendi kupiga kura ni MPUMBAVU.!!!
Najua kutokana na kiwango kibaya cha masomo Bongo, watu hata wale unaodhania kidogo wameelimika , kama wale wanaochangia humu, huonesha dhahiri kiwango kibovu cha elimu. Mfano nimesoma mchango wa mtu anayeandika laisi (rahisi au rais),hatali, aluki (haruki), lizika (ridhika), galama (gharama) n.k. Ajabu ni kuwa mara nyingi hawafanyi makosa hayo wanapoandika Kiingreza! Nataka kumsahihisha Kivumah juu ya kauli mbiyu ya zamani ya TANU. Ili tuendelee....' ya mwisho ni UONGOZI BORA na si UTAWALA BORA. Katika Kiswahili, tofauti ya utawala na uongozi ni kubwa. Utawala ni ule unaofanywa na mgeni juu ya wazalendo. Iwapo mtawala ni mzalendo, yeye huitwa kiongozi na 'utawala wake' huitwa uongozi. Vijana wa siku hizi hawapambanui kati ya haya. Utawakuta wanasema, utawala wa Kikwete!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.