Hali tete Masasi

Hali tete Masasi

Hapo pekundu: Hata vyombo vya habari vikinyamzishwa JF ipo na wapasha habari wenye uchungu na wananchi wapo. Lazima kitaileweka.
Kama wewe ulihusika kuhamasisha uchomaji moto miundombinu ya serikali wewe sema tu na utatembelewa.
 
Pinda ni muongo pia ni mnafiki, mlimwaminije?
Simamieni na kupigania haki zenu na uhuru wa watu wenu, CCM na Pinda msiwasikilize. Walishasema Wana-mtwara ni wahuni na wahalifu na ndivyo wanayoamini.

Big Show, what's in your locker comrades?
 
Unajua yanayokea Misri sasa ? so called peoples power nje ya kura ni uhaini tu... na dawa yake inapatikana baada ya mudamfupi...Misri is a good case study ... Tunis same..Syriaa same.

Mapenzi ni ugonjwa mbaya sana!!
Wtu wanaipenda CCM....hadi wakuwa wajinga..!! Egypt kulikuwa na Dikteta akatolewa kwa nguvu ya umma..kaingia dikteta naye sasa hivi anashugulikiwa kwa nguvu ya umma pia!

Huoni sisi tulimtoa mkoloni mwingereza....Alieingia TANU/CCM katugeuka nae tuna mchenjia....akija CDM akaja kuboronga nae anachenjiwa tu.....
Mapambano huwa hayaishi........nani alikuambia duniani kuna kupumzika!!!???
 
Walipochoma moto mali za umma na za watu wengine walitegemea nini? waiteni waliowashawishi wawasaidie walau kutumikia mahabusu.wajinga ndio waliwao.Viongozi wenu wengi wanakula bata tu huku wananchi waliodanganywa wanateseka.Safari hii lazima watafungwa wengi sana liwe fundisho kwa wengine.
 
Ukombozii haukuja kirahisi, hayo ni mapito tu, baadaye watakuta wale wenye kadi za magamba ndo wanahatarisha amani. tupo nyuma yenu
 
Huu ni mtego maarufu wa CCM, nadhani bado una nafasi ya kufanikiwa miongoni mwa jamii yetu!![/QUOTE Ukiungana na mtaji mkuu wa watawala, yaani ujinga wa walio wengi. Safari bado ipo ingawa haina siku nyingi.
 
Tuition kwa RAIA! maana wengine wakiambiwa serikali ni mbaya , hata hawasikii !!!
 
Tunaposema Tanzania haijawa huru, mijitu mingine hata haielewi.Sasa tunatafuta ukombozi wa pili wa taifa letu.Miungundu!
 
Nabaki JF humuhumu mpaka nisikie tamko\msimamo wa CHADEMA taifa kuhusu ujambazi huu.
 
Ndugu zangu Watanzania,
Kumfundisha mtu mzima na mwenye kushika madaraka kitu cha kufanya pale anapokosea si matusi, wala sio dhihaka, ni hekima. Wakati umefika sasa tumsaidie Rais Kikwete cha kufanya. Kwamba gharama za kuweka maswahiba katika madaraka wasio na uwezo nayo, ndio hizi. Kama George Washington alipoingia madarakani kwa mara ya kwanza angewakumbatia rafiki zake Marekani isingekuwa hivi. Lakini aliwaambia "You are friends of George Washington, not friends of President of United States of America". Kikwete alikumbatia sana marafiki zake, akawapa nafasi japokuwa hawana uwezo. Wao wakawa wanakula "deals" na kurudisha gharama za kuchangia uchaguzi mkuu wa 2005. Nani alikuwa hajui kuwa Nazir Karamagi alipewa Uwaziri kwa kuwa alikuwa mfadhili wa uchaguzi? Nani alikuwa hajui kuwa Anthony Dialo naye alipewa Uwaziri kwa sababu alikuwa akifadhili uchaguzi? Nani hajui kwamba mtu kama Stephen Wassira anaendelea kuwa Waziri kwasababu yeye ndiye alikuwa anaongoza kampeni za kuwamaliza Frederick Sumaye, Dk. Salim Ahmed Salim na Mzee John Malecela kule kanda ya ziwa mwaka 2005?
Matatizo ya watanzania wa leo yanatokana na dhambi ya viongozi wetu. Na dhambi hii itatutesa milele. Gesi ya kusini mwa Tanzania ni kielelezo. Lakini pia tukumbuke namna ambavyo wanyamapori wanauzwa wakiwa hai. Nani aliwahi kutafakari kuhusu mnunuzi wa wanyama hawa?
Kama Watanzania wanazo kumbukumbu, warejee mwaka 2005. Gazeti moja liliwahi kuandika kwamba Bilionea kutoka Ufalme wa Oman alikuwa ametoa dola milioni 40 kusaidia kampeni za Kikwete. Kikwete na watu wake wakatangaza kuwa watalishitaki gazeti hilo (Nadhani ni Radi Tanzania) nchini Uingereza kwasababu gazeti hilo lilinukuu habari iliyochapishwa na Jarida la African Analysis la nchini humo.
Niwakumbushe kuwa ni Salva Rweyemamu ambaye sasa ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu aliyetumwa London kufungua mashitaka dhidi ya Radi Tanzania na Jarida hilo la Uingereza na tukatangaziwa hivyo. Waandishi wa Tanzania leo hakuna anayeuliza kuhusu kesi hiyo kama kweli ilifunguliwa. Na kama ilifunguliwa, mashitaka yalikwendaje na kesi imekwishaje?
Lakini Waandishi wetu hawaulizi kwanini mtu yuleyule anayeandikwa kwamba alitoa dola milioni 40 ndiye huyo huyo ambaye alihusika katika mitambo ya kufua umeme wa dharura? Kwanini hawaulizi kwanii wanyama wanaouzwa nje ya nchi wanahusika na ukoo huo wa kifalme?
Watanzania, ni kweli kwamba kuendelea kukumbuka hali ilivyokuwa huko nyuma wakati nchi hii ikiwa na viongozi wasafi, ni kutafuta machozi. Lakini hebu tuanze kuvuta hisia, kama kweli Mwalimu Nyerere angekuwa fisadi, leo hii watoto wake wangeishi maisha ya kifahari sana. Mwalimu aliipenda Tanzania kwanza.
Leo tunaona kuwa watoto wa viongozi wetu ndio matajiri wakubwa. Wanapata wapi pesa zote hizo?
Mradi wa Gesi ambao leo unawatesa watanzania wenzetu ni matokeo ya miradi kandamizi na ya kifisadi. Mradi huu una manufaa kidogo kwa Wamakua, Wamakonde, Wayao na Wamwera kuliko watu wengine. Kusini ilitengwa sana,ilikabwa sana ni vema sasa ikaachwa nayo ipumue.
 
acha kulia lia wahalifu ni lazima wakamatwe na vitu walivyopora! unaudanganya uma,
 
Pamoja na Waziri Mkuu kuamuru kuwa wale wote waliokamatwa kwa uchochezi wa matukio ya vurugu Mtwara waachiwe hali ni kinyume kabisa kwani kila siku watu wanakamatwa hovyo. Kwa sasa watu wanakamatwa kwa kosa la kuwa wananchama wa CHADEMA. Jana huko Lulindi kata ya Namalenga kijiji cha Mitesa mwenyekiti wa kijiji hicho kupitia CHADEMA aitwaye GHADAFI amekamatwa saa 6 usiku na polisi wa Masasi. Alikamatwa pamoja na kaimu mtendaji wa kijiji hicho.
.

Ndio ukamanda huo. Komaeni nao hivyo hivyo mpaka kieleweke!
 
hili wanalofanya litapelekea 2015 isifike kabla ya mabadiliko nasi ndo tunataka kwani tunaona 2015 ni mbali, Mungu apewe ssifa. AMEN
 
Mhalifu ni mhalifu tu, Ni lazima achukuliwe hatua hakuna cha kukiomba chama labda mtuaminishe kuwa mmetumwa na chama chenu.
kufanya uhalifu kwa kisingizio cha chama! Mtashughurikiwa tu hata na hao wanaowatuma.

Mhalifu namba moja ni MACCM,hao waliokamatwa tunajua ni utaratibu wa siku zote wa POLICCM kuwabambikia watu makosa ,lakini kwa hili la gesi Mtwara mtabambikia watu kesi mpaka mtachoka,kwetu sisi kufuatilia kilichowapata viongozi hao ni utaratibu wa kawaida,na hao mnawatuhumu,lakini all in all ni chuki zenu mafisadi za kutaka kukidhoofisha chama
 
Vitendo wanavyovifanya serkal ccm masasi kwa wananchi nisawa na kuzima moto kwa petrol! Nb: You can kill people but revolution ideas will never die!
 
Vitisho au kukamata viongozi wa CDM sio suluhisho bali kunazidi kuwajenga na kuwapatia umaarufu mara dufu. Magamba wameshindwa kufikiri. Nawapa pole!
 
Back
Top Bottom