Hali tete Masasi

Hali tete Masasi

Joined
Dec 5, 2009
Posts
65
Reaction score
23
Pamoja na Waziri Mkuu kuamuru kuwa wale wote waliokamatwa kwa uchochezi wa matukio ya vurugu Mtwara waachiwe hali ni kinyume kabisa kwani kila siku watu wanakamatwa hovyo. Kwa sasa watu wanakamatwa kwa kosa la kuwa wananchama wa CHADEMA. Jana huko Lulindi kata ya Namalenga kijiji cha Mitesa mwenyekiti wa kijiji hicho kupitia CHADEMA aitwaye GHADAFI amekamatwa saa 6 usiku na polisi wa Masasi. Alikamatwa pamoja na kaimu mtendaji wa kijiji hicho.

Jana hiyo hiyo yapata Mahabusu 110 walifikishwa mbele ya hakimu wa mahakama ya mwanzo. Kwa kuwa mahakama ya mwanzo ilichomwa moto hakimu alilazimika kuwasomea mashitaka yao katika chumba cha hakimu mkazi. Kosa kubwa linalowagharimu viongozi na wanachama wa CHADEMA ni kukutwa na kadi ya CDM. Kwa sasa imewalazimu wananchi kutembea na kadi za CCM kama njia pekee ya kunusurika na kukamatwa na polisi ambao wengi wao wametoka Tunduru na Songea.

Askari hawa wakija kukamata watu wanapora vitu mbalimbali vya ndani. Ukikutwa una TV unadaiwa risiti kama huna wanaichukua. Viongozi wote wa mashina wa CDM wamekamatwa. Kwa kweli hali ni mbaya sana. Hakuna chombo cha habari hata kimoja kinachotoa taarifa ya mambo yanayotokea huku. Wananchi wanadai kwamba vyombo vya habari vimenyamazishwa.

Viongozi kadhaa wa CHADEMA wa Masasi na karibu mkoa wote wa Mtwara wako katika wakati mgumu sana. Baadhi wamekimbia majumbani mwao na sasa wengine inasemekana kwamba wameenda DSM kujificha.

CCM wameamua kutumia jeshi la polisi kuhakikisha kwamba wapenzi, wanachama,viongozi na mashabiki wa CHADEMA wananywea na kuogopa kabisa kujitambulisha na chama chao. Hii sasa ni nchi ya vitisho. Sioni kama tutafika tuendako. Hali ni tete sana huko Mtwara.
 
Nilijua yangekuja kuwa hivi....
 
sasa sijui tuwasaidiaje jamani?kwani kabla hamjaanza harakati zenu hamkujua reaction itakuaje?au mlidhani watawakubalia madai yenu.
 
Pamoja na Waziri Mkuu kuamuru kuwa wale wote waliokamatwa kwa uchochezi wa matukio ya vurugu Mtwara waachiwe hali ni kinyume kabisa kwani kila siku watu wanakamatwa hovyo. Kwa sasa watu wanakamatwa kwa kosa la kuwa wananchama wa CHADEMA. Jana huko Lulindi kata ya Namalenga kijiji cha Mitesa mwenyekiti wa kijiji hicho kupitia CHADEMA aitwaye GHADAFI amekamata saa 6 usiku na polisi wa Masasi. Alikamatwa pamoja na kaimu mtendaji wa kijiji hicho.

Jana hiyo hiyo yapata Mahabusu 110 walifikishwa mbele ya hakimu wa mahakama ya mwanzo. Kwa kuwa mahakama ya mwanzo ilichomwa moto hakimu alilazimika kuwasomea mashitaka yao katika chumba cha hakimu mkazi. Kosa kubwa linalowagharimu viongozi na wanachama wa CHADEMA ni kukutwa na kadi ya CDM. Kwa sasa imewalazimu wananchi kutembea na kadi za CCM kama njia pekee ya kunusurika na kukamatwa na polisi ambao wengi wao wametoka Tunduru na Songea.

Askari hawa wakija kukamata watu wanapora vitu mbalimbali vya ndani. Ukikutwa una TV unadaiwa risiti kama huna wanaichukua. Viongozi wote wa mashina wa CDM wamekamatwa. Kwa kweli hali ni mbaya sana. Hakuna chombo cha habari hata kimoja kinachotoa taarifa ya mambo yanayotokea huku. Wananchi wanadai kwamba vyombo vya habari vimenyamazishwa.

Viongozi kadhaa wa CHADEMA wa Masasi na karibu mkoa wote wa Mtwara wako katika wakati mgumu sana. Baadhi wamekimbia majumbani mwao na sasa wengine inasemekana kwamba wameenda DSM kujificha.

CCM wameamua kutumia jeshi la polisi kuhakikisha kwamba wapenzi, wanachama,viongozi na mashabiki wa CHADEMA wananywea na kuogopa kabisa kujitambulisha na chama chao. Hii sasa ni nchi ya vitisho. Sioni kama tutafika tuendako. Hali ni tete sana huko Mtwara.

Hapo pekundu: Hata vyombo vya habari vikinyamzishwa JF ipo na wapasha habari wenye uchungu na wananchi wapo. Lazima kitaileweka.
 
mwisho wa hayo upo karibu sana tena umekwishawadia vilio hivi vitaisha e4ndapo wananchi wakiamua ni nani awe kiongozi wao na sio kulazimishiwa kiongozi.
 
kuna utabiri ulitolewa humu jamvini kuwa maadam pinda ameenda mtwara basi liwalo na liwe. Serikali na ccm wamepoteza mwelekeo. Wanajinadi kuwa ni wasikivu lakini ukweli ni kuwa wanaongozwa na genge la majambazi, magaidi na mafia wasio na uzalendo wala huruma kwa wananchi
 
Mungu Ibariki Tanzania , Dumisha Uhuru na Umoja,
Wake kwa Waume na Watoto..........

Nikiikumbuka versi hii halafu ikiwa inaimbwa na MCCM machozi hunidondoka.
Poleni Wanantwara
 
Kuna taarifa za ndani kwamba wale viongozi na wanachama wa CDM waliokamatwa na kufikishwa mahakamani jana wamenyimwa dhamana. Wapo waliokaa mahabusu takribani wiki moja sasa. Eti wanashikiliwa kwa kosa la kula njama.
 
Poleni wana wa Masasi... Napenda kuwapa faraja kwamba haya yote yatapita na mwisho mtashinda..

Hakuna majeshi, polisi,mahakama, mabomu na nguvu zote za uovu zimewahi kushinda nguvu ya umma.. hata kama wakileta majeshi yote ya nchi hii na kuazima ya jirani bado ukweli utabakia palepale na nguvu ya umma itashinda.

Msife moyo kwani wa tz wapenda haki wapo pamoja nanyi na tunawaombea kwenye wakati huu mgumu...

Msiache kupambana kwa umoja kwani utengano wenu ni nguvu kwa adui yenu... TUTASHINDA ... WAO WANA JESHI SISI TUNA MUNGU
 
Mungu Ibariki Tanzania , Dumisha Uhuru na Umoja,
Wake kwa Waume na Watoto..........

Nikiikumbuka versi hii halafu ikiwa inaimbwa na MCCM machozi hunidondoka.
Poleni Wanantwara
Dumisha uhuru wa kupiga raia na umoja wa wenye nacho.
 
kama mulianzishe tena

Umeniwahi,watu wachache wanafaidi rasilimali zetu tu kana kwamba wao tu ndio waliozaliwa na mwanamke?Kumbe wengine wamepita kwenye magogo eti?Acha kinuke tu,hakuna mtu wa kusimamia kwa faida ya wengi,nyang'..u wakubwa hawa.
 
Kwa sasa imewalazimu wananchi kutembea na kadi za CCM kama njia pekee ya kunusurika na kukamatwa na polisi ambao wengi wao wametoka Tunduru na Songea.

Huuni mtego maarufu wa CCM, nadhani bado una nafasi ya kufanikiwa miongoni mwa jamii yetu!!
 
Poleni wana wa Masasi... Napenda kuwapa faraja kwamba haya yote yatapita na mwisho mtashinda..

Hakuna majeshi, polisi,mahakama, mabomu na nguvu zote za uovu zimewahi kushinda nguvu ya umma.. hata kama wakileta majeshi yote ya nchi hii na kuazima ya jirani bado ukweli utabakia palepale na nguvu ya umma itashinda.

Msife moyo kwani wa tz wapenda haki wapo pamoja nanyi na tunawaombea kwenye wakati huu mgumu...

Msiache kupambana kwa umoja kwani utengano wenu ni nguvu kwa adui yenu... TUTASHINDA ... WAO WANA JESHI SISI TUNA MUNGU

Tena watambue kuwa huu moto ulioanza kuwaka mioyoni mwa watanzania wazalendo wa kweli hautazimwa kwa mbinu wazitumiazo kamwe!Hicho wanachokifanya ni sawa na kutumia petrol kuzimia moto.
 
Kuamini kuwa CHADEMA ndio adui yao, wanakosea sana......Kuamini hivyo ni kuwatukana wananchi wa huko! Ina maana watanzania wenzetu wa huko hawana ufahamu wa kutambua mateso, dhiki inayowakabili mpaka aje mtu awaambie?
Yaliyotokea huko na yanyoendelea kutokea kila pembe ya nchi hii, ni ishara kuwa watanzania wamechoshwa na porojo zao, wanataka mabadiliko chanya yatakayosababisha kuboreka kwa maisha yao pia.

Wa deal na matatizo ya msingi yanayowakabilil wananchi, watafute majawabu ya kueleweka na sio kukimbizana na vyama vya siasa.
 
Aiseee mwaka gani waziri mkuu alisema wahalifu waachiwe? Wakati Rais alisema vizuri tu vyombo vya dola vifanye kazi yao Mwana CDM kama akishikwa isivyo haki Mahamani atashinda usiwe na wasiwasi?
 
Viongozi wa kitaifa wa cdm fuatilieni hilo ili kujua kama linaukweli na baada ya hapo kitengo cha wanasheria wa chama wasimamieni viongozi hawa wa masasi.pia mlioko huko kama taarif ahamjazileta ngome fanyeni mpango wa haraka kuleta taarifa hizo na ikibidi mtu au watu waje physical pale ngome na kulitolea maelezo jambo hili na kisha najua chama kitachukua hatua za haraka kulitatua hili.
 
hizo ni dalili za dola inayoanguka hivi punde kutumia jeshi na vitisho kujaribu kujinusuru lakini watashindwa na nguvu ya umma!na viongozi waliokimbia wanapaswa wafukuzwe kwenye chama maana hakuna dhambi mbaya kama woga! wanatakiwa wabakie kwenye maeneo yao kuongoza mapambano sio kukimbia! Na viongozi wakuu makao makuu watoa tamko na kuchukua hatua za haraka kuwanusuru ndugu zetu wa kusini! M4C forever freedom is soon coming!
 
Hosin Mubarak wa misri alitumia vifaru; wanajeshi wakaua hadi wakaona ni upuuzi! waandamanaji wakapanda juu ya vifaru huku askari wakiwalinda. We cannot defeat injustice by becoming more inferior before oppressors but by becoming more superior against injustice and oppressors! Ukiona unyanyasaji unashamiri ujue ukombozi umekaribia. I prefer non violence struggle which is at hand-2015. Lets come together kingsmen and reject the bark-shelled exploiters.
 
Back
Top Bottom