Mwalimu Makini
Member
- Dec 5, 2009
- 65
- 23
Pamoja na Waziri Mkuu kuamuru kuwa wale wote waliokamatwa kwa uchochezi wa matukio ya vurugu Mtwara waachiwe hali ni kinyume kabisa kwani kila siku watu wanakamatwa hovyo. Kwa sasa watu wanakamatwa kwa kosa la kuwa wananchama wa CHADEMA. Jana huko Lulindi kata ya Namalenga kijiji cha Mitesa mwenyekiti wa kijiji hicho kupitia CHADEMA aitwaye GHADAFI amekamatwa saa 6 usiku na polisi wa Masasi. Alikamatwa pamoja na kaimu mtendaji wa kijiji hicho.
Jana hiyo hiyo yapata Mahabusu 110 walifikishwa mbele ya hakimu wa mahakama ya mwanzo. Kwa kuwa mahakama ya mwanzo ilichomwa moto hakimu alilazimika kuwasomea mashitaka yao katika chumba cha hakimu mkazi. Kosa kubwa linalowagharimu viongozi na wanachama wa CHADEMA ni kukutwa na kadi ya CDM. Kwa sasa imewalazimu wananchi kutembea na kadi za CCM kama njia pekee ya kunusurika na kukamatwa na polisi ambao wengi wao wametoka Tunduru na Songea.
Askari hawa wakija kukamata watu wanapora vitu mbalimbali vya ndani. Ukikutwa una TV unadaiwa risiti kama huna wanaichukua. Viongozi wote wa mashina wa CDM wamekamatwa. Kwa kweli hali ni mbaya sana. Hakuna chombo cha habari hata kimoja kinachotoa taarifa ya mambo yanayotokea huku. Wananchi wanadai kwamba vyombo vya habari vimenyamazishwa.
Viongozi kadhaa wa CHADEMA wa Masasi na karibu mkoa wote wa Mtwara wako katika wakati mgumu sana. Baadhi wamekimbia majumbani mwao na sasa wengine inasemekana kwamba wameenda DSM kujificha.
CCM wameamua kutumia jeshi la polisi kuhakikisha kwamba wapenzi, wanachama,viongozi na mashabiki wa CHADEMA wananywea na kuogopa kabisa kujitambulisha na chama chao. Hii sasa ni nchi ya vitisho. Sioni kama tutafika tuendako. Hali ni tete sana huko Mtwara.
Jana hiyo hiyo yapata Mahabusu 110 walifikishwa mbele ya hakimu wa mahakama ya mwanzo. Kwa kuwa mahakama ya mwanzo ilichomwa moto hakimu alilazimika kuwasomea mashitaka yao katika chumba cha hakimu mkazi. Kosa kubwa linalowagharimu viongozi na wanachama wa CHADEMA ni kukutwa na kadi ya CDM. Kwa sasa imewalazimu wananchi kutembea na kadi za CCM kama njia pekee ya kunusurika na kukamatwa na polisi ambao wengi wao wametoka Tunduru na Songea.
Askari hawa wakija kukamata watu wanapora vitu mbalimbali vya ndani. Ukikutwa una TV unadaiwa risiti kama huna wanaichukua. Viongozi wote wa mashina wa CDM wamekamatwa. Kwa kweli hali ni mbaya sana. Hakuna chombo cha habari hata kimoja kinachotoa taarifa ya mambo yanayotokea huku. Wananchi wanadai kwamba vyombo vya habari vimenyamazishwa.
Viongozi kadhaa wa CHADEMA wa Masasi na karibu mkoa wote wa Mtwara wako katika wakati mgumu sana. Baadhi wamekimbia majumbani mwao na sasa wengine inasemekana kwamba wameenda DSM kujificha.
CCM wameamua kutumia jeshi la polisi kuhakikisha kwamba wapenzi, wanachama,viongozi na mashabiki wa CHADEMA wananywea na kuogopa kabisa kujitambulisha na chama chao. Hii sasa ni nchi ya vitisho. Sioni kama tutafika tuendako. Hali ni tete sana huko Mtwara.