Hali si shwari Jumuiya ya Wazazi CCM

PISTO LERO

JF-Expert Member
Mar 8, 2011
2,819
1,454
HALI si shwari ndani ya Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), baada ya Diwani wa Kata ya Magomeni, Julian Bujugo kufungua kesi Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam akiitaka Jumuiya hiyo kumlipa Sh3 bilioni kama gharama alizotumia kukarabati majengo ya Shule ya Sekondari Kaole iliyopo Bagamoyo mkoani Pwani.

Sekondari hiyo awali ilikuwa chini ya jumuiya hiyo lakini baada ya kushindwa kujiendesha, ilichukuliwa na Bujugo ambaye aliikarabati na kuibadilisha kuwa Chuo cha Kilimo Kaole, ambapo huchukua asilimia 75 ya mapato huku asilimia 25 zikienda katika mfuko wa Jumuiya hiyo.

Hatua hiyo imekuja siku tatu baada ya Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Taifa, Abdallah Bulembo kumtaka Bujugo aikabidhi shule hiyo kwa jumuiya kabla hajachukuliwa hatua za kisheria.

Katika maelezo yake, Bulembo alisema Bujugo hana haki ya kuendelea na ujenzi wowote katika majengo ya chuo hicho kwa kuwa mikataba aliyoingia na jumuiya ni feki na haina baraka za Baraza Kuu wa Wadhamini la Wazazi, huku akifafanua kuwa diwani huyo alikabidhiwa shule ili awe meneja lakini alikiuka makubaliano na kuifanya kuwa chuo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Bujugo alisema kesi hizo namba 16 na 20 amezifungua juzi, ikiwa ni wiki mbili tangu kupewa barua na jumuiya hiyo akitakiwa kusimamisha ujenzi wa chuo hicho.

"Nimefungua kesi namba 16 ambayo inalenga kuizuia jumuiya kutowasumbua wanachuo na kesi ya pili ni namba 20 ambayo inawataka wanilipe gharama nilizotumia kukarabati chuo" alisema.

Alifafanua, "Niliingia nao mkataba ambao tuliusaini mwaka 2010 kati yangu mimi, aliyekuwa mwenyekiti wa jumuiya ambaye kwa sasa ni marehemu, Athumani Mhina pamoja na katibu ambaye mpaka sasa yupo katika jumuiya, Khamis Dady" alisema Bujugo huku akionyesha mkataba huo.

Akifafanua fedha anazoidai jumuiya hiyo alisema ili kuyaachia majengo ya chuo hicho, ameitaka jumuiya hiyo ya wazazi kumlipa Sh3 bilioni kama gharama alizotumia kufanya ukarabati.

"Wakati wananikabidhi shule hii niliwakuta walimu wanadai fedha na nikawalipa Sh45 milioni.

Nimelipa madeni ya Mamlaka ya Mapato (TRA)Sh65 milioni, umeme nilikuta wanadaiwa Sh15 milioni, nilitumia zaidi ya Sh1.8 bilioni kufanya ukarabati wa majengo, ukiweka na gharama nyingine inafikia Sh3 bilioni," alisema Bujugo na kuongeza; "Ninachotaka ni wao kunilipa gharama zinizotumia, sina kinyongo na mtu na wala sitaki kuking'ang'ania chuo.

Kwanza pale chuoni kuna wanafunzi 300 wanashindwa kusoma kwa sababu ya mvutano huu." Akizungumzia kauli hiyo Bulembo aliliambia gazeti hili jana kwa njia ya simu kwamba, msimamo wake uko palepale na chuo hicho ni lazima kirudi mikononi mwa jumuiya hiyo. "Nilishasema hata nilipokuwa wilayani Bagamoyo, mikataba ile aliyoingia ni feki na lazima chuo kirudi mikononi mwa jumuiya" alisema Bulembo
 
Du!!!!!! hapo patamu kweli maana Panya anajitafuna mkia wake mwenyewe. Tunashukuru sana vyama vya upinzani angalau tumeweza kujua nini maana ya mikataba feki. Hapo zamani za kale hatukujua kitu kiitwacho MIKATABA sembuse MIKATABA FEKI?
 
Mbona swala dogo tu hili. Mama diwani alete vithibitisho vya gharama aliyotumia, then utaratibu wa kumrudishia ufanyike.
 
SSM hao, na mikataba yao ya kupeana kama ile ya kule kwenye kiwanda cha ARV fake Arusha!!! Kweli sasa ni wakati umefiaka SSM mpumzike!! Bora tuongozwe na ng'ombe au jiwe!!
 
Wanafahamiana hawa, angalia:
katika lugha ya Kihaya maana ya haya majina ni;

BUJUGO-- Sehemu au mahali pa kutolea mahari

BULEMBO-- Uwanja wa Mbele wa nyumba.

shughuli zote za harusi hufanyika uwanja huu siyo kama mjini ambapo kumbi zinashika hatamu maana yake Bujugo huafanyikia Bulembo
 
Japo ni kweli hali si shwari kule 'Wazazi CCM',

lakini nako nao Ma-Kada kibao CCM nao hivi sasa wanamchukia Kinana hakuna fanania yake; madai yakiwa ni kwamba huyo mwakilishi rasmi wa MASLAHI YA MAFISADI chamani na katika biashara mbalimbali nchini hivi sasa anasomwa kama MHARIBIFU MKUBWA aliyetumwa na Lowassa kuja kukiua kabisa chama chao hata kabla ya 2015.

Habari ndio hiyo!!!
 
Bujugo ana historia ndefu ya utapeli, siwezi kushangaa makaratasi anayosema ni mkataba hayakupata baraka za Jumuiya ya wazazi bali maelewano yake na alioingia nao mkataba baada ya kuwakatia fedha ndefu.

Bujugo iache Jumuiya Ipumue. Rudisha majengo kwa amani
 
Japo ni kweli hali si shwari kule 'Wazazi CCM',

lakini nako nao Ma-Kada kibao CCM nao hivi sasa wanamchukia Kinana hakuna fanania yake; madai yakiwa ni kwamba huyo mwakilishi rasmi wa MASLAHI YA MAFISADI chamani na katika biashara mbalimbali nchini hivi sasa anasomwa kama MHARIBIFU MKUBWA aliyetumwa na Lowassa kuja kukiua kabisa chama chao hata kabla ya 2015.

Habari ndio hiyo!!!

Baada ya Kinana kuteuliwa na Rais ( Mwenyekiti wa CCM) jina lake lilirudishwa kwa wanaCCM kwa ajili ya kuthibitishwa kukubali au kumkataa, kama walikuwa hawamtaki kwa nini hawakumkataa?
 
Hivi si nilisikia kwamba Le Mutuzi ni Mjumbe kwenye hiyo Jumuia? Kazi wanayo kama kweli sijui Le Mutuzi mawazo yake huwa wanayachambua vizuri!
 
Vita vya panzi furaha ..............! Laana zinawarudia wezi wakubwa hao na ccm yao
 
Hapo zamani za kale kulikuwa na diwani anaitwa Bujugo ambaye kwa sababu zisizofahamika aliamua kukarabati majengo ya shule ya chama chake kwa Tsh. bilioni 3. Fedha hii ilikuwa inamtosha Bujugo kununua kipande cha ardhi na kujenga shule/chuo lakini yeye akaamua kukarabati cha CCM. Hadi hivi leo haijulikani ni kwa nini Bujugo alichukua uamuzi huu.
 
Hapo zamani za kale kulikuwa na diwani anaitwa Bujugo ambaye kwa sababu zisizofahamika aliamua kukarabati majengo ya shule ya chama chake kwa Tsh. bilioni 3. Fedha hii ilikuwa inamtosha Bujugo kununua kipande cha ardhi na kujenga shule/chuo lakini yeye akaamua kukarabati cha CCM. Hadi hivi leo haijulikani ni kwa nini Bujugo alichukua uamuzi huu.
huyu mwiz tu hzo bilion tatu anazsikia kwel angeweza kununua sehemu kubwa na kujenga chuo bora zaid,laana hyo inawamalza mumeanza kulana wenyewe je kwa wengne c baraa
 
Back
Top Bottom