The Listener
JF-Expert Member
- Feb 5, 2012
- 993
- 213
Kutokana na kanuni za Utumishi wa Umma kutumia mbinu yoyote ya ulaghai ni kosa. Zoezi la Kutengeneza vitambulisho vya utaifa limezaa scandal japo ni kwa sehemu ndogo tu ya watumishi wa Serikali. Kada ya uaskari ni nyeti sana katika nchi yetu. Kama askari polisi 700 na wanajeshi 248 wamekutwa na matumizi ya majina ya watu wengine ambao hatuna uhakika hata baadhi yao kuwa bado wako hai au la. Nisaidieni kujua wana jamii kama watumishi hawa kwa mujibu wa taratibu wanaweza kupewa adhabu inayoweza kufikia kufukuzwa kazi? Mimi nauliza hivi nikiwa na hofu kubwa kwamba kundi hili (ambalo ni la hapa DSM tu) likifukuzwa kazi huko mtaani kutakuwaje.