Siri ya sifuri
JF-Expert Member
- Sep 21, 2018
- 2,016
- 1,501
Uko Wapi ubabe wa mwanaume mbele ya mwanamke anaempenda!?huwezi amini lakini ndio ukweki wenyewe, Mwanaume nikiumbe dhaifu sana kwa mwanamke wake, ubabe wa mwanaume unaishia kwa MTU baki na kwamwanamke wake.
Achana na baunsa "mbavu Nene" kuna jambazi mwenye silaha anaweza kumripua yeyote yule bila kufikiria lakini ukimkuta kwa bibie huwezi amini, anaweza hata kushikwa kalio na akacheka, mbele ya mpenzi wake mwanaume ni sawa na mtoto, tofauti kubwa ni kwamba yeye mwanaume ndio mchumi.
Mwanaume yupo tayari umshambulie yeye lakini usimguse mkewe, yeye mwanaume ashinde njaa lakini mwanamke wake ale kwa kuchagua CHAKULA akipendacho, Mwanaume mchafu bibie ng'aring'ari, hajali.
Wanaume tukiwa wenyewe kwa wenyewe tunavyojisifu kwa kudhibiti wenza wetu ni nani awezae kumpinga mwenzie!? Ila tukiingia ndani aibu. Hivi ni nani kati yetu sisi wanaume ambaye anauwezo wa kuhamisha nguvu zilizokwisha shuka chini nakuzirudisha kifuani ili afanye ubabe wakati ule kishazungushiwa upande wa Kanga kiunoni anasindikizwa bafuni kuoga!? Hivi wanaume tunakwama Wapi?
Achana na baunsa "mbavu Nene" kuna jambazi mwenye silaha anaweza kumripua yeyote yule bila kufikiria lakini ukimkuta kwa bibie huwezi amini, anaweza hata kushikwa kalio na akacheka, mbele ya mpenzi wake mwanaume ni sawa na mtoto, tofauti kubwa ni kwamba yeye mwanaume ndio mchumi.
Mwanaume yupo tayari umshambulie yeye lakini usimguse mkewe, yeye mwanaume ashinde njaa lakini mwanamke wake ale kwa kuchagua CHAKULA akipendacho, Mwanaume mchafu bibie ng'aring'ari, hajali.
Wanaume tukiwa wenyewe kwa wenyewe tunavyojisifu kwa kudhibiti wenza wetu ni nani awezae kumpinga mwenzie!? Ila tukiingia ndani aibu. Hivi ni nani kati yetu sisi wanaume ambaye anauwezo wa kuhamisha nguvu zilizokwisha shuka chini nakuzirudisha kifuani ili afanye ubabe wakati ule kishazungushiwa upande wa Kanga kiunoni anasindikizwa bafuni kuoga!? Hivi wanaume tunakwama Wapi?