Hakuna mashabiki wanafiki kama Simba FC

Hakuna mashabiki wanafiki kama Simba FC

ukikaidi utapigwa2

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2015
Posts
16,286
Reaction score
31,675
Hivi karibuni mashabiki wa ile timu ya Manzoki na Mzee Rage walikua wanapigania haki ya Mzize aende nje akajitafutie maisha kwamba timu yake ina roho mbaya ajabu ni kwamba timu yao imemsajiri Salim Mwalimu kutoka Wydad aje huku alipo Mzize, hii ina maana Mwalimu hana future au mapenzi yao kwa Mzize ni mkubwa sana?
 

Attachments

  • IMG-20241229-WA0002.jpg
    IMG-20241229-WA0002.jpg
    30.9 KB · Views: 20
Kuna utofauti wa kimuktadha kati yya Mzize na Seleman Mwalimu.

Mzize ilikuwa ni sakata la ndoto binafsi dhidi ya vizingiti vya kiuongozi. Mzize alitamani kujiendeleza kimataifa, akilenga klabu yenye ushindani mkubwa kama Esperense de Tunis.

Mashabiki tulimtetea kwa misingi ya haki. Tuliona Club yake ya Yanga ikiuzuia uhamisho kwasababu zisizo za kiufundi, ikikataa ofa bora na kuhimiza aende Club dhaifu kwa maslahi ya udalali.

Selemani Mwalimu ni usajili usiokuwa na kipengele wala migogoro
Hakuna sakata la mgongano wa kimaslahi, Wydad haikugomea uhamisho wake na wala hakuna dalili ya udalali au mgongano wa kimaslahi.
 
Kuna utofauti wa kimuktadha kati yya Mzize na Seleman Mwalimu.

Mzize ilikuwa ni sakata la ndoto binafsi dhidi ya vizingiti vya kiuongozi. Mzize alitamani kujiendeleza kimataifa, akilenga klabu yenye ushindani mkubwa kama Esperense de Tunis.

Mashabiki tulimtetea kwa misingi ya haki. Tuliona Club yake ya Yanga ikiuzuia uhamisho kwasababu zisizo za kiufundi, ikikataa ofa bora na kuhimiza aende Club dhaifu kwa maslahi ya udalali.

Selemani Mwalimu ni usajili usiokuwa na kipengele wala migogoro
Hakuna sakata la mgongano wa kimaslahi, Wydad haikugomea uhamisho wake na wala hakuna dalili ya udalali au mgongano wa kimaslahi.
Kwanini msimpiganie Kibu
 
Kuna utofauti wa kimuktadha kati yya Mzize na Seleman Mwalimu.

Mzize ilikuwa ni sakata la ndoto binafsi dhidi ya vizingiti vya kiuongozi. Mzize alitamani kujiendeleza kimataifa, akilenga klabu yenye ushindani

Wewe ndio mzize? Au hayo maneno kayasema wapi Mzize?
 
Hivi karibuni mashabiki wa ile timu ya Manzoki na Mzee Rage walikua wanapigania haki ya Mzize aende nje akajitafutie maisha kwamba timu yake ina roho mbaya ajabu ni kwamba timu yao imemsajiri Salim Mwalimu kutoka Wydad aje huku alipo Mzize, hii ina maana Mwalimu hana future au mapenzi yao kwa Mzize ni mkubwa sana?
Sio kila anayetofautiana na Yanga ni Simba. Sakata la Mzize ni kati ya uongozi wa Yanga na meneja/msimamizi wa mchezaji. Sema ulitafsiri hivyo kuwa ni Simba wanampigania Mzize. Mchezaji ajipiganie mwenyewe.
Simba imeshamuuza Edwin Balua huko Cyprus, ilimuachia Kibu akajipambanie Marekani ashindwe mwenyewe. Kuhusu Selemani Mwalimu, ni wapi uliposoma kwamba Simba imemzuia kubaki Wydad?
 
Mzize anaongea kupitia mwakilishi wake ambaye ni Meneja
Yeye ni bubu? Kipi kinachoaminisha kuwa huyo mwakilishi yote anayoongea ndiyo aliyoambiwa na Mzize ayaongee?
 
Sio kila anayetofautiana na Yanga ni Simba. Sakata la Mzize ni kati ya uongozi wa Yanga na meneja/msimamizi wa mchezaji. Sema ulitafsiri hivyo kuwa ni Simba wanampigania Mzize. Mchezaji ajipiganie mwenyewe.
Simba imeshamuuza Edwin Balua huko Cyprus, ilimuachia Kibu akajipambanie Marekani ashindwe mwenyewe. Kuhusu Selemani Mwalimu, ni wapi uliposoma kwamba Simba imemzuia kubaki Wydad?
Edwin Balua ana impact gani kwenye kikosi cha 5imba? kiasi kwamba uondokaji wake uwe na ugumu
 
Yeye ni bubu? Kipi kinachoaminisha kuwa huyo mwakilishi yote anayoongea ndiyo aliyoambiwa na Mzize ayaongee?
Ally Kamwe ambaye ni msemaji wa klabu, ina maana anapotoa taarifa kuhusu taasisi au mchezaji, mchezaji au aliyewakilishwa anakuwa bubu?

Katika dunia ya michezo ya kisasa, kuna level ya kimawasiliano ambayo mchezaji hawezi kuisimamia moja kwa moja, hasa pale linapokuja suala la mikataba, uhamisho, au masuala ya kisheria. Hii ndiyo sababu wachezaji wengi hutumia mawakala, wasemaji wa klabu, au wanasheria kama wawakilishi wao.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom