nsanzu
JF-Expert Member
- Jul 29, 2015
- 4,390
- 4,822
Mwaka 2011 nikiwa natoka Mwanza nakuja Dar, nilipanda bus tukaianza safari, kufika Singida tukashuka kula, mimi nikachukua chakula nikachukua Tissue paper za kutosha, sasa kila mmoja kwenye kiti chake tunakula ndani ya bus, sasa siti za pembeni kulikuwa na mdada mrembo sana, tangu napanda nikawa namuangalia tu. Kamaliza kula alikuwa anatumia mikono kula, sasa kimbembe kikaja kwenye kunawa, atanawia wapi. Ile kuhangaika mi nikachomoa tishu 3 nikampa, yule mdada alinishukuru sana, bas kushuka Ubungo nikamuuliza anakoelekea akanambia Survey, nikamwambia tuchangie bajaji mi nilikuwa naenda Changanyikeni, tukawa tunawasiliana mwisho wa siku akaja kuwa mpenz wangu ingawa sikudumu nae.
Nisamehe tu J, nilikutenda visivyo ingawa ulionesha mapenzi ya dhati kwangu.
Nisamehe tu J, nilikutenda visivyo ingawa ulionesha mapenzi ya dhati kwangu.