KAVULATA
Mimi nitatofautiana na wewe kwa kitu kimoja hapa, Dr. Slaa sidhani kama suala la kuwa mgombea kupitia UKAWA ni issue kubwa kwake....!!! Hapa tatizo ni kwamba, Dr. amejisikia mpweke na kapuuzwa mno!!! YES hata ningekuwa mimi, tumempigia mtu kelele za mwizi mwizi na kuwaamiinisha watu kuwa mwizi,mara mtu katuambia huyu si mwizi tuanzishe urafiki nae...!!! Sijui umenielewa? Kwa haraka haraka hapa , nitamuomba huyu mwizi awaeleze watu tuliowaaminisha kuwa mwizi kuwa YEYE si mwizi, wamwelewe then tufanye nae urafiki.....nje ya hapo inaweza kuleta sintofahamu kwa mtu yeyote!!! Ndo maana kwa binafsi ya moyo wangu bila kuleta ushabiki wa aina yoyote, nmemwomba mzee wangu na baba yangu kwa vile ni mcha Mungu,akumbuke kusamehe saba mara sabini...awasamehe wote akiwemo na EL ili asijehesabiwa dhambi ya kutosamehe.... Kavulata ni kweli Dr. Slaa wamemkwaza, utoto wa mjini umetumika katika hili wala si misingi na maadili ya kichama kama ambavyo mzee wangu Dr. Slaa amekuwa akiyasimamia....hapa tusitetee mtu, maadili ya kichama yamekiukwa. Ingekuwa busara kwa wakubwa wa chama pia kuachana na mambo ya mitaa ya Samora, wamuombe msamaha mzee kwa ajili ya kunusuru chama na mshikamano uliojengeka. Wakati huu si wa kuruhusu sintofahamu ya aina yoyote iwe ndogo au kubwa....Mwenyekiti nmekuwa nikimwamini sana kwa busara, kama ataamua potelea mbali atawavunja moyo sana watanzania walokuwa wakimwanini....Asijekengeuka kwa u-mimi ni mwenyekiti na yeye ni katibu tu!!! Tutafeli na EL wetu. Ikumbukwe upande wa pili nao wanautumia sana huu ufa kupenyeza siraha za maangamizi, kama mwenyekiti shupavu na makini, asijejidanganya kuwa hata akiachia ufa huu na Lowasa wake wataitoa CCM...NEVER!!! na kama haamini ajaribu, tunahitaji umoja wa hali na mali, si kwa EL na Dr Slaa tu bali kwa kila atakaeonyesha utayari wa kuungana na sisi. Tuwe kimkakati na si kiutoto wa mjini...Bila ushirika ulio thabiti CDM na UKAWA ni ndoto kwenda magogoni.