kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 16,252
- 16,171
Sitaki kuamini kama yupo mtu yeyote sasa ambaye anaweza kuwa yuko juu ya joto la matamanio ya watanzania wanaotaka mabadiliko ya uongozi wa nchi. Morali wa wananchi uko juu na matumaini yao yote yamebebwa na ukawa. Kila mtu ni lazima asome alama za nyakati na asome mioyo ya watanzania kwa sasa kuelekea October 2015.
Watanzania wako tayari kumsikiliza, kumheshimu na kumthamini mtu yeyote atakayewasaidia kuiangusha CCM October 2015 bila kujali rangi, kabila, dini, umaarufu wake wala itikadi ya chama anachotoka. Watanzania sasa wako tayari kumkasirikia milele mtu yeyote atakayeonekana kwa wazi au kwa kificho kuwa chanzo cha kuvunjika UKAWA na chanzo cha kushindwa uchaguzi 2015. Watamuandama kwa kumzomea na kumdharau mtu huyo popote atakapokuwa iwe msikitini, kanisani, barabarani au kwenye shughuli za kijamii kama misiba, atakosa raha ya kudumu ndani ya jamii yake.
Mfano, sitaki kuamini kuwa Dr. Slaa anaweza kupata amani ya roho kama akitoka chadema kwa wakati huu, wale watu waliomkweza hadi kuwa maarufu watamshusha chini tena kwa kasi ya ajabu sana kama atajitenga nao kwenye kipindi hiki kigumu na muhimu kwao.
Hataweza kupata maelezo yatakayowatosheleza mashabiki wa Ukawa ili kuhalalisha kujitenga kwake nao. Lowassa ni tegemeo sio tu kwa UKAWA lakini hata kwa CCM kwenyewe anakotoka. Lowassa ana rasilimali watu, fedha na software muhimu ambazo ndio vipuli muhimu kwenye gari la kuleta mabadiliko ya kisiasa nchini. Kumsusa Lowassa ni sawa na kuwasusa mashabiki wako na safari yao ya kuitoa CCM madarakani, lazima watakupa adhabu ya kisiasa unayostahili kwa kosa kama hili.
Ushauri wangu kwa mzee Dr. Slaa, sijui nani alikuahidi nini ndani au nje nchi ya nchi kama ukiwa rais wa nchi hii kinachokufanya hata usimuone tembo aliyeko kwenye sitting room yako, lakini wale tuliokufikisha hapo ulipo leo hii wanakuhitaji uwe nao katika kipindi hiki bila ya masharti yoyote kwa wafuasi, mashabiki na wasioipenda CCM kuingoza nchi hii tena miaka 5 ijayo.
Rudi kundini muda huu sio mwafaka kwa wewe kusemwa hivyo unavyosemwa sasa kwa kukaa kwako kimya
Watanzania wako tayari kumsikiliza, kumheshimu na kumthamini mtu yeyote atakayewasaidia kuiangusha CCM October 2015 bila kujali rangi, kabila, dini, umaarufu wake wala itikadi ya chama anachotoka. Watanzania sasa wako tayari kumkasirikia milele mtu yeyote atakayeonekana kwa wazi au kwa kificho kuwa chanzo cha kuvunjika UKAWA na chanzo cha kushindwa uchaguzi 2015. Watamuandama kwa kumzomea na kumdharau mtu huyo popote atakapokuwa iwe msikitini, kanisani, barabarani au kwenye shughuli za kijamii kama misiba, atakosa raha ya kudumu ndani ya jamii yake.
Mfano, sitaki kuamini kuwa Dr. Slaa anaweza kupata amani ya roho kama akitoka chadema kwa wakati huu, wale watu waliomkweza hadi kuwa maarufu watamshusha chini tena kwa kasi ya ajabu sana kama atajitenga nao kwenye kipindi hiki kigumu na muhimu kwao.
Hataweza kupata maelezo yatakayowatosheleza mashabiki wa Ukawa ili kuhalalisha kujitenga kwake nao. Lowassa ni tegemeo sio tu kwa UKAWA lakini hata kwa CCM kwenyewe anakotoka. Lowassa ana rasilimali watu, fedha na software muhimu ambazo ndio vipuli muhimu kwenye gari la kuleta mabadiliko ya kisiasa nchini. Kumsusa Lowassa ni sawa na kuwasusa mashabiki wako na safari yao ya kuitoa CCM madarakani, lazima watakupa adhabu ya kisiasa unayostahili kwa kosa kama hili.
Ushauri wangu kwa mzee Dr. Slaa, sijui nani alikuahidi nini ndani au nje nchi ya nchi kama ukiwa rais wa nchi hii kinachokufanya hata usimuone tembo aliyeko kwenye sitting room yako, lakini wale tuliokufikisha hapo ulipo leo hii wanakuhitaji uwe nao katika kipindi hiki bila ya masharti yoyote kwa wafuasi, mashabiki na wasioipenda CCM kuingoza nchi hii tena miaka 5 ijayo.
Rudi kundini muda huu sio mwafaka kwa wewe kusemwa hivyo unavyosemwa sasa kwa kukaa kwako kimya