Mbufi jina lako ni wale wadudu wanaosukuma kinyesi cha ng'ombe kinyumenyume kisha kufanya kama mpira mkubwa wa kinyesi. Au Mbufi una maanisha muumbaji???
sasa huyu siyo mavi ya ng'ombe bali ya binadamu..
Sasa ulijuaje akili zimeruka wakati akili zimekwisha ruka???? Duh story zingne bhana!
Omba sana yasikukute.[ Ina maana kila tukio linalompata mtu m1 ni lazma na mwingne
Omba sana yasikukute.[ Ina maana kila tukio linalompata mtu m1 ni lazma na mwingne
Si lazima na wewe likukute lilelile bali hapa namaanisha tusiwacheke watu wanaopatwa na matatizo maana matatizo yapo kwa kila mwanadam.
Ni hivyo tu ndugu yangu.
Ebu tufafanulie mkuu, isije ikawa tukawa tunaogopa kusalimina na waku tikihisi wanchokifanya ni "hypotization"... binafsi sieliwi hiyo hypnotization ikojeikoje?kuna mahali huyo jamaa alikosea katika mtiririko ukagutuka....hypnotization ilitaka kufanyika...pole
Inabidi tuanze kusalimiana kama wajapani..
Pole sana Bubu Msemahovyo!!! Nataka na wengine wajue kuwa hata siku moja usikubali eti mtu anakusimamisha anakuuliza maswali, wengi wao ni kama hao uliokutana nao leo. Huwa natoka baru tu, siangalii wala sisikii maana Tz imeharibika sasa!! Nilikutana na binti mmoja maeneo ya fulani Dar analia sana nikamuuliza kulikoni akasema alikutana na watu wakamsemesha mwishowe akatoa kila kitu. Kwa hiyo alikuwa analilia simu yake.
Wanasalimianaje wao?
Kwanza pole kwa msukosuko huo ndugu yetu. Hata mimi juzi nilikua Iringa na rafiki yangu, tukawa tunatoka mitaa ya sokoni kuelekea stendi ya mabasi, mara ghafla wakatokea vijana watatu wakaonekana kumfaham sana rafiki yangu maana walianza kumchangamkia sana kwa maswali mengi.
Ikabidi nimsubiri na badae nikaona kama muda unaenda nikaamua kumstua.
Asalaalee! Kumbe walikua washampumbaza akawa kama haelewi kinachotokea ila wale vijana wakaanza kunilalamikia kua nampeleka wapi jamaa yao (yaani yule rafiki yangu).
Kuepusha mengi nikampeleka pemben nikamuuliza kilichompata akasema hakumbuki ila bahati nzuri hawakumwibia.
Kwa kweli tuwe makini sana kwa sasa kuna wizi kwa njia ya kupumbaza.
Aliporejewa na akili ndio alijua hayo yoteSasa ulijuaje akili zimeruka wakati akili zimekwisha ruka???? Duh story zingne bhana!
Tafuta the science of hypnosis au kama una rafiki daktari umuulize kuhusu hypnosis kwenye psychiatry then you will realise that at times you do not know everything. By the way, uchawi na mambo mengine spiritual huwa science haiwezi sana kuyaeleza ila pia science cannot refute them so be cautious when uttering matters in public.
Leo asubuhi nimeteremka kituo cha Palm Beach, nikatoa nauli yangu kwa konda Tsh 2000/= Wakati nikisubiri change mbele yangu nawaona watu wawili wakiniangalia sana. Nikapokea change yangu na wakati nikiiweka mfukoni mmoja wao ananisemesha Nipe mia tano ya gazeti, kisha "Habari yako, za siku nyingi huku akinipa mkono. Nikampa mkono. Akaendelea kuniuliza "Vipi uko makao?" Wakati akiniuliza kama niko makao huku kanishikilia mkono ghafla nilianza kusikia kizunguzungu na kusikia kichefu chefu, nikajihisi akili zinaanza kama kuniruka. Hakika nilichofanya ni kutoka mbio nikiwa hoi ndani ya sekunde. Jamani nadhani itafika muda hatutasalimiana kwa kupeana mikono. Haya yamenikuta leo asubuhi.
Hata Iringa Mjini! Nilizani ni jiji DSM tu, Mungu unilinde na hao matapeli, kwa kuwa ni mungwana kwa watu wenye shida.