Hakika spika Makinda hajamwelewa Tundu Lissu.

Ringo Edmund

JF-Expert Member
May 10, 2010
4,879
1,125
Katika kufuatilia kauli ya makinda nimegundua hajamwelewa kamanda lissu.

Lissu alipoongea na wanahabari alitaja majina ya wana ccm walio na mgongano wa maslahi na tanesco na sio waliokula rushwa ili kuikataa bajeti ya wizara ya nishati na madini.kamati aliyounda makinda ni ya kuchunguza rushwa sasa akimwita lissu kutoa ushahidi wa rushwa lissu ataupata wapi?

Na je kuwa na mgongano wa kimaslahi ndio kupokea rushwa?

Madai ni kuwa kuna wala rushwa na wenye mgongano wa kimaslahi.

Naombeni tulidadavue hili wadau.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Katika kufuatilia kauli ya makinda nimegundua hajamwelewa kamanda lissu.
Lissu alipoongea na wanahabari alitaja majina ya wana ccm walio na mgongano wa maslahi na tanesco na sio waliokula rushwa ili kuikataa bajeti ya wizara ya nishati na madini.kamati aliyounda makinda ni ya kuchunguza rushwa sasa akimwita lissu kutoa ushahidi wa rushwa lissu ataupata wapi?
Na je kuwa na mgongano wa kimaslahi ndio kupoke4a rushwa?
Madai ni kuwa kuna wala rushwa na wenye mgongano wa kimaslahi.

Naombeni tulidadavue hili wadau.
Mimi naona wewe ndio hukumwelewa Lissu. Mbona aliweka kila kitu wazi? Na alichosema ni kile kilichosemwa na Waziri Muhongo kama vile biashara ya matairi na mafuta. Huo pekee ni ushahidi na hata Tundu Lissu mwenyewe sidhani kama atashindwa kutoa ushahidi na ninafikiri Spika yupo sahihi
 
Tusubiri tuone mwisho wa jambo hili ni nini.
Mgongano wa kimaslahi ni nini wadau?
Kuchua rushwa ni nini wadau?
 
Ringo kasema kweli. Inashangaza hata Nape kakurupuka kusema kuwa Mh. lissu kataja wala rushwa! Alichotaja Lissu ni watu wenye mgongano wa maslahi (conflict of interest).

Nina hakika Mwanasheria huyu mahiri anachekelea jinsi uelewa wa watu wanokurupuka ulivyo mdogo.

Mgomgano wa maslahi unaweza usiwe ni rushwa bali ukawa ni sababu ya mhusika kutokutenda haki ili kulinda maslahi yake.
 
Nafikiri Lissu atawaambia nilimaanisha 'maadili' mabovu ya utumishi though rushwa ni mojawapo lakini nilimaanisha ilie la 'conflict of interest' na ushahidi ni Waziri wa nishati kupitia hansard!!
 
Katika kufuatilia kauli ya makinda nimegundua hajamwelewa kamanda lissu.
Lissu alipoongea na wanahabari alitaja majina ya wana ccm walio na mgongano wa maslahi na tanesco na sio waliokula rushwa ili kuikataa bajeti ya wizara ya nishati na madini.kamati aliyounda makinda ni ya kuchunguza rushwa sasa akimwita lissu kutoa ushahidi wa rushwa lissu ataupata wapi?
Na je kuwa na mgongano wa kimaslahi ndio kupoke4a rushwa?
Madai ni kuwa kuna wala rushwa na wenye mgongano wa kimaslahi.

Naombeni tulidadavue hili wadau.

Samahani kuuliza; kwani kuna wakati huwa anawaelewa waheshimiwa wa kambi ya upinzani??
 
Hapa kwenye mgongano wa kimasilahi kuna tatizo hili linaanzia kwa viongozi wetu,huwezi kuisimamia wizara na mashirika yake harafu wakati huo ukafanya biashara na mashirika hayo huu ni wizi na ni kosa kimaadili.
Kuhusu rushwa na wizi je hizo kampuni zao zimeorodheshwa na kuonyeswa kwenye kamati ya maadili ya viongozi kuwa wanazimiliki?Kama hakuna basi hilo ni kosa lingine.

Tunahitaji wazalendo katika kulisimamia taifa letu
:A S cry:for TANZANIA
 
Tusubiri tuone mwisho wa jambo hili ni nini.
Mgongano wa kimaslahi ni nini wadau?
Kuchua rushwa ni nini wadau?

Mgongano wa kimaslahi - Conflict of interest
Mfano mdogo ni huu, mfano mimi ni mfanyakazi wa kampuni A meneja usafiri, lakini pia nina kampuni yangu binafsi ya usafirishaji. Sasa haiwezekani mimi leo niamue kuipa kazi kampuni yangu kusafarisha/kubeba mizigo kwenye kampuni ambayo nimeajiriwa yaani kampuni B.
 
Hapa kwenye mgongano wa kimasilahi kuna tatizo hili linaanzia kwa viongozi wetu,huwezi kuisimamia wizara na mashirika yake harafu wakati huo ukafanya biashara na mashirika hayo huu ni wizi na ni kosa kimaadili.
Kuhusu rushwa na wizi je hizo kampuni zao zimeorodheshwa na kuonyeswa kwenye kamati ya maadili ya viongozi kuwa wanazimiliki?Kama hakuna basi hilo ni kosa lingine.

Tunahitaji wazalendo katika kulisimamia taifa letu
:A S cry:for TANZANIA
Kuna nchi za wengine mfano kama wewe ni mkulima wa matunda huruhusiwi kutengeneza juice, lakini hapa una kuna kiwanda kinacho tengeneza juice ndicho kincho safarisha, kinauza jumla jumla wakati huo kina uza rejareja.. hii naamini inatokea hapa kwetu tu.
 
Katika kufuatilia kauli ya makinda nimegundua hajamwelewa kamanda lissu.
Lissu alipoongea na wanahabari alitaja majina ya wana ccm walio na mgongano wa maslahi na tanesco na sio waliokula rushwa ili kuikataa bajeti ya wizara ya nishati na madini.kamati aliyounda makinda ni ya kuchunguza rushwa sasa akimwita lissu kutoa ushahidi wa rushwa lissu ataupata wapi?
Na je kuwa na mgongano wa kimaslahi ndio kupoke4a rushwa?
Madai ni kuwa kuna wala rushwa na wenye mgongano wa kimaslahi.

Naombeni tulidadavue hili wadau.
Katika sheria ya Rushwa kuna kifungu kinachohusiana na kujipatia manufaa au Obtaining advantage without lawful consideration.

Kifungu hicho kinasema ni kosa la rushwa kwa mtumishi wa uma kupokea chochote toka kwa mtumishi ambaye alimhudumia, anamhudumia, au atakuja kumhudumia wakati akitekeleza majukumu yake ya kazi.

Mi si mwanasheria ila mi ninaona kuwa hawa wabunge wajipatia manufaa wakati wakijua kuwa wanaisimamia Tanesco. Hata kama Lisu hakutamka kuwa walipokea Rushwa, kujipatia manufaa toka Tanesco ni kosa la Rushwa.
 
Katika kufuatilia kauli ya makinda nimegundua hajamwelewa kamanda lissu.
Lissu alipoongea na wanahabari alitaja majina ya wana ccm walio na mgongano wa maslahi na tanesco na sio waliokula rushwa ili kuikataa bajeti ya wizara ya nishati na madini.kamati aliyounda makinda ni ya kuchunguza rushwa sasa akimwita lissu kutoa ushahidi wa rushwa lissu ataupata wapi?
Na je kuwa na mgongano wa kimaslahi ndio kupoke4a rushwa?
Madai ni kuwa kuna wala rushwa na wenye mgongano wa kimaslahi.

Naombeni tulidadavue hili wadau.
Haya wewe utakuwa wakili wa LISSU atakapohojiwa na kamati ya maadili ya bunge, Mkuu hilo LISSU analo hawezi kukwepa. Sasa tunaanza kuona hasara ya kuropoka.
 
Kuna nchi za wengine mfano kama wewe ni mkulima wa matunda huruhusiwi kutengeneza juice, lakini hapa una kuna kiwanda kinacho tengeneza juice ndicho kincho safarisha, kinauza jumla jumla wakati huo kina uza rejareja.. hii naamini inatokea hapa kwetu tu.

Mfano nchi kama America huwezi kufanya biashara na taasisi unayo isimamia au kuiongoza Je!wakati hizi kamati zinateuliwa kuna kipengele kinachomzuia mbunge kufanya biashara na shirika au taasisi inayosimamiwa na kamati husika?Kama hakuna basi bunge na serikali walifanya hivyo makusudi
 
Tusubiri tuone mwisho wa jambo hili ni nini.
Mgongano wa kimaslahi ni nini wadau?
Kuchua rushwa ni nini wadau?

Mgongano wa kimaslahi ni dhana pana ndugu Idios.

Kwa ufupi dhana hii inaanzia kwenye malengo ya uwepo wa kampuni au taasisi ya umma/binafsi. Kila kampuni/taasisi ya umma/binafsi inaanzishwa kwa malengo maalumu. Lakini bila kujali aina ya taasisi lengo kuu la taasisi yoyote ile ni kuwapatia ama faida au huduma bora wamiliki wake ambao ndio hasa walengwa wakuu. Haya malengo ya taasisi kwa ujumla wake yanaitwa maslahi ya kampuni au taasisi.

Ili Taasisi ifikie maslahi yake hulazimika kuajiri wafanyakazi ambao jukumu lao kubwa hi kuhakikisha kuwa malengo makuu ya kampuni/taasisi yanafikiwa. Waajiriwa hawa hulipwa mshahara na marupurupu mengine ili waweze kutelekeza majukumu yao bila kuathiri maslahi ya waajiriwa wao. Lakini ni ukweli usiopingika kuwa kila mwajiriwa naye ana malengo binafsi ambayo yanatofautiana toka mtu mmoja mpaka mwingine. Haya malengo binafsi ya waajiriwa mara nyingi yanahitaji pesa zaidi ya mshahara na marupurupu ili kuyafikia. Haya malengo ya waajiriwa kwa ujumla wake yanaitwa maslahi binafsi.

Inapotokea mwajiriwa akatumia mamlaka yake aliyopewa kwa ajili ya kuiwezesha taasisi kufikia malengo yake kupata pesa za ziada ili afikie malengo yake binafsi tunasema kuna mgongano wa maslahi.

Mfano: Mhando wa Tanesco amepewa madaraka ya ukurugenzi mkuu ili aitumikie taasisi yake. Analipwa mshahara na marupurupu kwa ajili hiyo. Inapotokea Mhando akatumia mamlaka yake ya ukurugenzi mkuu wa Tanesco kutoa upendeleo kwa kampuni yake binafsi kupata kazi ya kusambaza stationeries kwa Tanesco anakuwa ameingia kwenye mgongano wa kimaslahi. Kwani ametumia madaraka ya umma kutoa kazi kwa kampuni itakayompatia faida binafsi.

Unaweza ukaipanua dhana hii kwa wabunge ambao wameajiriwa na wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuisimamia Tanesco ili itimize malengo ya kuanzishwa kwake. Wanapotumia nafasi hiyo kushinikiza na kupata biashara ya kusambaza mafuta ama bidhaa nyingine yoyote kwa shirika la Tanesco wanakuwa na mgongano wa kimaslahi kwani hawawezi tena kuisimamia Tanesco.

Kuchukua rushwa
ni kupewa pesa au upendeleo mwingine wowote ili ufanye maamuzi yanayompendelea yule aliyekupa pesa au kitu kingine chochote.
 
siwezi kuchangia mengi masikini tz inadidimia ardhini kila mwenye nafasi kidogo anazoa kilichopo,watu wanakula bila kunawa.ooooooooooh tz tunakupoteza kwa moyo wote.
 
Natamani Mwl.Nyerere afufuke asimamie maadili ya viongozi.Jambo la conflict of interest linawatesa Watanzania wengi.Viongozi wa umma ambao ndio wasimamizi wa mali/maslahi ya umma ndio wafanyabiashara wakubwa na hao hao ndio wenye tenda nyingi katika mashirika ya umma.Kutokana hali hiyo kiongozi wa umma ambaye anayotenda mahali anapofanyia kazi i.e shirika la umma kamwe hawezi kulinda maslahi ya umma bali maslahi ya kampuni yake iliyopewa tenda ndani ya shirika la umma analoliongoza.Tokea raisi awamu ya tatu ndipo watumishi wengi walipoteza haki ya nyongeza ya mishahara kwa sababu wasimamizi wa haki za watumishi ndio wana makampuni makubwa hivyo kwa viongozo hao kukubali nyongeza za mishahara maana yake kampuni zao zinapunguza mapato kwa kulipa mishahara mikubwa!! Taifa limepotoka afufuke Mwalimu awachape bakora na kuwaweka vizuizini!
 
Kinachonishangaza kwenye hili ni kwa vipi jambo lililozungumzwa kwenye ofisi ya upinzani bungeni liwe na kinga ya bunge.Nilifikiri kuwa hili liwe suala la mahakamani badala ya kamati ya haki na madaraka ya bunge.Lakini kwa kutumia tafsiri mpya ya bunge ya bw.Ndugai siku ile alipomtoa Mnyika nje ya ukumbi wa bunge alisema kuwa aende nje kabisa kwa kuwa hata viunga vya nje ya ukumbi wa bunge ni ukumbi wa bunge bado!

Kuna haja ya kuangalia upya tafsiri hizi za maneno kwenye kanuni za bunge kwani kwa mtazamo wangu mara nyingi kiti kinatoa tafsiri yenye maslahi nacho.Ni kwa jinsi gani jambo lililoongelewa nje ya ukumbi wa bunge linakuwa counted kama vile limezungumzwa kwenye ukumbi wa bunge.

Mpaka sasa ni mambo mangapi upinzani wamezungumza kwenye hiyo ofisi yao ndogo hapo bungeni.Je yote yana kinga ya bunge au ni hili tu?

Na kama Zitto pia leo ataitumia ofisi hiyo wakati akiongea na waandishi wa habari ina maana yote atakayoongea tayari yana kinga ya bunge na mtu yeyote hawezi kumshtaki mahakamani bila kupitia kanuni za bunge?
 
Ringo kasema kweli. Inashangaza hata Nape kakurupuka kusema kuwa Mh. lissu kataja wala rushwa! Alichotaja Lissu ni watu wenye mgongano wa maslahi (conflict of interest).

Nina hakika Mwanasheria huyu mahiri anachekelea jinsi uelewa wa watu wanokurupuka ulivyo mdogo.

Mgomgano wa maslahi unaweza usiwe ni rushwa bali ukawa ni sababu ya mhusika kutokutenda haki ili kulinda maslahi yake.

Ni kweli mkuu, tatizo watu huwa wana generalise sana statements za Lissu, hawajui kuwa unatakiwa uziangalie kwa jicho la tatu! Manake huwa hakurupuki na taaluma yake ya Sheria inampa uelewa mkubwa sana, nashangaa watu wasiojua maana ya "Mtu mwenye Conflict of Interest" na yule ambaye ni Mla Rushwa, japo Conflict of Interest ina association kubwa tu na rushwa!
 
Haya wewe utakuwa wakili wa LISSU atakapohojiwa na kamati ya maadili ya bunge, Mkuu hilo LISSU analo hawezi kukwepa. Sasa tunaanza kuona hasara ya kuropoka.

hii nchi itakuja kuendelea tu kama mijitu kama ninyi asilimia 20 ipotezwe!
 
Katika kufuatilia kauli ya makinda nimegundua hajamwelewa kamanda lissu.

Lissu alipoongea na wanahabari alitaja majina ya wana ccm walio na mgongano wa maslahi na tanesco na sio waliokula rushwa ili kuikataa bajeti ya wizara ya nishati na madini.kamati aliyounda makinda ni ya kuchunguza rushwa sasa akimwita lissu kutoa ushahidi wa rushwa lissu ataupata wapi?

Na je kuwa na mgongano wa kimaslahi ndio kupokea rushwa?

Madai ni kuwa kuna wala rushwa na wenye mgongano wa kimaslahi.

Naombeni tulidadavue hili wadau.

Ndio sababu ni muhimu sana kiti cha Spika kikakaliwa na mtu aliyesomea sheria. Kanuni za bunge ziko wazi kabisa, kwamba kama mbunge ana maslahi kwenye jambo/shirika lazima aweke wazi. Baadhi ya wabunge wa CCM ambao wako kwenye kamati ya nishati na madini wanafanya biashara na Tanesco (e.g. supply matairi) lakini wakati huo huo wanaisimamia Tanesco! Na mbaya zaidi hawakuweka wazi mgongano huu wa kimaslahi kama ambavyo kanuni za bunge zinavyoelekeza.

Mgongano huu maslahi ndio aliousema Prof Muhongo na ndicho hicho hicho alichosema Lissu. Tofauti ni kwamba Lissu kataja majina ya wabunge wenye maslahi. Tukumbuke uongozi wa Tanesco uliosimamishwa ndio uliotoa tender kwa hao wabunge waliotuhumiwa hivyo kitendo cha wao (wabunge) kumtetea Mhando wa Tanesco kinaweza kutafsiriwa kuwa ni kutetea 'tender' zao maana akiondoka Mhando mambo yanaweza kuwaendea kombo.


Sielewe utashi wa Spika kwenye hili maana amerukia upande wa mipasho wakati anajua fika hoja iliyosemwa na Lissu ya mgongano wa maslahi. Tuna kazi sana.
 
Back
Top Bottom