Hakika mapenzi ni darasa tosha, nahitaji ushauri wako!!

Hakika mapenzi ni darasa tosha, nahitaji ushauri wako!!

chakii

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2013
Posts
21,576
Reaction score
28,497
Heshima kwenu wana MMU.

Nimeadimika sana hapa Jamvini ingawa huwa napitia kuzisoma post za wadau mara kwa mara.

Wakuu nisiwachoshe sana, niingie kwenye mada iliyonileta hapa.

Nina mpenzi wangu ambaye tupo naye kwenye mahusiano takriban miaka miwili sasa, tumekuwa tukishirikiana katika hali na pale tunapokwazana huwa tunafikia muafaka na kuondoa tofauti zetu.

Mpenzi wangu huyu bado yupo Chuo Jijini Dar akichukua masomo ya Usimamizi wa biashara na akaunti na mimi kwa sasa nipo nje ya Jiji kwa majukumu yangu ya kikazi.

Huyu binti nilishamuahidi kuanzisha naye familia Mungu akijalia.

Kuna wakati mawasiliano yetu yanakuwa hafifu sana lakini mara nyingi hili jambo halileti tatizo kwani tunaaminiana.

Wiki kama mbili hivi zilizopita amepata eneo la kufanya mazoezi kwa vitendo (field) katika ofisi fulani ya uhasibu Jijini Dar.

Jana tumewasiliana kaniambia kuna jamaa hapo ofisini kwao anapofanyia field kuna Principal accountant ametokea kumtongoza na anaendelea kumsumbua sana licha ya yeye kumuambia tiyari ana mpenzi ambaye ni mimi.

Wakuu huyu mpenzi wangu amekosa raha kabisa katika eneo hiki analolifanyia field work.

Nilimuuliza jina lake akanitajia, pia nilimuambia anipatie namba ya huyo Jamaa niwasiliane naye na nimuambie aache kumsumbua mpenzi wangu, lakini mpenzi wangu aliniambia jamaa akimpigia simu huwa hapokei simu yake na anazifuta namba zake, ila kaniambia akishazipata atakapopiga tena au ataziomba kwa wenzake atanipatia, yupo na wenzake sita katika eneo hilo lakini yeye ndiye anasumbuliwa sana.

Mpenzi wangu ni wa kawaida, siyo wa kuwatisha wanaume kiviile lakini kuna kitu fulani ndani yake nimekipenda na nisingependa kukipoteza kamwe ndiyo maana nataka awe mwenzi wangu.

Wana MMU naombeni ushauri wenu juu ya hili Jambo, na nitakapozipata hizo namba nifanyeje maana nisingependa kumpoteza mpenzi wangu, pia vilevile nisije nikaharibu matokeo yake ya field work baada ya kuongea na huyo Principal accountant wao akapoteza marks,..

Natanguliza shukrani wakuu,..
 
field ni somo moja tu, atacompasate kwa mengine, mke ni wa kudumu. Mpigie.

Ila inawezekana keshalambwa anajistukia.
 
field ni somo moja tu, atacompasate kwa mengine, mke ni wa kudumu. Mpigie.

Ila inawezekana keshalambwa anajistukia.

Inawezekana mkuu ila pia nahisi anapima upepo aangalie ni namna gani nita react katika hili,.

Naona namba itatoa proof ya hili,.
 
Heshima kwenu wana MMU.

Nimeadimika sana hapa Jamvini ingawa huwa napitia kuzisoma post za wadau mara kwa mara.

Wakuu nisiwachoshe sana, niingie kwenye mada iliyonileta hapa.

Nina mpenzi wangu ambaye tupo naye kwenye mahusiano takriban miaka miwili sasa, tumekuwa tukishirikiana katika hali na pale tunapokwazana huwa tunafikia muafaka na kuondoa tofauti zetu.

Mpenzi wangu huyu bado yupo Chuo Jijini Dar akichukua masomo ya Usimamizi wa biashara na akaunti na mimi kwa sasa nipo nje ya Jiji kwa majukumu yangu ya kikazi.

Huyu binti nilishamuahidi kuanzisha naye familia Mungu akijalia.

Kuna wakati mawasiliano yetu yanakuwa hafifu sana lakini mara nyingi hili jambo halileti tatizo kwani tunaaminiana.

Wiki kama mbili hivi zilizopita amepata eneo la kufanya mazoezi kwa vitendo (field) katika ofisi fulani ya uhasibu Jijini Dar.

Jana tumewasiliana kaniambia kuna jamaa hapo ofisini kwao anapofanyia field kuna Principal accountant ametokea kumtongoza na anaendelea kumsumbua sana licha ya yeye kumuambia tiyari ana mpenzi ambaye ni mimi.

Wakuu huyu mpenzi wangu amekosa raha kabisa katika eneo hiki analolifanyia field work.

Nilimuuliza jina lake akanitajia, pia nilimuambia anipatie namba ya huyo Jamaa niwasiliane naye na nimuambie aache kumsumbua mpenzi wangu, lakini mpenzi wangu aliniambia jamaa akimpigia simu huwa hapokei simu yake na anazifuta namba zake, ila kaniambia akishazipata atakapopiga tena au ataziomba kwa wenzake atanipatia, yupo na wenzake sita katika eneo hilo lakini yeye ndiye anasumbuliwa sana.

Mpenzi wangu ni wa kawaida, siyo wa kuwatisha wanaume kiviile lakini kuna kitu fulani ndani yake nimekipenda na nisingependa kukipoteza kamwe ndiyo maana nataka awe mwenzi wangu.

Wana MMU naombeni ushauri wenu juu ya hili Jambo, na nitakapozipata hizo namba nifanyeje maana nisingependa kumpoteza mpenzi wangu, pia vilevile nisije nikaharibu matokeo yake ya field work baada ya kuongea na huyo Principal accountant wao akapoteza marks,..

Natanguliza shukrani wakuu,..

Subiri utapewa namba ya mtu ambaye ameisha mseti tayari. Chezea mwanamke wewe.
 
Cha kufanya mwambie mpenzi wako atunze ahadi mliyowekeana pasipo hata wewe kumpigia simu Huyo mwanaume kwa sababu aitasaidia kitu Kama mwanamke akiamua atakudanganya tu. Cha kufanya mwambie Mke mtarajiw awe makini
 
Achana na huyo jamaa,mpenziyo ndiye wa kudeal nae,just mweleze unavyompenda na usingependa kumpoteza,
naamini huyo siyo mwanaume wa kwanza kumtongoza.
Kama bidada ni mwelewa ataelewa,
 
Cha kufanya mwambie mpenzi wako atunze ahadi mliyowekeana pasipo hata wewe kumpigia simu Huyo mwanaume kwa sababu aitasaidia kitu Kama mwanamke akiamua atakudanganya tu. Cha kufanya mwambie Mke mtarajiw awe makini

Ahsante kwa ushauri mkuu,.

Najiuliza kwanini alinishirikisha jambo hili? Ili nifanyeje?
 
Ulishaharibu deal toka mapema.

Alivyokupigia mwambie uamuzi ni wake, mpe uhuru wa kuamua atakavyo.

Na wewe uanze u-FBI wa kimyakimya.
 
Mkuu wanawake kwenye mapenz wanaakili moja ya kaulaghai sana.
Anaweza kukuambia hvyo kumbe ni defence yake juu ya mahusiano yao ili ww hata sku ukikuta msg isikustue.
Hapo ww kaa naye chini mkanye yeye kama yeye.
- hvi wakat mnaanza mahusiano ulimkuta bikra?
- na kama hukumkuta bikra vp aliwahi kukwambia waliomtoa bikra?
- au amewahi kukwambia idadi ya wanaume aliotoka nao kabla na baada ya kuwa na ww?
 
Ku-date watoto wa chuo ni kazi sana..! Mie sijui mnawezaje aisee!!
 
Aaaaaaaaaaaa!! Humu maofisini nini gf, hadi wake za watu wanapigwa free p tu wakijilegeza! Sasa gf wako anaenda ofisi za watu, anacheka cheka, mpasuo huo, mini hizo, anawadolishia wasimtongoze kaka zake wale? Wanamjaribu tu sio kiwa wanamtaka sanaaaa, akiwa strict wanasepa, akiachia wanakamua mzigo na kuzindua album kama kawaida!
 
Ulishaharibu deal toka mapema.

Alivyokupigia mwambie uamuzi ni wake, mpe uhuru wa kuamua atakavyo.

Na wewe uanze u-FBI wa kimyakimya.

Sawa kabisa mkuu, nilimuuliza yeye kaamua vipi? Akanijibu hayupo tayari kuwa naye. Tatizo Jamaa bado anamsumbua sana,.

Mimi nipo mkoani kikazi!
 
Back
Top Bottom