kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
Naitwa Yohana Benjamin, nimezaliwa mwaka 1993 Kigoma.
Nimesoma shule ya msingi Kabanga mazoezi, Kigoma wilaya ya Kasulu. Mimi nina ulemavu wa miguu, hata hivyo nimebahatika kumaliza na kufaulu vizuri mtihani wa darasa la saba (7) mwaka 2010.
Nilibahatika kupangiwa Shule ya Sekondari Mwadui , Shinyanga. Mwalimu mkuu wa Shule ya Sekondari Mwadui alinipokea vizuri sana lakini akawa na wasiwasi mkubwa sana juu ya mahitaji muhimu kwangu kutokana na aina ya ulemavu wangu. Kwa mfano, mazingira ya pale shule kama vile kupanga ngazi, au kwenda kujisaidia ndio ilikuwa changamoto kwa Mwl Mkuu wangu na mimi mwenyewe.
Ilifika mahali nikajipangia kula mlo mmoja wa jioni tuu, ili nisije kuhitaji kujisaidia mchana. Ikifika usiku nawaomba wenzangu wanisaidie kunisindikiza kwenye vichaka ndio nipate kujistiri.
Hali hii ilinisumbua mimi na mwl mkuu wangu, ikabidi nifanye uamuzi wa kwenda kuomba msaada kwa afisa elimu wa wilaya na hatimae afisa elimu mkoa, lakini kwa bahati mbaya wote walishindwa jinsi ya kuniwekea mazingira yakuniwezesha kuendelea na masomo. Nikarudi nyumbani.
Siku kata tamaa, nika amua kuja DSM kuonana na Idara ya Elimu Maalum, Wizara ya Elimu na Ufundi. Mungu si Athumani, nimemkuta Bwana Mwiga Afisa katika Idara hii, ndio amekubali kunipa barua nikajiunge na Shule ya Sekondari Pugu.Ndugu zangu mtakajaaliwa kuona taarifa hii, ninacho omba kwenu nisaidiwe kupata wheel chair inayonifaa kujisukuma kwenda darasani kutoka bweni na kwengineko.
Katika picha hii, kigari kinacho nisaidia nimebuni na kutengeneza mwenyewe baada ya kusaidiwa kuletewa vifaa kama mnavyoona. Najiendesha kwa kutumia mkono mmoja kuendesha usukani na mkono wa kulia ndio najisukumia chini.
Nina penda na kumudu masomo ya sayansi, hisabati na maarifa ya jamii. Malengo yangu ni kusoma hadi chuo kikuu. Nikiwezeshwa nitaweza.
Hapa DSM nimepokewa na ndugu yangu Bw. Robert Revocatus cm 0763 299960 au 0714 495951
Nimesoma shule ya msingi Kabanga mazoezi, Kigoma wilaya ya Kasulu. Mimi nina ulemavu wa miguu, hata hivyo nimebahatika kumaliza na kufaulu vizuri mtihani wa darasa la saba (7) mwaka 2010.
Nilibahatika kupangiwa Shule ya Sekondari Mwadui , Shinyanga. Mwalimu mkuu wa Shule ya Sekondari Mwadui alinipokea vizuri sana lakini akawa na wasiwasi mkubwa sana juu ya mahitaji muhimu kwangu kutokana na aina ya ulemavu wangu. Kwa mfano, mazingira ya pale shule kama vile kupanga ngazi, au kwenda kujisaidia ndio ilikuwa changamoto kwa Mwl Mkuu wangu na mimi mwenyewe.
Ilifika mahali nikajipangia kula mlo mmoja wa jioni tuu, ili nisije kuhitaji kujisaidia mchana. Ikifika usiku nawaomba wenzangu wanisaidie kunisindikiza kwenye vichaka ndio nipate kujistiri.
Hali hii ilinisumbua mimi na mwl mkuu wangu, ikabidi nifanye uamuzi wa kwenda kuomba msaada kwa afisa elimu wa wilaya na hatimae afisa elimu mkoa, lakini kwa bahati mbaya wote walishindwa jinsi ya kuniwekea mazingira yakuniwezesha kuendelea na masomo. Nikarudi nyumbani.
Siku kata tamaa, nika amua kuja DSM kuonana na Idara ya Elimu Maalum, Wizara ya Elimu na Ufundi. Mungu si Athumani, nimemkuta Bwana Mwiga Afisa katika Idara hii, ndio amekubali kunipa barua nikajiunge na Shule ya Sekondari Pugu.Ndugu zangu mtakajaaliwa kuona taarifa hii, ninacho omba kwenu nisaidiwe kupata wheel chair inayonifaa kujisukuma kwenda darasani kutoka bweni na kwengineko.
Katika picha hii, kigari kinacho nisaidia nimebuni na kutengeneza mwenyewe baada ya kusaidiwa kuletewa vifaa kama mnavyoona. Najiendesha kwa kutumia mkono mmoja kuendesha usukani na mkono wa kulia ndio najisukumia chini.
Nina penda na kumudu masomo ya sayansi, hisabati na maarifa ya jamii. Malengo yangu ni kusoma hadi chuo kikuu. Nikiwezeshwa nitaweza.
Hapa DSM nimepokewa na ndugu yangu Bw. Robert Revocatus cm 0763 299960 au 0714 495951