Hakijanyooka lakini wamejitahidi

Hakijanyooka lakini wamejitahidi

Hawa ni Askari Polisi wa Tanzania wakimhoji binti wa Nigeria mwendesha pikipiki. Ametokea Uganda na ameeleza kuwa angeenda kupumzika/ kulala Kibondo.

Japo Kizungu cha "makamanda" wetu hakijanyooka kivile, lakini mawasiliano yamefanikiwa. Kila mmoja ameweza kumwelewa mwenzake, na hilo ndilo lengo la lugha, mawasiliano.
Hakuna shida kabisa na kiingreza chao. Tena wameongea vizuri ukifananisha na polisi wa nchi ambazo hazitumii kiingereza kama Ujerumani au Sweden.
 
Hawa ni Askari Polisi wa Tanzania wakimhoji binti wa Nigeria mwendesha pikipiki. Ametokea Uganda na ameeleza kuwa angeenda kupumzika/ kulala Kibondo.

Japo Kizungu cha "makamanda" wetu hakijanyooka kivile, lakini mawasiliano yamefanikiwa. Kila mmoja ameweza kumwelewa mwenzake, na hilo ndilo lengo la lugha, mawasiliano.

Always nice for foreigners and if u do not have any problem
 
How many cc? Two fifty.

Wao: MIA HAMSINI

Dah inasikitisha sana. Hata mtoto wangu wa darasa la pili anajua two fifty ni mia mbili hamsini.
Umewahi kutembelea nchi zilizoendelea ambazo hazitumii english? Hali ya polisi wao kwenye kuzungumza kiingereza ni mbaya zaidi. Labda utasema sisi tunajifunza kiingereza tangu shule za msingi? Elimu yetu nadhani unaijua.
 
Umewahi kutembelea nchi zilizoendelea ambazo hazitumii english? Hali ya polisi wao kwenye kuzungumza kiingereza ni mbaya zaidi. Labda utasema sisi tunajifunza kiingereza tangu shule za msingi? Elimu yetu nadhani unaijua.
Sikatai mkuu na kuna nchi zimeendelea wala hawana habari na kiingereza. Ila kwetu sisi tunasoma kiingereza kuanzia level za chini ni ajabu ukute mtu amehitimu walau form four hajui kuwa two fifty ni mia mbili hamsini.
 
Ni kweli mkuu, kama kisingeeleweka asingekuwa anajibu! Makamanda kinawatosha kwa level yao! Hawa tujue wengi wao ni form failure yaani wanamzidi kidogo tu Mh. Musukuma! Kiingereza chao hakina tofauti na cha Mchina!
Kama mimtu ina akili tena imesoma pcm but engilish ni tatizo mzee

By the way kuna mwalimu fulani hivi yuko mkoa wapwani Hingh School kaajiriwa 2017 ni mzuri sana mathe + phy but kwenye ngere ya kuongea hayupo vzuuri najikanyaga sana!

Hivyo akili ya mtu haipimwi kwakujua kiingereza!
 
Sikatai mkuu na kuna nchi zimeendelea wala hawana habari na kiingereza. Ila kwetu sisi tunasoma kiingereza kuanzia level za chini ni ajabu ukute mtu amehitimu walau form four hajui kuwa two fifty ni mia mbili hamsini.
Mkuu. Inawezekana hakusikia vizuri. Mbona hata kiswahili mtu anaweza kukusemesha lakini ukaelewa kivingine? Hili la kusoma shuleni da... nadhani utakuwa hutendi haki kwa sababu siyo kiingereza tu bali ni kila kinachofundishwa kwenye shule hizi zetu kinakuwa changamoto kwa wahitimu.
 
Police huwa hawana shida sana na bikes sema basi walitaka TU kumfurahia Wala wasingeomba kitu kimsingi huwa wako poa shida ni pale wanapopewa oda za lazima na wale wakubwa wao ndipo shida huanzia
 
Hapo kamera ndio amekuwa mkombozi wa huyo rider. Jamaa anakamera, inarekodi kila kitu. Polisi gani wasitake kukagua nyaraka 😀😀.

Hizi kamera nimezieelewa sana, ni muhimu kuziweka katika vyombo vyetu vya moto na ofisi zote za umma zinazohudumia .

Inarekod kila kitu, 😂😂
 
Back
Top Bottom