Haki za Marehemu

Maamuma

JF-Expert Member
Dec 22, 2008
848
303
Wapendwa wanaJF, Heshima mbele!
Nimekuwa nikitafakari kuhusu haki za marehemu. Hivi marehemu anakuwa hana haki tena ya kuwa na siri? Mtakubaliana nami kwamba siku hizi kuna utaratibu wa kusoma wasifu wa marehemu wakati wa maziko. Kati ya vitu vinavyotajwa ni pamoja na umri, elimu, kazi alizowahi kufanya, idadi ya watoto na pengine idadi ya wake (wives), chanzo cha kifo, n.k.
Mfano: Watu wengi katika uhai wao hawapendi kutaja umri wao (mimi simo). Inakuwaje basi mtu aliyekuwa anaficha umri wake atajiwe tarehe au mwaka wake wa kuzaliwa anapokuwa marehemu?

Mbaya ni kwamba hakuna Chama cha Marehemu (kifupi CCM? Kibunango usinipige viboko) kinachoweza kutetea maslahi yao na wala hawawezi kuandamana kutoa kilio chao.

Mi nadhani habari yoyote ambayo mtu aliifanya siri yake, basi ibaki kuwa siri milele. Mnalionaje hili wanaJF?
 
Nalo ni Neno!

Lakini na ieleweke kwamba mtu huficha particulars zake akiwa hai kwa malengo fulani.

Wengine huficha umri kuhofia kuonekana wamechoka, na hivyo kupunguzwa makazini.

Wengine hufanya hivyo ili wakubaliwe na mademu,
Wengine hufanya hivyo ili asitendewe kitu fulani asichokipenda, au apate favor flani, na kadhalika.
Lakini mtu akishakufa, mambo yote ya kufichaficha huonekana hayana maana yoyote, na hivyo ndipo ukweli hudhihirika.
 
Ni suala pana kiasi. Kwa Upande wa Waislam , Marehemu ana haki zifuatazo
1. Kusitiriwa baada ya kufa ( yaani kufunikwa baada ya kifo.
2. Kuoshwa
3. kuvishwa sanda
4. kuhakikisha kuwa madeni yake ( wale anaowadai na wanaomdai) yanalipwa kwa waridhi wake au kuweka makubaliano nao namna ya kulipwa au kulipa.
5Kuswaliwa
6. Kuzikwa.


Haki hizo zinatakiwa zitimizwa haraka sana mara mtu anapofariki.
 
swala zima linakuja kwenye mirathi.kama tutakuwa na utamaduni wa kuandika mirathi kabla ya mauti basi kila unachotaka kinaweza kuwekwa katika mirathi yako.tatizo letu ni kuwa tunaona mirathi kama vile ni uchuro eti mtu unakuwa unajitabiria kufa,kumbe si hivyo.swala la kuacha mirathi linalenga kulinga haki zako wewe pale utapokuwa umefariki na kwa wale unowaacha nyuma yako,wanao,mkeo au wakeo na ndugu wengine wa familia.
walio na elimu ya sheria wasaidie hapa.....
 
....Hivi kuna watu wana kasumba ya kuficha umri wao dunia ya leo!!!
Na hili tatizo la kuficha umri lipo haswa developing countries, ughaibuni hawana kitu kama hichi cha kuficha ficha umri kila mtu yupo huru kueleza umri wake na si kudanganya, kwani umri wala si siri.
 
.... kila mtu yupo huru kueleza umri wake na si kudanganya,
.....uhuru unahusu kuficha au kutokuficha,ndio uzuri wa mtu kuwa huru.kwa hiyo kuficha umri pia ni uhuru wa mtu kama ulivyo uhuru wa mwingine kutokuficha umri.........
 
Ni suala pana kiasi. Kwa Upande wa Waislam , Marehemu ana haki zifuatazo
1. Kusitiriwa baada ya kufa ( yaani kufunikwa baada ya kifo.
2. Kuoshwa
3. kuvishwa sanda
4. kuhakikisha kuwa madeni yake ( wale anaowadai na wanaomdai) yanalipwa kwa waridhi wake au kuweka makubaliano nao namna ya kulipwa au kulipa.
5Kuswaliwa
6. Kuzikwa.


Haki hizo zinatakiwa zitimizwa haraka sana mara mtu anapofariki.
Asante Mkuu kwa ufafanuzi huo. Lakini labda title nimeiweka vibaya. Nilikuwa nalenga hasa katika hoja ya kuendelea kusitiri siri za marehemu au yale mambo ambayo marehemu hakutaka yajulikane wakati wa uhai wake. Mpaka hapo?
 
Back
Top Bottom