Haki Za Binadamu Wamgeukia RC Makonda

Haki Za Binadamu Wamgeukia RC Makonda

Hao haki za binaadamu waende bilicanas kwa Mbowe wakaone wafanyakazi wanavyoteseka bila mishahara mwezi wa nne (ripoti imo humu JF).

Achana na Makonda, wao walikuwa wanaona raha huyo mtoto kudhulumiwa urithi wake? Mbona wasimtetee aliodhulumiwa haki yake na hao hao watu ardhi?
 
Huyu mtoto ni aibu kwa wateuzi wake, na amevaa taswira ya hao waliomteua.
Kakosa adabu,misingi na maadili ya kiutu na nidhamu.
 
Dkt. Helen Kijo-Bisimba, mama yangu utapata presha bure na hawa watu. Siku zote kiongozi akishalewa madaraka hekima na busara hukimbia na hivyo hujikuta akiongozwa na mihemko.Huitaji kudhalilisha watu ili uonekane mtendaji. lugha ya staha inatosha kabisa kufanya watu wakuheshimu hata bila kuwalazimisha.Lakini jambo la kushangaza wakati ndugu huyo anawadhalilisha hao wafanyakazi kuna raia waanashangilia.Kila ninapoisikia kauli alizotoa huyo mtu nasikia kuudhika kiasi ambacho najiuliza,je kuwa kiongozi ni lazima utumie mabavu?MY LORD FORGIVE US!

Tatizo tumeshasahau wajibu wetu kama RAIS.Tukikumbuka wajibu wetu tutawanyoosha watawala wa sampuli hii
 
mbona watumishi tusipotekeleza majukumu yetu haki za bidamu hawasimami?? au wananchi wanaotumikia hawana haki za kibinadamu kama Wao???

Hivi unajua chimbuko la haki za binadamu na mashirika au taasisi zinazotetea haki hizo? na zinatetewa zinapokuwa zimepokonywa na nani?. wewe mtumishi usipotimiza majukumu yako mamlaka ya ajira yako ipo itakushughulikia bila kuvunja haki zako ila ikitokea umevunjiwa haki zako wewe binasi huwezi kuzipigania ni lazima taasisi kama hizi zikutetee. wewe unaona hiyo kauli ya mungu makondaa ni sahihi dhidi ya huyo mama?
 
tobaa!! wanataka na wao? hivi yule mtz aliopigwa mpk kufa na yule mchina haki za binadamu waliingilia kati..?

Wenye mamlaka ya kulinda raia ni serikali kabla hujauliza haki za binadamu ilifanya nini ,ungeuliza serikali yenye jeshi ,polisi na mahakama ilifanya nini ,usitake kuwapuuza haki za binadamu kwa uzembe wa serikali idiot.
 
makonda anachokifanya sijui anamatatuzo gani kichwani? hakika imeniuma sana
 
Mimi binafsi bado sijaona mantiki ya hilo genge linalojiita kuwa ni watetezi wa haki za binadamu....maana sielewi ni binaadamu yupi wanayemtetea na haki zipi wanazozitetea zaidi ya watu wanaoongozwa na mihemko........

Au labda wanamaanisha ni haki za viongozi kutowajibishwa wanaposhindwa kutekeleza wajibu wao....maana naona kwao viongozi ni binaadamu pekee ammbao haki zao hazipaswi kuvunjwa.......

Kimsingi ni kwamba hao viongozi wanaposhindwa kutekeleza wajibu na kwenda kinyume na taratibu maana yake ni kuwa wanavunja haki za binaadamu wengine....( pengine kwa tafsiri yao sio wanadamu).....

Daktari anapokataa kumtibu mgonjwa ambaye amegoma kumpa rushwa na mgonjwa aakafariki kwa kukosa matibabu maana yake ni kwamba amedhurumu haki ya mgonjwa ya kuishi.......

Mtoa huduma anaposhindwa kutoa huduma kwa kukosa rushwa maana yake amewadhurumu haki zao hao watu.....
Sasa sijui ni haki ipi inayozungumziwa.........

Wanyonge wamekuwa wakinyanyasika kwenye taifa kana kwamba ni wakimbizi huku huko ofisi zinazojiita kuwa ni watetezi wa haki za binadamu walishinda ofisini na kula kuku kwa mrija.......

Wao wamekuwa watu wa kungoja matukio tu.....ndio unashtuka kuwa kumbe nao wapo......

Ieleweke kuwa sitetei uvunjifu wowote wa haki za binadamu bila kujali kuwa amefanyiwa nani au amefanya nani na kwa wakati gani.....

NB; kauli ya Makonda dhidi ya huyo mama imekosa hekima ya kiuongozi..( kama kweli ameyatamka hayo)...,,
 
Hao haki za binaadamu waende bilicans kwa Mbowe wakaone wafanyakazi wanvyoteseka bila mishahara mwezi wa nne (ripoti imo humu JF).

Achana na Makonda, wao walikuwa wanaona raha huyo mtoto kudhulumiwa urithi wake? Mbona wasimtetee aliodhulumiwa haki yake na hao hao watu ardhi?

Nadiriki kusema kuwa Haki za binaadamu wanatumika kisiasa......ingawa najitahidi kupambana ukweli huo....
 
Wenye mamlaka ya kulinda raia ni serikali kabla hujauliza haki za binadamu ilifanya nini ,ungeuliza serikali yenye jeshi ,polisi na mahakama ilifanya nini ,usitake kuwapuuza haki za binadamu kwa uzembe wa serikali idiot.
nafahamu nachojaribu kuangalia hapa ni nguvu ya lile na hili la makonda nadhani utakuwa umeshanipata
 
Kwa upande wangu sijaona kosa la mheshimiwa makonda acha awanyooshe walizoea sana hata ilikuwa ukifika ktka ofisi zao wanakuangalia kama kinyago kwa sasa hayo mambo acha yakomeshwe. Makonda oyeeeeeee

Ninachokiona kwenye uzi huu ndugu ni watu waliokuwa na fikra hasi dhidi ya Makonda hivyo kupelekea wao kuona kuwa kila jambo analofanya ni baya......,

Kama ulishawahi na bado unakumbana na kero za hao watumishi huko kwenye ofisi zao utakuwa unaelewa Makonda anamaanisha nini ingawa hatua anazochukua si sahihi.....
 
Na yeye kwa kutokuwajibika kwake achukuliwe hatua gani huyo Afisa ardhi

I Hope Makonda aliteleza tu katika kuongea
Kwa hiyo kila siku yeye ni wakuteleza tu sjui sheria inasema nini kwa mtu mzalilishaji,nazani ni vyema ss kuitazama hiyo sheria, mungu ni mmoja tu na wala hakuna MUNGU mwingine zaidi yake ss kiburi humdanganya mpumbavu na kuzani yu mwanzo pia mwisho
 
Sasa hapa Makonda kakosea nini? Makonda kataka mtu anaejuwa swala hilo kanyanyuka huyo mwanamke ambae hana majibu, ni punguani huyo mwanamke si bure.



Makonda alichokifanya sawasawa, wamezowea "shortcuts" na uongo na wanafikiri kila mtu anadanganyika "anasomeshwa".

Makonda anataka majibu wao wanaleta porojo na kubwabwaja bila mpango.
 
Back
Top Bottom