Gaston Mbilinyi
JF-Expert Member
- Jan 24, 2010
- 296
- 51
WanaJF,
Jana nilikuwa nasafiri kwa daladala tokea Mzumbe kwenda Morogoro(M). Njiani tukasimamishwa na trafik ambaye alimchukua kondakta wa daladala hiyo wakawa na mjadala kwa takribani nusu saa mbali na lilipokuwapo gari. Abiria tulipoomba kuwa ama tupelekwe tuendako na wenye gari wafikishwe katika vyombo sheria iwapo yako makosa yaliyofanywa kisheria au tuambiwe gari mbovu ili turudishiwe nauli ili tupande gari lingine. Trafik waliokuwapo hapo wakawa wakali kwa madai kuwa tunawaingilia kazi na wanaweza kutufikisha kituo cha Polisi na baadae kufikishwa mahakamani.
Kwa majibu hayo ya trafik ilibidi abiria tuwe wapole, lakini swala hilo lilinipa cha kufikiri na hatimaye sijapata jibu na ndio maana nikaona niombe msaada wenu wanaJF ili mnielimishe kama siku nyingine nifanyeje ikitokea hali kama hiyo maana naona kama haki yetu abiria ilikuwa inadhurumiwa tu. NISAIDIENI!
Jana nilikuwa nasafiri kwa daladala tokea Mzumbe kwenda Morogoro(M). Njiani tukasimamishwa na trafik ambaye alimchukua kondakta wa daladala hiyo wakawa na mjadala kwa takribani nusu saa mbali na lilipokuwapo gari. Abiria tulipoomba kuwa ama tupelekwe tuendako na wenye gari wafikishwe katika vyombo sheria iwapo yako makosa yaliyofanywa kisheria au tuambiwe gari mbovu ili turudishiwe nauli ili tupande gari lingine. Trafik waliokuwapo hapo wakawa wakali kwa madai kuwa tunawaingilia kazi na wanaweza kutufikisha kituo cha Polisi na baadae kufikishwa mahakamani.
Kwa majibu hayo ya trafik ilibidi abiria tuwe wapole, lakini swala hilo lilinipa cha kufikiri na hatimaye sijapata jibu na ndio maana nikaona niombe msaada wenu wanaJF ili mnielimishe kama siku nyingine nifanyeje ikitokea hali kama hiyo maana naona kama haki yetu abiria ilikuwa inadhurumiwa tu. NISAIDIENI!