Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 359,869
- 828,378
Truth and reconciliation... Ukweli na maridhiano huletwa na haki na wajibu baada ya hapo ndio hupata matokeo ya tunda la amani
Kuna kitu tunakilazimisha kifanyike hata kama hakiwezekani kabisa! Tumepanda magugupori lakini tunataka tuvune mahindi mtama na uwele
Tumefuga nguchiro na panyabuku lakini tunataka watotoe vifaranga vya kuku au bata
Kwa uchafu wetu tumeruhusu Chawa, kunguni na papasi waweke makazi ya kudumu viungani mwetu, lakini kwa uwendawazimu wa kiwango cha lami tunasema hawa ni sisimizi madu na mende.. Sijui tunatafuta kuvunja rekodi gani ya dunia
Zimebakia siku chache kuumaliza mwaka 2025.. Mwaka ambao hautasaulika kwenye historia ya Tanganyika.. Si kwa mema la hasha, si kwa furaha bali kwa uchungu huzuni na majonzi makubwa, kutokana na ukatili mkubwa uliopelekea kumwaga damu za maelfu ya watanganyika wasio na hatia ndani ya siku tano za giza kati ya October 29 na November 3
Baada ya yote hayo ya kunajisi uumbaji na ardhi, tukaanza kutangaziwa maridhiano na amani huku haki wajibu na ukweli vikitengwa pembeni kabisa! Hiki nacho kinaweza kuwa kituko cha aina yake
Tungeanza na UKWELI kwanza wa nini kilitokea ama kilisababisha yatokee yaliyotokea.. Ukweli huo ungefuatwa na takwimu sahihi na za wazi
Walikufa/uliwa wangapi
Walijeruhiwa wangapi
Walitibwa wangapi na kurusiwa
Wangapi bado wako kwenye matibabu
Wangapi walipata majeraha makubwa
Wangapi walipata ulemavu wa muda
Wangapi walipata ulemavu wa kudumu
Wangapi walipotea na kupatikana wakiwa hai
Wangapi walipotea na kupatikana wakiwa marehemu
Wangapi walipotea na hawakuwahi kupatikana
Baada ya ukweli huo tungefuata WAJIBU.. Nani awajibike kwenye nini kwa yaliyotokea.. Uwajibikaji wa mtu mmoja mmoja na uwajibikaji wa pamoja
Kisha ingefuata HAKI.. haki kwa wote waliodhurika kwa namna moja ama nyingine! Hasa wahanga wa vifo, majeruhi na ulemavu. Bila kusahau familia zilizoathirika kutokana na hayo madhila
Baada ya yote hayo tungetafuta suluhu ya muda mfupi na ya kudumu kwenye meza ya maridhiano.. Hapa sasa amani ingepatikana bila hata ya kutumia nguvu yoyote!
Huu si mchakato wa siku mbili au tatu ni mchakato mrefu na mgumu lakini kwanza NIA NJEMA ingeoneshwa kwa vitendo kwa kutangaza mkeka huu wa kutafuta amani
Hii janja janja inayoendelea ya kutangaza amani huku mengine ya msingi Sana yakifumbiwa macho haitatufikisha popote na badala ya kudhani kwa kufanya hivyo tutafubaza harakati ni kujiongopea kulikopitiliza kwakuwa badala ya kufubaza ndio tutakuwa tunakomaza
Kuna kitu tunakilazimisha kifanyike hata kama hakiwezekani kabisa! Tumepanda magugupori lakini tunataka tuvune mahindi mtama na uwele
Tumefuga nguchiro na panyabuku lakini tunataka watotoe vifaranga vya kuku au bata
Kwa uchafu wetu tumeruhusu Chawa, kunguni na papasi waweke makazi ya kudumu viungani mwetu, lakini kwa uwendawazimu wa kiwango cha lami tunasema hawa ni sisimizi madu na mende.. Sijui tunatafuta kuvunja rekodi gani ya dunia
Zimebakia siku chache kuumaliza mwaka 2025.. Mwaka ambao hautasaulika kwenye historia ya Tanganyika.. Si kwa mema la hasha, si kwa furaha bali kwa uchungu huzuni na majonzi makubwa, kutokana na ukatili mkubwa uliopelekea kumwaga damu za maelfu ya watanganyika wasio na hatia ndani ya siku tano za giza kati ya October 29 na November 3
Baada ya yote hayo ya kunajisi uumbaji na ardhi, tukaanza kutangaziwa maridhiano na amani huku haki wajibu na ukweli vikitengwa pembeni kabisa! Hiki nacho kinaweza kuwa kituko cha aina yake
Tungeanza na UKWELI kwanza wa nini kilitokea ama kilisababisha yatokee yaliyotokea.. Ukweli huo ungefuatwa na takwimu sahihi na za wazi
Walikufa/uliwa wangapi
Walijeruhiwa wangapi
Walitibwa wangapi na kurusiwa
Wangapi bado wako kwenye matibabu
Wangapi walipata majeraha makubwa
Wangapi walipata ulemavu wa muda
Wangapi walipata ulemavu wa kudumu
Wangapi walipotea na kupatikana wakiwa hai
Wangapi walipotea na kupatikana wakiwa marehemu
Wangapi walipotea na hawakuwahi kupatikana
Baada ya ukweli huo tungefuata WAJIBU.. Nani awajibike kwenye nini kwa yaliyotokea.. Uwajibikaji wa mtu mmoja mmoja na uwajibikaji wa pamoja
Kisha ingefuata HAKI.. haki kwa wote waliodhurika kwa namna moja ama nyingine! Hasa wahanga wa vifo, majeruhi na ulemavu. Bila kusahau familia zilizoathirika kutokana na hayo madhila
Baada ya yote hayo tungetafuta suluhu ya muda mfupi na ya kudumu kwenye meza ya maridhiano.. Hapa sasa amani ingepatikana bila hata ya kutumia nguvu yoyote!
Huu si mchakato wa siku mbili au tatu ni mchakato mrefu na mgumu lakini kwanza NIA NJEMA ingeoneshwa kwa vitendo kwa kutangaza mkeka huu wa kutafuta amani
Hii janja janja inayoendelea ya kutangaza amani huku mengine ya msingi Sana yakifumbiwa macho haitatufikisha popote na badala ya kudhani kwa kufanya hivyo tutafubaza harakati ni kujiongopea kulikopitiliza kwakuwa badala ya kufubaza ndio tutakuwa tunakomaza