Haji Manara: Simba imerudi nyuma miaka 100, alia na Malinzi

Opera Min

JF-Expert Member
Nov 28, 2013
901
657
1503125682844.png
Akiongea na Kipindi cha 360 Saturday cha clouds Tv Afisa habari wa Simba Haji Manara amesema Licha ya Simba kuwa ndio taasisi kubwa na maarufu kwa sasa Tanzania nzima kuliko taasisi yoyote ile,imerudi nyuma miaka 100 kwa kuendeshwa kienyeji kwa mfumo wa kutegemea ada za wanachama.
"Kwa sasa Simba inaendelea na semina ya ueledi kwa wanachama wake kubadili mfumo wa uendeshaji wa klabu kutoka mfumo wa uanachama kwenda mfumo wa hisa"

Akifafanua kwa mifano amesema Simba iliyotimiza miaka 81 mwaka huu ina idadi ya wanachama wapatao zaidi ya Elfu Nane ambao wanatakiwa kulipa ada ya shilingi Shilingi Elfu Moja kwa Mwezi sawa na Shilingi Elfu kumi na mbili kwa mwaka lakini wengi wao hawalipi ada.Aliongeza kwa kusema hata kwenye klabu ya yanga,vyama vya Siasa hali ni hiyo hiyo wanachama ni wagumu kilipa ada

Akiongelea faida ya mfumo wa hisa amefafanua Simba itanufaika kwa mgawanyo wa asilimia 50 kwa 50,ambapo Asilimia Tisa itarudishwa kwa wanachama hai,Asilimia Moja kwa waasisi wa klabu na Asilimia Arobaini itabaki klabuni kwa ajili ya uendeshaji wa timu.

Hata hivyo Alipingwa na kukosolewa vikali na bwana Issa Masoud mdau wa Simba na Mtaalam wa mambo ya fedha aliyebobea kwenye maswala ya hisa kwamba mfumo wa hisa ni mgumu kwa klabu kwani unahitaji kuibadilisha Simba iendeshwe kimfumo wa kampuni,Bwana Issa alisema kunahitajika juhudi ya kuwashirikisha wanachama wajadiliane na kukubaliana upi mfumo bora utumike kuiendesha klabu na sio kuwadikteti wanachama wakubali tu kuipeleka Simba kwenye mfumo ambao mbeleni unaweza ukaleta Matatizo makubwa.

Akijibu swali lililoulizwa na moja ya mtazamaji wa kipindi hicho "kwa nini kila mwaka Manara anajigamba kuchukua ubingwa lakini wanaangukia pua?" Manara alijibu kwa kumshutumu vikali aliyekuwa Rais wa TFF Jamali Mlinzi kuwadhulumu Ubingwa na kuwapangia Ratiba ngumu na Waamuzi wa hovyo kwa lengo la kuwakwamisha Simba.Malinzi kwa sasa yuko Rumande akishikiliwa kwa kesi ya Matumizi mabaya ya Ofisi.
 
Hivi Manara sio huyu aliye furahi kabla ligi haija anza kuwa wanachukua Kombe...

Wakati msimu 2016-2017 huyu huyu alifurahi sana ratiba ilivyo walianza kuvheza mechi 5 mfululizo Home mzunguo wa walibuna alama nyingi sana kana kwamba Simba inachukua kombe ila mzunguko wa pili walishindwa kuhimili miki miki ya ligi...

Timu ilikuwa inacheza vizuri ila ufungaji hamna kitu..Sasa atasemaje ni Malinzi MCHAWI WA SIMBA hayupo mbali saa ni OMOG tu...MAYANJA yupo vizuri sana anajua na wakidhubutu kumtoa Mayanja Simba hamna kitu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Polite request:

Simba mtoeni Manara kwenye usemaji wa timu yenu, tunashindwa kumjibu kwa hali yake aliyonayo, wekeni mtu mwingine tuwe huru kumjibu pale anapotugusa.
 
Hivi Manara sio huyu aliye furahi kabla ligi haija anza kuwa wanachukua Kombe...

Wakati msimu 2016-2017 huyu huyu alifurahi sana ratiba ilivyo walianza kuvheza mechi 5 mfululizo Home mzunguo wa walibuna alama nyingi sana kana kwamba Simba inachukua kombe ila mzunguko wa pili walishindwa kuhimili miki miki ya ligi...

Timu ilikuwa inacheza vizuri ila ufungaji hamna kitu..Sasa atasemaje ni Malinzi MCHAWI WA SIMBA hayupo mbali saa ni OMOG tu...MAYANJA yupo vizuri sana anajua na wakidhubutu kumtoa Mayanja Simba hamna kitu

Sent using Jamii Forums mobile app
Hawa wanaojiita wasemaji wa timu ni shda.wakifungwa Mara refa Mara tff.shida 2pu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio pekee ako watu wengi wanamuacha Manara aropoke bila kumjibu kwa sababu kama yako.
Tatizo lenu badala mumshambulie kwa maneno mnaanza kumu attack personally ,mbona muro alikuwa anamsema sana manara na ilikuwa poa tu ila siku alipoenda mbali kumu attack kwa personal yake ndio alilaumiwa

Na kuanza kushambuliana kwa muonekano ni ujuha ,tanianeni na bishaneni kikawaida
 
Manara amezungumza hoja zake kutokana na maono yake mnashindwa kuzivunja kwa kisingizio cha maumbile yake. Shameful
 
Back
Top Bottom