"halow mama!"
"halow Frank hujambo?"
"sijambo shikamoo!"
"marahaba mbona hukuniambia kama jana umefika saa ngapi na je umefika salama ukanyamaza tu?"
"mambo yalikuwa mengi mengi mama basi lililala njiani na simu ikazima basi mambo vurururu vururu lakini leo nilipanga hapa niweke vocha nikutafute mama!"
"pole baba yako vipi hajambo huko?"
"hajambo kabisa!"
"uwe unampikia pikia si unajua kuwa anaishi mwenyewe tu asile sile mavyakula ya kwenye migahawa migahawa kila siku siyo mazuri sawa?" mama aliniambia nikaguna tu, nikitamani hata nimwambie bimkubwa wangu huyo kinachoendelea lakini ikabidi nijipige tu kifua
"sawa mama nitafanya hivyo!"
"haya nina dakika chache zimebaki ngoja nimpigie baba yako yupo au kaenda kazini?"
"ameondoka!"
"sawa!" mama alikata simu nami nikashusha pumzi ndefu na kuitupa simu hiyo kitandani nikajiinamia huku nikijikuna kichwa changu
Upande mwingine kichwa changu kilishavurugwa, yaani namaanisha akili, nilikuwa tayari nimeshakuwa mlevi kwa mwanamama huyo, Penina, mchepuko wa baba, mahaba yake yaliniingia kisawa sawa mpaka kwenye mishipa ya damu, nikiwa tayari na mzio (addicted) wa mapenzi yake, lakini wasiwasi wangu mkubwa ukiwa kwanini ile meseji, kuna nini nyuma ya mahaba anayonipa, tena mimi na baba mpaka, kuna ajenda gani hizo zinazoonekana kama za kishirikina shirikina hivi
Nikainuka nikiwa nimevaa bukta tayari na vest juu nikatoka chumbani na ndipo nilipomsikia akiongea kwa simu kwa mbali sana chumbani kwake mlango akiwa ameurudisha, nikakishika taratibu kitasa cha mlango huo usio na kelele nikamkuta amekaa kitako kitandani akiwa amejifunga kitenge akiwa hajaniona akiendelea kuzungumza na simu
"ni kweli nia yangu ilikuwa hiyo kama nilivyopewa masharti na mganga lakini shosti nimekwama mwenzako kwa huyu mtoto wa huyu baba, nainjoi sana hayo maswala ya biashara sijui nini yapotelee mbali tu wala sitaki tena, hapa asubuhi asubuhi nimetoka kupewa mahaba moto moto mpaka nyonga zote hazina kazi navyokwambia, kijana anayajua mahaba mwenzangu halafu ana sura nzuri, mrefu na huko ndani ya suruali ndo nisiongee dude dude sijui inchi kumi maana mh likizamaga huku kwa bibi karibia liguse tumbo la uzazi" mwanamama huyo aliongea na ndipo nilipourudisha mlango wake na wakati huohuo nikasikia mlango wa sebuleni ukigongwa
"hodi hodi!" ilikuwa ni sauti ya mwanamke
"karibu!" niliufuata mlango huo na kuufungua na kukutana na sura ambayo haikuwa ngeni machoni mwangu
"wewe??!!!" mwanamama huyo alinishangaa, alikuwa ni yule tuliyesafiri nae kwenye basi wakati nakuja, ambae alinipa mtoto nimshikie mtoto wake akanikojolea kwenye suruali
Kama mnamkumbuka niambieni anaitwa mama nani???!!!
"Unaishi hapa kumbe?"
"ndiyo"
"kha jamani hapa kwa rafiki yangu wa damu yani kufa na kuzikana, Penina, ni nani yako mbona nakujaga hapa sijawahi kukuona?!"
"ni mama yangu"
"mama yako, mh Penina huyu huyu awe na mtoto mkubwa kijana wa kuoa kabisa kama wewe kwa umri wake ule halafu anifiche tu asiniambie inawezekanaje wezekanaje kwa mfano?"
"ni mtoto wa mume wangu kaja tu jana!" mwanamama Penina alijibu, maana alikuwa ameshatoka chumbani kwake mara baada ya kusikia maongezi yetu kati yangu na mwanamama huyo mgeni wake
"ooh Penina shoga yangu nimekumisije!" mwanamama huyo ambae alifanana tu umbile na mwanamama Penina, alimkumbatia, akiwa amevaa kigauni kifupi kilichombana na kumshika mwilini, akiwa na mitak** mikubwa iliyomzidi hata mwanamama Penina mwenyewe
"mbona unakuja ghafla ghafla bila kuniambia Diana?" mama yangu huyo wa kambo alimwuliza rafiki yake huyo akionekana kutomchangamkia sana
"tangu lini mimi nikaja kwako kwa taarifa mambo hayo yameanza lini mbona kama hujafurahia kuniona au hutaki zawadi nilizokuletea eeh?" mama huyo alimwuliza huku akigeuka kunitazama mimi