Mwachiluwi
JF-Expert Member
- Mar 10, 2022
- 17,796
- 32,148
MAMA WA KAMBO*
*SEHEMU YA 01
Mpyaa
Basi lilianza safari ya kuelekea jijini Dar es Salaam nami nikiwa mmoja wa abiria tuliokuwa tumepanda, ikiwa ni safari yangu siyo ya mara ya kwanza kabisa kuelekea kwenye jiji hilo la kibiashara lenye kila aina ya starehe na maisha ya watu mchanganyiko kutoka kila kabila na kila mkoa, maana niliwahi kusoma kwenye jiji hilo shule ya bweni ya sekondari binafsi kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha nne mpaka nilipohamishiwa mkoani kwenye shule ya vipaji maalumu baada ya kuwa na ufaulu wa juu, hivyo jiji la Dar es Salaam nalijua ingawa siyo kwa sehemu kubwa maana nilikuwa natumia muda mwingi shuleni kutoka ilikuwa ni mara chache na kwa kibali maalumu au wakati mwingine ni kwa kutoroka tu
Nikiwa ndani ya basi ilibidi nimpigie baba ambae ndiye mwenyeji wangu ninayemtegemea jijini Dar es Salaam akiwa ni mtumishi katika ofisi moja ya serikali huku mama yangu akiwa ni mfanyakazi kwenye shirika moja la wakimbizi akiwa ni mtu wa kuhama hama mara nyingi kwenye vituo vya kazi
Simu ya baba iliita kwa sekunde kadhaa bila kupokelewa mpaka ikakata, nikajaribu kuipiga tena ikaita na safari hii ikapokelewa
"halow??!" sauti ilikuwa ya kike
"halow habari yako?"
"salama nani?"
"mimi ni Frank!"
"ooh Frank mwanangu??!!" mwanamke huyo aliongea nikashtuka kidogo
"ina maana baba anaishi na mwanamke mwingine?" nilijiuliza kimoyo moyo maana baba hakuwa ameachana na mama, ni mwaka huu tu baba amehamishiwa kikazi jijini Dar es Salaam lakini hapo awali alikuwa anaishi na mama wote mkoani
"Frank mwanangu??" aliuliza tena
"eeh shikamoo naongea na nani samahani maana namba hii niliyopiga ni ya baba?"
"mimi mama yako baba yako amesahau simu leo badala ya kuchukua ya kwake kajisahau kachukua yangu!"
"ooh sa...wa nilitaka kumwambia tu kuwa nipo kwenye basi njiani nakuja!"
"ooh karibu sana sana nitakuja kukupokea mimi baba yako yupo kazini utakapofika stendi kuu ya mabasi utaniambia sawa?"
"sawa!" nilimjibu nikakata simu nikishangaa tu na kubaki kinywa wazi
"mdogo wangu huendi kula?" mama mmoja jirani niliyekaa nae kiti kimoja akiwa na mtoto aliniuliza baada ya gari kusimama kwenye kituo cha kupata chakula
"hapana siwezagi kula njiani, nimetoka nimepiga supu kabisa!"
"ooh basi samahani nahitaji msaada wako kidogo"
"bila samahani!"
"unaweza kunisaidia kidogo kunishikia mtoto wangu nataka nikachimbe dawa kidogo?"
"haina shida!" nilimjibu mwanamama huyo ambae alinipa mtoto wake huyo wa mwaka mmoja hivi na miezi kadhaa, nikamnyanyua, nae akainuka taratibu huku akilishusha shusha gauni lake lililopanda juu na kuliweka vizuri akatoka kwenye kiti kuelekea nje maana gari lilisimama kila mtu hasa wanaume wakimkodolea macho mama huyo ambae alikuwa mnene na nyuma ana mitak** mikubwa kwelikweli mpaka kutembea anapata tabu, mimi nikabaki na mtoto wake wa kike niliyempakata
Baada ya dakika kama kumi gari likiwa limesimama kwenye sehemu ya wa watu kupata chakula mwanamama huyo akarudi ndani ya gari akiwa na vifurushi vya chakula
"karibu!"
"asante endelea tu!"
"sipendi hebu chukua!" alinilazimisha mpaka nikachukua chakula alichoninunulia
"asante sana!" aliniambia na ni kweli nilipojitazama kwenye suruali nilikuwa nimelowa chapa mwenyewe nikiwa sina hata habari
"oohooo!!" ilibidi tu nicheke
"Careen kwa nini umemkojolea anko, hujui kuongea kama yamebanwa, nakuchapa leo!?"
"wala usimchape mrembo wangu kajisahau tu!"
"ana makusudi huyu anaongea sana ngoja nikufute fute kaka yangu!" alitoa khanga
"acha tu!" niliipokea khanga na kujifuta futa mwenyewe akiendelea kumsema sema bintiye mpaka usingizi ulipowashika wote, mwanamama huyo akalala
Gari liliendelea kuchanja mbuga mpaka saa nne za usiku na mwanamama huyu mama Careen akanilalia begani akiwa usingizini nikataka kumshika nimsogeze lakini ikashinidikana ikabidi nimuache tu jioni ikiwa imeingia, akaaniwekea mkono wake kwenye suruali yangu kwenye zipu akiendelea kuuchapa usingizi tu, ikabidi niutoe taratibu na kuurudisha mahali pake
*SEHEMU YA 01
Mpyaa
Basi lilianza safari ya kuelekea jijini Dar es Salaam nami nikiwa mmoja wa abiria tuliokuwa tumepanda, ikiwa ni safari yangu siyo ya mara ya kwanza kabisa kuelekea kwenye jiji hilo la kibiashara lenye kila aina ya starehe na maisha ya watu mchanganyiko kutoka kila kabila na kila mkoa, maana niliwahi kusoma kwenye jiji hilo shule ya bweni ya sekondari binafsi kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha nne mpaka nilipohamishiwa mkoani kwenye shule ya vipaji maalumu baada ya kuwa na ufaulu wa juu, hivyo jiji la Dar es Salaam nalijua ingawa siyo kwa sehemu kubwa maana nilikuwa natumia muda mwingi shuleni kutoka ilikuwa ni mara chache na kwa kibali maalumu au wakati mwingine ni kwa kutoroka tu
Nikiwa ndani ya basi ilibidi nimpigie baba ambae ndiye mwenyeji wangu ninayemtegemea jijini Dar es Salaam akiwa ni mtumishi katika ofisi moja ya serikali huku mama yangu akiwa ni mfanyakazi kwenye shirika moja la wakimbizi akiwa ni mtu wa kuhama hama mara nyingi kwenye vituo vya kazi
Simu ya baba iliita kwa sekunde kadhaa bila kupokelewa mpaka ikakata, nikajaribu kuipiga tena ikaita na safari hii ikapokelewa
"halow??!" sauti ilikuwa ya kike
"halow habari yako?"
"salama nani?"
"mimi ni Frank!"
"ooh Frank mwanangu??!!" mwanamke huyo aliongea nikashtuka kidogo
"ina maana baba anaishi na mwanamke mwingine?" nilijiuliza kimoyo moyo maana baba hakuwa ameachana na mama, ni mwaka huu tu baba amehamishiwa kikazi jijini Dar es Salaam lakini hapo awali alikuwa anaishi na mama wote mkoani
"Frank mwanangu??" aliuliza tena
"eeh shikamoo naongea na nani samahani maana namba hii niliyopiga ni ya baba?"
"mimi mama yako baba yako amesahau simu leo badala ya kuchukua ya kwake kajisahau kachukua yangu!"
"ooh sa...wa nilitaka kumwambia tu kuwa nipo kwenye basi njiani nakuja!"
"ooh karibu sana sana nitakuja kukupokea mimi baba yako yupo kazini utakapofika stendi kuu ya mabasi utaniambia sawa?"
"sawa!" nilimjibu nikakata simu nikishangaa tu na kubaki kinywa wazi
"mdogo wangu huendi kula?" mama mmoja jirani niliyekaa nae kiti kimoja akiwa na mtoto aliniuliza baada ya gari kusimama kwenye kituo cha kupata chakula
"hapana siwezagi kula njiani, nimetoka nimepiga supu kabisa!"
"ooh basi samahani nahitaji msaada wako kidogo"
"bila samahani!"
"unaweza kunisaidia kidogo kunishikia mtoto wangu nataka nikachimbe dawa kidogo?"
"haina shida!" nilimjibu mwanamama huyo ambae alinipa mtoto wake huyo wa mwaka mmoja hivi na miezi kadhaa, nikamnyanyua, nae akainuka taratibu huku akilishusha shusha gauni lake lililopanda juu na kuliweka vizuri akatoka kwenye kiti kuelekea nje maana gari lilisimama kila mtu hasa wanaume wakimkodolea macho mama huyo ambae alikuwa mnene na nyuma ana mitak** mikubwa kwelikweli mpaka kutembea anapata tabu, mimi nikabaki na mtoto wake wa kike niliyempakata
Baada ya dakika kama kumi gari likiwa limesimama kwenye sehemu ya wa watu kupata chakula mwanamama huyo akarudi ndani ya gari akiwa na vifurushi vya chakula
"karibu!"
"asante endelea tu!"
"sipendi hebu chukua!" alinilazimisha mpaka nikachukua chakula alichoninunulia
"asante sana!" aliniambia na ni kweli nilipojitazama kwenye suruali nilikuwa nimelowa chapa mwenyewe nikiwa sina hata habari
"oohooo!!" ilibidi tu nicheke
"Careen kwa nini umemkojolea anko, hujui kuongea kama yamebanwa, nakuchapa leo!?"
"wala usimchape mrembo wangu kajisahau tu!"
"ana makusudi huyu anaongea sana ngoja nikufute fute kaka yangu!" alitoa khanga
"acha tu!" niliipokea khanga na kujifuta futa mwenyewe akiendelea kumsema sema bintiye mpaka usingizi ulipowashika wote, mwanamama huyo akalala
Gari liliendelea kuchanja mbuga mpaka saa nne za usiku na mwanamama huyu mama Careen akanilalia begani akiwa usingizini nikataka kumshika nimsogeze lakini ikashinidikana ikabidi nimuache tu jioni ikiwa imeingia, akaaniwekea mkono wake kwenye suruali yangu kwenye zipu akiendelea kuuchapa usingizi tu, ikabidi niutoe taratibu na kuurudisha mahali pake