Hadithi ya kusisimua- Mimba ya Jini

Hadithi ya kusisimuwa mimba ya jini-15-

ILIPOISHIA:
Hakika Shehna alikuwa mrembo wa warembo.
“Haki ya nani Shehna sijakuita,” Mustafa alijitetea kwa kuamini toka aachane naye hakumpigia simu wala kuonana naye.
“Huna kitu unachotaka kuniuliza?” Shehna alimuuliza huku amemkazia macho yaliyozidisha uzuri wake.
SASA ENDELEA...“

Ninacho lakini nilijua tutaonana jioni.”
“Sawa angeniuliza jioni lakini toka ufike una muda gani?”
“Zaidi ya saa nzima.”
“Umeishafanya kazi gani?”
“Bado sijaanza.”
“Kwa nini?”
“Sina kazi nyingi ningefanya wakati wowote.”
“Kwa hiyo Mustafa unataka kunidanganya hata mimi?”
“Kwa nini unasema hivyo?”
“Mustafa toka uingie kuna vitu vinakutatiza na kujikuta muda mwingi ukijiuliza maswali mengi ambayo unaamini mwenye majibu yake ni mimi, uongo?”
“Kweli.”
“Haya niulize.”
“Kwa nini tusizungumze jioni kwa vile huu ni muda wa kazi!”
“Mustafa mi si mjinga kuacha kazi zangu na kuja kukusikiliza, najua leo huwezi kufanya kazi mpaka upatiwe majibu ya maswali yako.”
“Umejuaje nataka kukuuliza?”
“Mustafa muhimu kwa muda huu kujua nimejuaje au kukujibu maswali yako.”
“Samahani Shehna.”
“Mustafa kama nisingekuwa mimi usingemruhusu mtu kuingia ndani, uongo kweli?”
“Kwa baadaye lazima ningewaruhusu.”
“Kwa hiyo niondoke?”
“Ha...hapana.”
“Unajua kuna kitu kimenifurahisha sana leo ambacho nimepanga kukuzawadia, lakini unataka kuniudhi.”
“Shehna samahani kama nitakukosea lakini naamini wewe ni mtu muhimu sana kwangu.”
“Ndiyo maana nipo hapa.”
“Kuna mengi ya kukuuliza nashindwa nianze na lipi.”
“La mkeo.”
“Umejuaje?”
“Mustafa acha kuwa mgeni wa dunia kushtuka kila kitu, uliza ili ujibiwe si kujua nimejuaje.”
Mustafa alizidi kumshangaa Shehna kuyajua yaliyojificha moyoni mwake, alijiuliza yeye ni kiumbe wa aina gani mwenye uwezo wa ajabu kama ule? Hakuwa na jinsi alimueleza aliyoelezwa na mkewe juu ya kumuomba msamaha kwa yote yaliyotokea.
“Mustafa nimemsamehe kwa vile nakupenda lakini mkeo ana kiburi, masharti mengi amekuwa akiyavunja matokeo yake mnatumia fedha nyingi na nguvu nyingi bila mafanikio.”
“Sasa utanisaidiaje?”
“Unataka msaada wangu upi?”
“Bado tunataka mtoto.”
“Mmechelewa.”
“Kivipi?’
“Unakumbuka nilikuambia nini?”
“Vitu vingi, kimoja wapo?”
“Kuhusu kupata mtoto.”
“Si ulisema utanipa mimi kwanza ndipo nikupe wewe.”
“Ni kweli, lakini makosa ya mkeo yamefanya mambo yabadilike.”
“Kivipi?”
“Zoezi la mimi kupata mtoto nimelianza usiku wa leo.”
“
Sasa tatizo nini?”
“Tatizo hatuwezi kushea watu wawili kupata mtoto kwa vile wewe sasa hivi una mbegu moja baada ya mkeo kuiharibu ya kwanza iliyokuwa yake.”
“Mmh! Kwa hiyo unataka kuniambia na wewe mjamzito sasa?”
“Hapana.”
“Kwa nini hukupata wakati dawa unaijua?”
“Mimi ni tofauti na mkeo lazima nilale na wewe mwezi mzima mfululizo, tukiacha hata siku moja tumeharibu dozi na muda huo wote usikutane na mkeo.”
“Dah! Itawezekanaje nilale mwezi mzima na mke wangu bila kukutana naye, akinitaka nitafanyaje?”
“Wala usihofu hawezi kukugusa mpaka mwezi uishe.”
“Mmh! Sawa.”
“Nina imani swali moja nimekujibu uliza lingine.”
“Nafikiri hili ndilo la muhimu mengine siyo muhimu sana.”
“Mustafa yote muhimu, nipo hapa kukufanya uwe huru na kuondoa wasiwasi wote.”


Itaendelea Kesho wakati kama huu.
 
[h=2]Hadithi ya kusisimuwa: Mimba ya jini-16-[/h]

ILIPOISHIA:
"Wala usihofu, hawezi kukugusa mpaka mwezi uishe."
"Mmh! Sawa."
"Nina imani swali moja nimekujibu uliza lingine."
"Nafikiri hili ndilo la muhimu, mengine siyo muhimu sana."
"Mustafa yote muhimu, nipo hapa kukufanya uwe huru na kuondoa wasiwasi wote."
ENDELEA…


"Mmh! Anyway, hivi Shehna tulionana wapi kabla na kipi kilichokuvutia kwangu kupelekea kutaka kuzaa na mimi na kuwaacha wanaume wengi wasio na wanawake?"

Shehna kabla ya kujibu alicheka kidogo kisha alitabasamu huku aibu ya kike ikimtawala na kuanza kuchezea kucha na kupeleka vidole mdomoni. Mustafa alitumia muda ule kuusanifu uzuri wa Shehna na kushangaa aibu iliyompata kutokana na swali lake.
"Shehna kama swali langu limekuudhi naomba unisamehe, naweza kubadili swali," Mustafa alijihami.
"Hapana, sivyo hivyo swali lako lazima nilijibu kwa vile nipo hapa kwa ajili ya kuondoa wasiwasi wa moyo wako. Mustafa huwezi kuamini nimekupenda muda mrefu sana hata kabla ya kuwa na Husna.
"Mapenzi yangu hayajaanza leo ni muda mrefu nimekuwa nakupenda. Katika maisha yangu nilitamani uwe mume wangu lakini kuna vikwanzo ambavyo vilisababisha nichelewe kukueleza ukweli wa moyo wangu.
"Bahati nilipata safari ya ghafla na kuondoka bila kukueleza dhamira yangu ungeweza kunisubiri. Niliporudi nilikuta tayari umeoa lakini sikuwa na jinsi zaidi ya kutaka hata nipate angalau ukumbusho wa sura yako, ndiyo maana nikataka kuzaa na wewe.
"Wakati napanga hivyo, niligundua una maumivu moyoni mwako kutokana na kuchelewa kupata mtoto. Baada ya kufanya uchunguzi, ilionesha umepoteza fedha nyingi kwenda kwa waganga bila mafanikio. Niliamini nikitatua tatizo ambalo limekunyima furaha, utakuwa tayari kunisikiliza na mimi shida yangu.
"Ndipo nilipokutafuta kwa njia ya simu na kukupa maelekezo ambayo mwenyewe uliona maajabu lakini kiburi cha mkeo kikaharibu kila kitu.
"Kwa vile nilipanga baada ya wewe kupata mtoto ndipo na mimi nipate wangu, basi baada ya mkeo kuvuruga ratiba, itabidi unipe kwanza mimi ujautito ndipo nikupe dawa ya kutafuta mtoto mwingine ambayo mkeo anatakiwa kuwa makini kosa lingine litamfanya awe tasa, hatazaa mpaka anakufa.
"Mustafa kama nilivyokueleza mapenzi yangu kwako hayakuanza leo bali muda mrefu, tumeonana sehemu nyingi lakini inaonesha umenisahau. Unakumbuka siku moja tulikutana ukitoka kufanya usaili ambapo ulikuwa mnyonge baada ya kujua amefanya vibaya.
"Nilikueleza kuwa pamoja na kufanya vibaya lazima jina lako litachaguliwa kati ya matano na kubakishwa jijini Dar. Najua ulishangaa lakini baada ya muda, ilitokea kama nilivyokueleza. Unakumbuka ulikutana na nani akakueleza habari zile?"
Maneno yale yalimfanya Mustafa ashtuke na kurudisha kumbukumbu nyuma miaka nane iliyopita. Siku aliyokwenda kufanya usaili wa kazi ambako walitakiwa watu watano katika watu mia moja waliokuwepo. Katika watu waliofanya vibaya katika usaili ule yeye alikuwa mmoja wapo, katika maswali kumi aliyoulizwa alijibu matatu hata nusu hakufika.
Hata waliokuwa wakiwafanyia usaili, walimkatisha tamaa baada ya kumweleza hakuweza kufika nusu tofauti na wenzake zaidi ya sabini waliotangulia. Aliondoka akiwa hana matumaini.
Lakini alipotoka nje ya ofisi ili aelekee nyumbani, aliitwa na msichana aliyekuwa amevaa hijabu iliyomziba mwili mzima na kuonekana macho.
"Mustafa."
"Naam," aligeuka kumtazama aliyeonekana anamfahamu, hakuweza kumuona uso zaidi ya macho.
"Pole."
"Ya nini?"
"Ya kufanya vibaya.'
‘Umejuaje?"
"Mbona umeniangusha kwa nini umeshindwa kujibu maswali yale mepesi?"
"Yaani hata sijui."
Yule msichana aliyarudia maswali yale na kumuuliza:
"Sasa hapa swali gani gumu?"
"Yaani hata mimi nashangaa, basi tena nitajaribu sehemu nyingine."
"Mbona umekata tamaa mapema?"
"Kama nimefanya vibaya huku zaidi ya watu sabini wamefanya vizuri huku nafasi tano tu zinatakiwa, kuna nini hapo?"
"Usiwe na wasiwasi katika hizo nafasi tano, wewe utakuwemo na ndiye utakayebakia Dar."
"Wewe nani?"
"Mustafa shida yako kujua mimi nani au wewe kupata kazi na kuteuliwa kubakia Dar?"
"Shida yangu kupata kazi."
"Basi subiri muda ufike."
"Nitajuaje?"
"Utapigiwa simu."
"Wataijuaje namba yangu ya simu wakati hawakuchukua kwa vile ni mmoja ya watu waliofanya vibaya."
"Namba yako nitawapa."
"Namba yangu umeipata wapi?"
"Mustafa hujawahi kuigawa namba yako?"
"Nimegawa basi nitashukuru japokuwa najua hakuna kitu."
"Siku tukikutana utaniambia."


Itaendelea kesho wakati kama huu.
 
!
!
imeishia kati jamani kuna nini tena jamani.....................inaendelea wapi hiyo sehemu ya 17




Hadithi ya kusisimuwa: Mimba ya jini-16-



ILIPOISHIA:
"Wala usihofu, hawezi kukugusa mpaka mwezi uishe."
"Mmh! Sawa."
"Nina imani swali moja nimekujibu uliza lingine."
"Nafikiri hili ndilo la muhimu, mengine siyo muhimu sana."
"Mustafa yote muhimu, nipo hapa kukufanya uwe huru na kuondoa wasiwasi wote."
ENDELEA…


"Mmh! Anyway, hivi Shehna tulionana wapi kabla na kipi kilichokuvutia kwangu kupelekea kutaka kuzaa na mimi na kuwaacha wanaume wengi wasio na wanawake?"

Shehna kabla ya kujibu alicheka kidogo kisha alitabasamu huku aibu ya kike ikimtawala na kuanza kuchezea kucha na kupeleka vidole mdomoni. Mustafa alitumia muda ule kuusanifu uzuri wa Shehna na kushangaa aibu iliyompata kutokana na swali lake.
"Shehna kama swali langu limekuudhi naomba unisamehe, naweza kubadili swali," Mustafa alijihami.
"Hapana, sivyo hivyo swali lako lazima nilijibu kwa vile nipo hapa kwa ajili ya kuondoa wasiwasi wa moyo wako. Mustafa huwezi kuamini nimekupenda muda mrefu sana hata kabla ya kuwa na Husna.
"Mapenzi yangu hayajaanza leo ni muda mrefu nimekuwa nakupenda. Katika maisha yangu nilitamani uwe mume wangu lakini kuna vikwanzo ambavyo vilisababisha nichelewe kukueleza ukweli wa moyo wangu.
"Bahati nilipata safari ya ghafla na kuondoka bila kukueleza dhamira yangu ungeweza kunisubiri. Niliporudi nilikuta tayari umeoa lakini sikuwa na jinsi zaidi ya kutaka hata nipate angalau ukumbusho wa sura yako, ndiyo maana nikataka kuzaa na wewe.
"Wakati napanga hivyo, niligundua una maumivu moyoni mwako kutokana na kuchelewa kupata mtoto. Baada ya kufanya uchunguzi, ilionesha umepoteza fedha nyingi kwenda kwa waganga bila mafanikio. Niliamini nikitatua tatizo ambalo limekunyima furaha, utakuwa tayari kunisikiliza na mimi shida yangu.
"Ndipo nilipokutafuta kwa njia ya simu na kukupa maelekezo ambayo mwenyewe uliona maajabu lakini kiburi cha mkeo kikaharibu kila kitu.
"Kwa vile nilipanga baada ya wewe kupata mtoto ndipo na mimi nipate wangu, basi baada ya mkeo kuvuruga ratiba, itabidi unipe kwanza mimi ujautito ndipo nikupe dawa ya kutafuta mtoto mwingine ambayo mkeo anatakiwa kuwa makini kosa lingine litamfanya awe tasa, hatazaa mpaka anakufa.
"Mustafa kama nilivyokueleza mapenzi yangu kwako hayakuanza leo bali muda mrefu, tumeonana sehemu nyingi lakini inaonesha umenisahau. Unakumbuka siku moja tulikutana ukitoka kufanya usaili ambapo ulikuwa mnyonge baada ya kujua amefanya vibaya.
"Nilikueleza kuwa pamoja na kufanya vibaya lazima jina lako litachaguliwa kati ya matano na kubakishwa jijini Dar. Najua ulishangaa lakini baada ya muda, ilitokea kama nilivyokueleza. Unakumbuka ulikutana na nani akakueleza habari zile?"
Maneno yale yalimfanya Mustafa ashtuke na kurudisha kumbukumbu nyuma miaka nane iliyopita. Siku aliyokwenda kufanya usaili wa kazi ambako walitakiwa watu watano katika watu mia moja waliokuwepo. Katika watu waliofanya vibaya katika usaili ule yeye alikuwa mmoja wapo, katika maswali kumi aliyoulizwa alijibu matatu hata nusu hakufika.
Hata waliokuwa wakiwafanyia usaili, walimkatisha tamaa baada ya kumweleza hakuweza kufika nusu tofauti na wenzake zaidi ya sabini waliotangulia. Aliondoka akiwa hana matumaini.
Lakini alipotoka nje ya ofisi ili aelekee nyumbani, aliitwa na msichana aliyekuwa amevaa hijabu iliyomziba mwili mzima na kuonekana macho.
"Mustafa."
"Naam," aligeuka kumtazama aliyeonekana anamfahamu, hakuweza kumuona uso zaidi ya macho.
"Pole."
"Ya nini?"
"Ya kufanya vibaya.'
‘Umejuaje?"
"Mbona umeniangusha kwa nini umeshindwa kujibu maswali yale mepesi?"
"Yaani hata sijui."
Yule msichana aliyarudia maswali yale na kumuuliza:
"Sasa hapa swali gani gumu?"
"Yaani hata mimi nashangaa, basi tena nitajaribu sehemu nyingine."
"Mbona umekata tamaa mapema?"
"Kama nimefanya vibaya huku zaidi ya watu sabini wamefanya vizuri huku nafasi tano tu zinatakiwa, kuna nini hapo?"
"Usiwe na wasiwasi katika hizo nafasi tano, wewe utakuwemo na ndiye utakayebakia Dar."
"Wewe nani?"
"Mustafa shida yako kujua mimi nani au wewe kupata kazi na kuteuliwa kubakia Dar?"
"Shida yangu kupata kazi."
"Basi subiri muda ufike."
"Nitajuaje?"
"Utapigiwa simu."
"Wataijuaje namba yangu ya simu wakati hawakuchukua kwa vile ni mmoja ya watu waliofanya vibaya."
"Namba yako nitawapa."
"Namba yangu umeipata wapi?"
"Mustafa hujawahi kuigawa namba yako?"
"Nimegawa basi nitashukuru japokuwa najua hakuna kitu."
"Siku tukikutana utaniambia."


Itaendelea kesho wakati kama huu.
 
Hadithi ya kusisimuwa: Mimba ya jini-17-

ILIPOISHIA JANA:"Namba yako nitawapa."
"Namba yangu umeipata wapi?"
"Mustafa hujawahi kuigawa namba yako?"
"Nimegawa basi nitashukuru japokuwa najua hakuna kitu."
"Siku tukikutana ataniambia."
SASA ENDELEA…

Mustafa aliagana na yule msichana mwenye lafudhi ya mwambao bila kumuuliza jina. Siku moja akiwa hana hili wala lile alipigiwa simu kujulishwa amefanikiwa kupita katika mchujo wa usaili na yeye ndiye aliyefanya vizuri kuliko wote anatakiwa kubakia Dar es Salaam.
Alishtuka sana lakini hakuamini aliona kama watu wanamchezea akili, siku ya pili alikwenda ofisini kujaribu lakini alipotaja jina lake alikabirishwa na kujaza fomu ya kuajiliwa na wiki iliyofuata alianza kazi kwa kupewa ofisi na sekretari pamoja na mshahara mzuri.

Lakini Mustafa alisahau kama kuna mtu alimweleza taarifa kuwa atapita kwenye usaili na atabakia jijini Dar japokuwa alikuwa amefanya vibaya sana.
Furaha ya kupata kazi ilimfanya asitumie muda kuwaza ilikuwaje mpaka kupita na msichana yule alijuaje. Mustafa alitulia na kuvuta kumbukumbu kisha aliteremsha macho kumuangalia Shehna na kuamini kabisa ndiye yeye. Kwa lafudhi aliyoitumia japokuwa alimuona macho tu aliamini kabisa ndiye msichana aliyemtabilia mambo ya ajabu.
"Dah! Kweli."

"Kweli nini?" Shehna alimuuliza akiwa anamtazama usoni.
"Nimekumbuka, hivi ulijuaje mi nitapita wakati nilikuwa najua nimefanya vibaya?"
"Leo siyo siku yakeikifika nitakueleza, mpaka hapo nina imani baadhi ya vitu umevielewa kama una swali niulize."
"Swali lingine nilitaka kujua wewe unakaa wapi katika familia yenu mpo wangapi, kwa sasa unajishughulisha na nini. Wewe ni mganga au nani?"

"Ninapokaa si rahisi kukuelekeza mpaka twende pamoja, katika familia yetu tupo watatu wote wanawake mimi ni mtoto wa mwisho na swali la mwisho mimi si mganga wala mnajimu ila Mungu kanipa uwezo wa kuyajua matatizo ya mwenzangu."
"Kwa nini huwezi kupata ujauzito kwa mara moja kama mke wangu?"
"Dawa ya haraka nilikuwa nayo moja ambayo nilimpa mkeo hii inachelewa, kwa vile nami nina hamu ya mtoto sina jinsi lazima nitumie njia ya muda mrefu."

"Kingine unajua sijawahi kulala nje ya nyumbani kwangu nitafanyaje?"
"Mustafa nyumba ndogo huwa unalala nayo nyumbani kwako?"
"Mmh!" Mustafa aliguna baada ya kujua ameumbuka.
"Najua wasiwasi wako kulala nje ya nyumba yako mwezi mzima, nitalala na wewe mwezi huo mzima nyumbani kwako na kitandani kwako."
"He! Na mke wangu atakuwa wapi?" Mustafa alioshtuka.

"Atakuwepo ndani."
"Siwezi kufanya mapenzi ndani na mke wangu akiwemo itakuwa kumdhalilisha."
"Mustafa naomba unisikilize, wewe kila siku naomba ukilala usiku wakati mnataka kulala hakikisha wewe unakuchelewa kulala usikubali hata siku moja mkeo akukute kitandani.
"Mkeo akiisha lala utaingia bafuni kuoga na kujipaka mafuta nitakayokupa.
Isipande kitandani hakikisha mlango wako umeurudisha bila kuufunga au dirisha ili nikija nisipate tabu ya kuingia.

"Ukiishapanda kitandani usilale na nguo ya ndani kisha hakikisha mkeo analala ukutani wewe lala katikati ya kitanda mimi nikija nitalala mwanzoni mwa kitanda. Mpake mkeo mafuta kichwani kisha lala."
"Mmh! Nitaweza kweli, mbona unanipa mtihani, kwa nini tusiwe tunakutana hotel na tukimaliza haja zetu, narudi nyumbani kulala?"

"Mustafa kutafuta kwangu mtoto natakiwa kupata dozi ya mara tatu kwa usiku mmoja hivyo lazima nilale na wewe."
"Una maanisha dozi ya kivipi."
"Ya saa sita, saa tisa na kumi na moja alfajiri, unaweza kulala nje?"
"Shehna mbona unanipa mtihani mgumu."

"Mbona wako niliuweza wa kwenda kubadili matokeo ya usaili ili upite kama ningekamatwa ningekuwa wapi?" Shehna alimuuliza Mustafa akiwa amemkazia macho huku sura ya uzuri iligeuka kama mzee na kumtisha Mustafa.

Itaendelea Kesho wakati kama huu......
 
Hadithi ya kusisimuwa: Mimba ya jini-18-


ILIPOISHIA:
"Mbona wako niliuweza wa kwenda kubadili matokeo ya usaili ili upite kama ningekamatwa ningekuwa wapi?" Shehna alimuuliza Mustafa akiwa amemkazia macho huku sura ya uzuri iligeuka kama mzee na kumtisha Mustafa.
SASA ENDELEA…


"Mustafa nimejitolea katika mambo yake mengi ambayo wewe huyajui, yaani kwa hili moja umeshindwa. Unakumbuka ulitaka kufukuzwa kazi mimi ndiye niliyerekebisha mahesabu ili ubakie kazini?

Wewe ni mtu gani usiyejiuliza kila kosa lako halionekani?" Shehna alimuuliza huku machozi yakimtoka.
Kauli ile ilimshtua sana Mustafa na kuzidi kumshangaa Shehna na kujiuliza ni kiumbe wa aina gani. Alikumbuka baada ya kupata nyumba ndogo alijikuta akitaka kumfurahisha, alijikuta akifanya ubadhilifu wa fedha kazini kwake.
Taarifa ilifika ofisi kuu na kufanya mahesabu ya ghafla huku akisimamishwa kazi kupisha wafanye mahesabu.
Kitendo kile kilimshtua Mustafa na kujikuta akipandwa na presha na kulazwa hospitali kwa kujua hana kazi na lazima afungwe kwa vile alichota zaidi ya milioni kumi na tano.
Siku ile akiwa hospitali majira ya usiku wa manane aliamshwa na daktari binti mrembo wa Kiarabu aliyekuwa amesimama pembeni ya kitanda chake.
Alikuwa amevalia mavazi ya kidaktari na miwani myeupe nywele zake zilikuwa ndefu na nyeusi. Alikuwa binti mrembo sana, hakuwahi kumuona mwanamke mzuri kama yule katika maisha yake na kumwita jina lake.
"Mustafa."
"Naam."
"Pole sana."
"Asante."
"Tatizo nini?"
"Wanadamu wabaya wamenisingizia nimekula fedha ya kampuni wakati sijala hata senti tano."
"Mustafa kuwa mkweli, fedha umekula. Heri ungeijengea familia yako, wazazi wako wanaishi maisha ya kubahatisha kuliko ulichokifanya kumhonga hawara."
Kauli ile ilimshtua Mustafa na kujiuliza yule daktari amejuaje au kuna mtu alimwambia, ilibidi amuulize amejuaje.
"We umejuaje?"
"Mustafa muhimu si kujua nimejuaje zaidi ya kukusaidia usifukuzwe kazi na kufungwa."
"Utafanyaje?"
"Kazi hiyo niachie mimi," Mustafa alizidi kumshangaa daktari atamsaidia vipi, daktari alitabasamu na kuzitikisa nywele zake ndefu nyeusi zilizoongeza uzuri wake.
"Mustafa bai."
Mustafa siku ya pili aliposhtuka alijua ile ilikuwa ni ndoto kwa vile pale hospitali hakukuwa na daktari wa vile. Lakini ajabu siku iliyofuata alielezwa arudi kazini kila kitu kimekutwa kipo sawa hakukuwa na hasara yoyote kwenye fedha ya kampuni. Japokuwa aliona kama ndoto iliyo na ukweli, hakutaka kushughulika nayo zaidi ya kushukuru kuponea tundu la sindano.
"Mustafa unakumbuka siku hiyo?"
Mustafa baada ya kuvuta kumbukumbu alijikuta akizidi kumshangaa Shehna na kujiuliza ni kiumbe gani aliyekuwa karibu ya matatizo yake muda wote na kujiuliza amekuwa akijuaje na kutokea kumsaidia. Alijiuliza alifanyaje mpaka hesabu zikakutwa zipo sawa wakati alijua tayari hana kazi na jela ilikuwa ikimwita.
Shehna baada ya kumuona Mustafa amehama kimawazo, alimuuliza tena swali lake la awali.
"Mustafa unakumbuka? Au umesahau maana akili yako ina ubongo wa samaki."
"Nakumbuka."
"Uliiba hela hukuiba?"
"Niliiba."
"Unajua kwa nini ulibakia kazini?"
"Sijui."
"Hukujiuliza uliporudishwa kazini wakati ukijua umefanya makosa?"
"Kwa kweli nilipitiwa kwa hilo."
"Mustafa wewe ni mwanadamu gani usiyejiuliza unakwenda kama mnyama?"
"Hata sijui nikuambie nini ili unielewe."
"Inaoneka hata ukipewa kitu hujui kusema asante."
"Shehna ukisema hivyo utanionea, kwa vile mazingira yake yalikuwa kama muujiza au kitu cha ndotoni. Hata wewe baada ya kunifanyia ulitakiwa kujitokeza na kunieleza ili nijue kwa kumshukuru."
"Basi elewa yote hayo niliyafanya kwa ajili yako, kama nilivyokueleza nilipata safari ya ghafla, pia nilitaka kujitokeza muda muafaka kama huu."
"Ulifanyaje?"
"Leo siyo siku yake muhimu ni hili langu, kwa nini hili langu dogo hutaki kunisaidia hujiulizi kuna wanaume wangapi lakini nimekupenda wewe?" Shehna alimuuliza huku machozi yakimtoka na kuyafanya macho yake kuwa mekundu na kuongeza uzuri wake kama njiwa manga.
"Basi nitajitahidi kufanya unavyotaka japokuwa unanipa mtihani mzito."
"Si mtihani kama unavyoona, hebu jaribu leo utaniambia fanya yote niliyokuelekeza kama mkeo atajua basi mimi navunja mapenzi na wewe."
"Shehna sitaki kukupoteza," Mustafa alichangwanywa na uzuri wa Shehna.
"Basi fanya hivyo."
"Nitafanya kwa ajili nakupenda."
Shehna alifurahi na kwenda kumkumbatia Mustafa na kumpiga mabusu.


Itaendelea kesho wakatı kama huu
 
Back
Top Bottom