Hadithi ya kusisimua- Mimba ya Jini

Hadithi ya kusisimua- Mimba ya Jini

Hadithi ya kusisimuwa mimba ya jini-21-

ILIPOISHIA JANA:
Mustafa baada ya kumtafuta Shehna kwa kuzunguka nyumba bila kumuona, alisogea mpaka

mbele ya nyumba labda yupo barabarani lakini hakumuona. Baada ya kutomuona alisimama kwa

muda kujiuliza atafanyaje ikiwa muda umekwenda na lazima akapande kitandani na ilikuwa lazima

ampe mkewe haki yake ya ndoa kwa vile hakuwa na sababu ya kumnyima.

SASA ENDELEA…


Aliamua kurudi ndani akiwa amejikatia tamaa ya kutimiza masharti ya Shehna, alipofika sebuleni alishangaa kukuta hakuna mtu. Alijua labda amekwenda msalani, alibeba Laptop yake na kuingia chumbani, alishangaa kumkuta mkewe chumbani amelala hajitambui.

Alishtuka usingizi wa dakika tano kumkuta mkewe amelala kama mtu aliyelala saa mbili zilizopita wakati anatoka alikuwa macho makavu. Hakuamini, aliona kama anamtania au alifanya vile ili kumtega. Alisogelea kitandani na kumwita mkewe kwa sauti lakini alionesha ana usingizi mwingi hata alivyomgeuza alionesha kweli amelala.
Hakuamini zoezi lake kufanikiwa akiwa amekata tamaa kwa vile naye alikuwa na usingizi. Alichukua chupa ya manukato aliyopewa na Shehna, alikwenda bafuni kuoga na kujipaka nanukato yale.
Kabla ya kupanda kitandani alihakikisha mlango amerudisha bila kufungwa, kisha alipanda kitandani na chupa yake ya manukato. Kwa vile mkewe alikuwa ameisha lala alimsogeza ukutani na yeye kulala katikati. Alifuata maelekezo ya kutolala na nguo ya ndani, alitoa nguo zote na kupanda kitandani akiwa mtupu. Alichukua mafuta kidogo na kumpaka kichwani mkewe ambaye alikuwa katikati ya usingizi mzito.
Naye alijilaza pembeni ya mkewe, haikuchukua muda usingizi ulimpitia. Katikati ya usiku aliamshwa kwa kubembelezwa, alipofumbua macho alimuona Shehna amesimama pembeni ya kitanda akiwa amejifunga mtandio mwepesi ulioonesha mwili wake mzuri uliokuwa hauna kitu ndani.
"Shehna," Mustafa alishtuka na kutaka kuongea kwa sauti.
"Shiiii!" Shehna alimkataza asitoe sauti.
Aliondoa mtandio aliojifunga na kuutupa pembeni kisha alipanda kitandani na kujilaza pembeni kwa Mustafa ambaye alikuwa akitetemeka huku jasho likimtoka, alijiuliza mkewe akiamka na kumkuta mwaname juu ya kitanda chake atamwambia nini. Hali ile Shehna aliiona.

"Mustafa," alimwita kwa sauti ya chini.
"Mmh!" Mustafa alishindwa kutoa sauti.
‘Wasiwasi wako nini?"
"Shehna nakupenda lakini unanitia kwenye matatizo."
"Naomba uniamini hakuna kitu chochote kitakachotokea, mkeo hawezi kuamka mpaka kesho asubuhi."

"Umejuaje?"
"Niamini."
"Sawa," Mustafa alikubali kumridhisha Shehna lakini alitetemeka mpaka utumbo.
Shehna alipomuona Mustafa hayupo naye kimawazo alianza kumpapasa na kulifanya joto lisambae mwili mzima na kujikuta akijisahau kama yupo kwenye kitanda chake na mwisho kuzama kwenye penzi zito ambalo hakuwahi kulipata katika maisha yake.

Shehna pamoja na kuwa mwanamke mrembo pia mapenzi aliyajua kwa kiwango cha hali ya juu. Kama kawaida, Shehna baada ya kupata dozi yake ya mara tatu, aliondoka na kumwacha Mustafa kwenye usingizi mzito.
***
Sara baada ya kuponea tundu la sindano kufukuzwa kazi alijikuta akimchukia Shehna na kumuona ni kiumbe mbaya katika maisha yake. Kabla ya kuja kwake alikuwa akielewana na bosi wake ambaye siku zote alikuwa mpole na mwenye hekima, hakuwahi kumfokea hata siku moja. Lakini toka alipokuja yule mwanamke imekuwa kinyume kabisa.

Alijikuta akikumbuka matukio ya kushangaza toka siku ya kwanza alipoitwa ofisini na Bosi wake kuulizia kama kuna mgeni ameingia ofisini. Tokea hapo amejikuta akikutana na matukio ya ajabu ya kupanda teksi na kujikuta nyumbani na lingine la kulala ofisini kitu ambacho siku za nyuma hakikuwahi kumtokea.
Na tukio la siku ile la kutaka kufukuzwa kazi bila kosa lilizidi kumfanya amchukie sana. Siku ile aliporudi nyumbani alijikuta mwenye hasira nyingi, kila aliyemuona alijua siku ile hayupo vizuri.
Shoga yake wa karibu Happy baada ya kufika nyumbani alimfuata chumbani kumsalimia. Alishangaa kumkuta amekaa kwenye kochi bila kuvua viatu na mkoba wake mkononi huku machozi yakimtoka.

"Shoga vipi mbona hivyo?"
Sara hakumjibu, alichukua kitambaa na kujifuta machozi, hali ile ilimfanya shoga yake adhanie labda amefiwa.


Je, nini kitatokea? Usikose kufuatilia Kesho wakati kama huu......
 
MziziMkavu hii hadithi ina sehemu ngapi? Mbona unaenda kwa kunyata sana? Malizia Boss tuanze kuisoma.
 
Last edited by a moderator:
kwa mtindo huu 2tasahau ilipoanzia bt any way hadith nzur sana ni vile con batani ya kulaiki hapa
 
Hadithi ya kusisimuwa mimba ya jini-22-

ILIPOISHIA JANA:
"Shoga vipi mbona hivyo?"
Sara hakumjibu alichukua kitambaa na kujifuta machozi, hali ile ilimfanya shoga yake awaze labda amefiwa.
SASA ENDELEA…


"Shoga una msiba?"

Alitikisa kichwa kukataa.
"Sasa nini?"
"Naomba kwanza maji," Sara alisema kwa sauti ya kukwaruza.
Shoga yake alikwenda kwenye friji na kuchukua maji kwenye jagi na kumuwekea kwenye glasi. Baada ya kunywa maji kwa mkupuo yaliyopunguza hasira, alishusha pumzi ndefu na kusema.
"Shoga kuna tukio moja leo linimeniudhi sana."
"Tukio gani?"
Sara alimweleza kilichomtokea na kutaka kufukuzwa kazi pamoja na matukio yote yaliyomtokea. Shoga yake alishtuka sana.
"Sara unayosema ni kweli?"
"Kweli kabisa, matukio ya yule mwanamke nina wasiwasi nayo, huenda yule ni jini si mwanamke wa kawaida."
"Mmh! Huenda kweli, lakini si nasikia majini wana kwato kwa chini, uliziona?"
"Yule ni mwanadamu wa kawaida lakini muonekano wake si wa kawaida hata manukato yake sijawahi kuyasikia sehemu yoyote!"
"Mmh! Mungu wangu kama ni jini unafikiri itakuwaje?"
"Dawa yake naijua, nakuapia kama ni jini atakimbia mwenyewe kuna vitu nitakwenda navyo kazini."
"Vitu gani?"
"Mifupa ya nguruwe au nyama yake, kama ni jini hawezi kuja tena ofisini na nitamwambia bosi kama yule si mtu ni jini."
"Basi fanya hivyo."
"Tena shoga nimejikuta nina hamu ya kiti moto, nakwenda kumchukua ili nimlie nyumbani."
"Unachukua kiasi gani?"
"Nusu na ndizi nne nikipiga na bia zangu mbili nalala vizuri."
"Shoga nunua kilo moja maana hata mimi nina hamu nayo sana."
"Poa nitakuchulia na ndizi mbili."
"Hakuna tatizo."
"Yaani kidogo kuzungumza na wewe hasira zimepungua, nakuapia nitamkomesha."
"Kwa kufanya hivyo, utamuweza."
Sara alijitapa huku akivua viatu kisha alibadili nguo na kuelekea bafuni kuoga.
Alipanga akitoka kuoga aende kwenye baa ya Macha iliyokuwa ikiuza kitimoto ili akatimize adhima yake ili ajue kama Shehna ni jini au mtu.
Alioga harakaharaka, alipotoka kuoga alijifuta maji na kujifunga upande wa khanga moja chini na nyingine alijitanda kwa juu. Alichukua noti ya elfu kumi na kutoka kuelekea kwenye baa hiyo.
***
Mustafa aliposhtuka usingizini alijishangaa kujikuta kitandani na mkewe lakini Shehna hakuwepo. Alipoangalia saa ya ukutani ilimuonesha ni saa kumi na moja kasoro alfajiri. Wasiwasi wake ulikuwa labda ameamka na kwenda bafuni kuoga kabla ya kuondoka.
Aliamka haraka kitandani huku akimtazama mkewe asiamke muda ule kabla hajajua Shehna yupo wapi. Alikwenda hadi bafuni lakini hakumkuta mtu akatazama msalani pia hakukuwa na mtu. Alikwenda mlangoni na kukuta umerudishiwa, alijua ameshatoka.
Kwa vile muda ulikuwa bado alirudi kitandani, alipojilaza usingizi ulimchukua mpaka aliposhtuliwa na mkewe kukiwa kumekucha. Alipofumbua macho kulikuwa kumekucha alinyanyuka kuelekea bafuni kuoga, alipotoka kuoga alikuta mkewe ameshamuandalia kifungua kinywa.
Baada ya kufungua kinywa, alimshukuru mkewe kwa kumbusu shavuni na kutaka kuelekea nje lakini mkewe alikumbuka kitu na kumuuliza.
"Mume wangu umefikia wapi?"
"Kuhusu nini?"
"Kuhusu Shehna, bado hujawasiliana naye?"
"Alinipigia na kumueleza, alisema kiburi kimejaa na dharau ndicho chanzo cha kuharibikiwa mambo yako ameapa kama utaendelea na tabia zako chafu utakufa bila mtoto."
"Muongo amejuaje mimi nina tabia chafu?"
Alimweleza kila alichoelezwa na Shehna kilichosababisha ashindwe kushika ujauzito, Husna alichanganyikiwa siri zake zote kuwa nje na kujikuta akitaka kumjua Shehna ni nani, alijiuliza ni kiumbe gani anayejua mambo yake ya siri kiundani ambayo hakuna mtu mwingine aliyekuwa akiyajua. Akiwa bado yupo katika dimbwi la mawazo, Mustafa alimuuliza.
"Lipi la uongo katika niliyokuambia?"
"Mmh! Shehna kiboko, kayajuaje haya?"
"Si kujua kwa nini anajua mambo yako, la muhimu kujua kwa nini natumia fedha na nguvu wakati mwenzangu huna ushirikiano?" Mustafa alizitoa hasira zake kwa mkewe baada ya kuonesha hakuwa na ushirikiano katika kutafuta mtoto.
"La..lakini mume wangu unamuamini vipi Shehna, yule ni mgombanishi tu," Husna alijitetea.
Mara simu ya Mustafa iliita alipoangalia aliiona inatoka kwa Shehna, aliipokea.
"Asalam aleykum."
"Waleykum Salamu, mmeamkaje?"
"Salama."
"Mbona hujatoka kwenda kazini?"
"Si huyu mshe…"


Itaendelea Kesho wakati kama huu....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom