Hadithi: Usife Haraka Mpenzi Wangu

Hadithi: Usife Haraka Mpenzi Wangu

ILIPOISHIA
“Waooo, I can’t beleave my dear, Thanks God thanks Deo I love you soooo much.”
Levina alishangilia kukubaliwa ombi lake na kujisahau kama yupo dukani na kuwashangaza wateja waliokuwa dukani wakisubiri amalize kuzungumza kwa simu.
SASA ENDELEA...

Hata baada ya kumaliza kuzungumza na simu, uso wa Levina ulionesha dhahiri kuwa amezama ndani ya dimbwi la huba. Aliendelea kuchekacheka mwenyewe kama mwendawazimu bila kujali idadi kubwa ya wateja ambao walikuwa wakisubiri kuhudumiwa. Akili yake ilijawa na taswira ya Deo kiasi cha kusahau kazi.

“Oya sista vipi? Tumesimama muda mwingi kusubiri huduma we uko bize na simu tu! Tuhudumie tafadhali!”
Kauli ya mmoja wa wateja waliokuwa wamesimama kusubiri huduma kwenye duka la simu la kina Levina ilimzindua kutoka kwenye mawazo yaliyoiteka akili yake.

Oops! Im sorry, samahani wateja, hii simu imetoka kwa mtu muhimu sana, enhe, ulisema unataka Nokia toleo gani?”
“Nokia 5130c-2!”
“Mimi nakudai chenji yangu, naona simu imekupagawisha kabisa, shemeji nini?”

Levina aliendelea kuwahudumia wateja waliokuwa wakiingia na kutoka kwenye duka lao la simu. Wakati akiendelea na kazi, majibu ya Deo yalikuwa yakiendelea kuzunguka kichwani mwake kama filamu nzuri ya kusisimua.

Wateja walipopungua, alichukua simu yake na kuendelea kuitazama picha ya Deo aliyompiga bila mwenyewe kujijua, akawa anaitazama huku usoni akiwa na bonge la tabasamu! Moto wa penzi la Deo ulikuwa umewaka kikweli ndani ya moyo wake, akawa anasubiri kwa hamu muda wa kufunga duka ufike haraka ili akaonane na Deo, kipenzi cha moyo wake.

***
Kuchanganya mapenzi na kazi ni suala ambalo Deo alikuwa akiliogopa sana. Mara kwa mara alikuwa akijiambia mwenyewe kuwa safari ya kutoka nyumbani kwao Shinyanga hadi Dar es Salaam ilikuwa ni kutafuta maisha, hivyo hakuwa tayari kuona anashindwa kutimiza ndoto zake kwa sababu ya kuchanganya mapenzi na kazi.

Alipofikiria kitakachotokea endapo uhusiano wake na Levina ungegunduliwa na wazazi wa Levina, alijikuta akibatilisha majibu aliyompa Levina siku ile. Alichokiamua ni kutojihusisha kwenye uhusiano wa kimapenzi na Levina, aliamua kuelekeza nguvu na akili zake kwenye kazi.

Saa zilizidi kuyoyoma na hatimaye muda wa Levina kurudi nyumbani ukawa umewadia. Akilini mwake, Levina alikuwa akiwaza namna atakavyomkumbatia na kumkiss Deo mara atakapowasili nyumbani kwao. Alipanga kufanya kila linalowezekana ili kumfanya Deo ampende kama yeye anavyompenda.

Baada ya kufunguliwa geti na kwenda kuegesha gari lake, Levina alishuka akiwa na hamu kubwa ya kuoanana na Deo. Nyumbani kwao hakukuwa na mtu mwingine yeyote zaidi ya mfanyakazi wao na Deo kwani wazazi wake walikuwa bado hawajarejea kutoka kwenye mihangaiko yao.

‘Jamani Deo! Nilikukumbuka sana sweetie, yaani nilikuwa naona saa haziendi,’ aliongea Levina kwa sauti ya kudeka na kumkumbatia Deo kimahaba. Katika hali ambayo hakuitegemea, Levina alishangaa kumuona Deo akikunja sura na kumsukuma pembeni, kisha akaondoka na kuelekea chumbani kwake na kumuacha Levina akiwa bado haamini kile kilichotokea.

“Kwa nini unanitesa Deo, nifanye nini ili uamini kuwa ni kweli nakupenda?” Aliongea Levina huku akimfuata Deo.
“Tafadhali sana Levina, sina maana ya kukutesa lakini naona kama najihatarisha sana pamoja na kukuweka wewe kwenye matatizo.”

“Kivipi Deo, mi sikuelewi mwenzio?”
“Namaanisha hivi, nakupenda sana Levina lakini sitaki kuwaudhi wazazi wako! Naamini wakigundua watakasirika sana na watanitimua hapa kwenu, nimetoka mbali sana Levina kuja mjini kutafuta maisha, sitaki mapenzi yaniharibie maisha yangu ya baadaye…”

Wakati Deo akiendelea kujitetea mbele ya Levina, walisikia geti la nje likifunguliwa na gari la wazazi wa Levina likaingia ndani. Kwa haraka Deo alitoka nje na Levina naye akaelekea chumbani kwake huku wakiahidiana kuzungumza vizuri baadaye wakiwa peke yao.

***
Deo alijitahidi kuficha hisia zake mbele ya wazazi wa Levina. Bado hofu ilikuwa imeupamba mtima wake. Muda wa chakula cha jioni ulipowadia, kama kawaida familia nzima ilijumuika Dinning room kwa ajili ya maakuli. Kwa makusudi kabisa, Levina alijisogeza na kukaa jirani na Deo, akamsaidia kumpakulia chakula na kumkaribisha kwa heshima.

Wakati wakiendelea kula huku wakibadilishana mawazo hapa na pale, Levina alikuwa akimtazama Deo usoni kwa kuibia na kuishia kutabasamu mwenyewe. Mchezo ule ulishtukiwa na mama yake Levina, ambaye hata hivyo alijikausha ili awanase vizuri.

Kwa aibu alizokuwa nazo Deo, alijikuta akishindwa hata kula kwa uhuru kwani mamcho ya Levina yalikuwa hayabanduki kwake. Kaamua kujikaza kiume na kumtaza na yeye usoni bila kujali kuwa wamekaa na baba na mama. Macho yao yalipogongana, wote walitabasamu kimahaba, hali iliyomfanyampaka baba Levina kushtuka.
 
Penzi linachipuka kutoka ndani mwa Levina kwenda kwa Deo, kijana anayefanya kazi nyumbani kwao kwa kasi ya ajabu sana. Anashindwa kufanya kazi vyema kutoka na hisia hizo kali za mapenzi. Anajaribu kumweleza Deo, ambaye alimkubalia kwa shangwe!

Hili lilimfanya afunge duka lake haraka na kurejea nyumbani ili aweze kupata wasaa wa kuzungumza na Deo, lakini jambo la ajabu, alipofika akakuta Deo akiwa na maamuzi mengine mapya! Hakuwa tayari kuwa naye kimapenzi, kiasi cha kumsukuma mbali!

Baadaye wakiwa kwenye meza ya chakula, Levina alionesha alama zote kuwa anampenda Deo au walikuwa katika uhusiano, jambo ambalo baba yake, aliligundua! Akahisi kuwepo kwa jambo linaloendelea kimya kimya! Je, nini kitatokea? Endelea kufuatilia...

MZEE Masamu aligundua kitu kupitia macho ya mwanaye aliyekuwa akimwangalia Deo kwa macho yaliyojaa ubembe wa mahaba. Ni kitu ambacho hakukipenda hakika, hakutaka kabisa mwanaye awe na uhusiano na kijana yule. Hakuwa na hadhi ya familia yao.

Mara ghafla, akasogeza pembeni sahani yake ya chakula na kunawa mikono yake, jambo hilo lilimshangaza sana mke wake.
“Vipi baba Levina?!”
“I’m okay!”

“No dady, you are not okay, vipi chakula hujakipenda?” Mama Levina akasema kwa sauti ya taratibu sana.
“Nimeshiba mama Levina,” akasema mzee Masamu akimwangalia Levina kwa macho yenye kiashiria kibaya.

Mama Levina aliweza kugundua kwamba kuna jambo ambalo si la kawaida lilikuwa likiendelea. Anamfahamu vizuri sana mume wake, hakuwa na kawaida ya kushiba haraka kiasi kile, lazima kulikuwa na kitu. Naye akasogeza sahani yake pembeni na kunawa mikono.
“Mom, kwanini mnasusa chakula?” Levina akauliza kwa mashaka kidogo.

“Shiiiiii...” mama Levina akamnyamazisha mwanaye.
Deo akagundua kwamba mchezo wa Levina ulikuwa umegundulika, mara moja akanawa mikono na kukimbilia chumbani kwake. Bwana na Bibi Masamu wote kwa pamoja wakaongozana kwenda chumbani kwako kulala.

“Mume wangu mpenzi, nini tatizo? Nini kimetokea mpenzi wangu, maana naona haupo sawa kabisa!” Mama Deo akamwuliza mumewe walipoingia chumbani kwao.
“Unataka kusema hujaona chochote?” Mzee Masamu akasema kwa hasira.
“Nini tena dear?”

“Hivi unakumbuka kwanini tulimwondoa Rashid hapa nyumbani?”
“Ndiyo!”
“Unaona anayofanya mwanao?”
“Nani Levina?”

“Kwani nani mwingine?”
“Kivipi basi mume wangu?”
“Hujaona anavyomwangalia yule kijana?”
“Kwakweli sijawa makini kuwaangalia mume wangu!”

“Sasa wewe kuwa makini au usiwe makini, lakini nataka kukuambia kwamba, sitaki matatizo katika familia yangu! Deo hana hadhi ya kuwa na mwanangu!”
“Kwani amesema anataka hivyo?”
“Hapana, lakini dalili zipo wazi.”
“Nitazungumza na Levina!”

“Siyo utazungumza naye, nenda ukaongee naye sasa hivi, sihitaji matatizo katika familia yangu. Narudia tena sihitaji matatizo katika familia yangu, nenda kazungumze naye tafadhali.”

“Nimekuelewa mume wangu, ngoja niende nikaongee naye.”
Mama Levina akatoka haraka na kumuacha mumewe chumbani akiwa amefura kwa hasira. Alipofika sebuleni, alimkuta Levina akiwa anamalizia kuondoa vyombo mezani.
“Levina nahitaji kuongea na wewe!”

“Natoa vyombo mama!”
“Achana navyo isitoshe si kazi yako, kwani Helena yupo wapi? Hiyo ni kazi yake, haikuhusu wewe hata kidogo.”
“Najua mama, lakini...” Levina akaendelea kujitetea.
“Wewe tusikilizane!”

“I’m coming mom!”
“Hurry up!”
“Ok mom!”
Levina akaacha kila kitu na kujisogeza kwa mama yake, aliyekuwa amekaa kwenye sofa kubwa pale sebuleni.

“Hebu niambie, nini kinaendelea kati yako na Deo?!” Mama yake akamwuliza mara baada ya kukaa sofani.
“Unamaanisha nini mama?”
“Macho yako yanaonesha jinsi unavyofahamu ninachomaanisha!”
“Sijui kitu mama, kwani vipi?”

“Sasa mimi sina kitu cha kuzungumza zaidi au kubembelezana na wewe, lakini nataka kukuambia kwa kifupi sana, kama una wazo la kuanzisha uhusiano na Deo, futa kabisa wazo hilo!”
“Uhusiano?”
“Ndiyo nimekuambia sasa, ondoa wazo hilo kichwani mwako na kama mmeshaanza tafadhali acha mara moja!”

“Maamaaa...mimi na Deo wapi na wapi mama?”
“Hili agizo limetoka kwa baba yako!” Mama Deo akaongeza kusema.
“Mungu wangu, kweli mama?” Levina akashtuka sana.
“Nadhani unamfahamu vizuri sana mzee Masamu, unajua hasira zake, sasa endelea na upuuzi wako ndiyo utajua kitakachotokea!” Mama yake akasema na kusimama kisha akaondoka zake.

Levina akabaki pale subuleni akiwa mwenye mawazo mengi sana kichwani mwake. Alimfahamu vizuri sana baba yake, kama ni kweli yeye ndiye alikuwa ameagiza aachane na Deo, basi hali ilikuwa mbaya kuliko alivyofikiria.

Jambo hilo lilimtisha sana, lakini halikusababisha penzi lake dhidi ya Deo lishuke, bado alihisi penzi zito sana moyoni mwake, alimpenda sana Deo na hakuwa tayari kumpoteza.
Je, Levina atatii kauli ya mama yake?
 
Tayari mambo yamekuwa mabaya kwa upande wa Deo, ambaye Levina anaonekana kumpenda sana, lakini kitu cha ajabu ni kwamba, Levina anashindwa kuficha hisia zake na hivyo kusababisha baba mzazi wa Levina mzee Massamu kuhisi kitu!

Jambo hilo lilimtisha sana Deo, ambaye aliingia chumbani kwake akiwa na mawazo tele akianza kuhofia kupoteza ajira yake. Akiwa bado ana mawazo, usingizi ukiwa umekataa kabisa kumchukua, akasikia mtu akigonga mlango. Akashtuka sana.

Alipouliza aliyekuwa akigonga ni nani, hakujibu! Je, nini kitatokea? Endelea kuisoma...

DEO alishtuka kuliko kawaida, mawazo tele kichwani mwake yakamuandama, kitu kilichoingia kwa kasi sana akilini mwake ni kwamba aliyekuwa akigonga mlango ule alikuwa ni mzee Massamu.

Hapo hakika ungekuwa mwisho wa ajira yake. Jambo ambalo hakutaka kabisa litokee. Akasogea mpaka kwenye kitasa cha mlango wa chumbani kwake, akasogeza mdomo wake kwenye tundu la funguo, akauliza kwa sauti ya chini kabisa...
“Nani?”

“Fungua!” Sasa akajibiwa na sauti ya kike, ambayo haikuwa ngeni sana masikioni mwake.
Alikuwa ni Levina.
“We’ Levina, acha ujinga bwana, rudi chumbani kwako.”
“Fungua kwanza, kuna kitu nataka kukuambia.”
“Nini?”

“Fungua.”
Deo akatumia muda wa dakika mbili tatu kuwaza, kisha akaamua kwenda kufungua ili kuepuka kelele za levina ambazo zingeweza kusababisha matatizo zaidi.
“Haya unasemaje?” Akamwuliza baada ya kufungua mlango.
“Kabla hata sijakaa?” Akauliza Levina kwa sauti ya chini, ambayo Deo alishtuka sana kuisikia, akihisi kama ni kubwa.

“Ongea taratibu bwana...” Deo akasema kwa woga.
“Niongee taratibu nini? Unamuogopa nani?”
“Wazazi wako.”
“Wameshalala bwana.”

“Kwani unasemaje?”
“Acha utoto, inamaana hujui kwamba mimi nakupenda?”
“Najua.”
“Sasa?”
“Sitaki tena.”

“Unasemaje?”
“Sitaki tena.”
“Utataka Deo, lazima utake, hujui ni kwa kiasi gani nimehangaika kukupata. Hujui nimefanya mambo mangapi na wakati mwingine kuwakosea watu kwa sababu yako.”
“Lakini Levina ukumbuke kwamba ulisema unanileta kazini.”

“Ndiyo nakumbuka.”
“Sasa?”
“Lakini si nilikuambia kwamba nakupenda? Unadhani ningeweza kufanya mambo yote hayo hivi hivi tu!”

“Hivi unajua kwamba haya mambo ni ya hatari sana? Kwanza baba yako anaonekana ameshaanza kuhisi kwamba kuna kitu kinaendelea, huoni kwamba ni tatizo kwangu? Hivi nikipoteza kazi, unadhani nitakuwa mgeni wa nani mimi?”

“Acha kuwaza mambo ya kijinga...” akasema Levina akivua gauni lake jepesi la kulalia.
“Acha kufanya hivyo Levina.”

Levina hakusikia kitu, akalitupa mbali baada ya kumaliza kulivua na kumsogelea Deo, kisha akamsukuma kitandani. Kama mzigo Deo akaanguka kitandani na mara Levina akamzidi ujanja, dakika chache baadaye wakajikuta wakiwa kwenye kiota cha huba ya mapenzi, wakiwa wamesahau shida zote za ulimwengu.

***
“Umeongea naye?” Mzee Massamu akamwuliza mkewe.
“Ndiyo.”
“Anasemaje?”
“Aseme nini?”
“Kwahiyo hajasema chochote?”

“Simaanishi hivyo...kifupi amekataa.”
“Amekataa?”
“Ndiyo amekataa.”
“Sasa kuanzia leo anza kuwafuatilia utapata majibu, tena nahisi huenda huwa wanalala pamoja usiku. Ngoja muda uende kidogo, nataka kwenda kuhakikisha mwenyewe leo.”

“Sawa mume wangu, unajua kama itakuwa ni kweli, utakuwa mchezo mbaya sana.”
“Siyo mchezo mbaya tu, sitaki mwanangu ajiingize kwenye matatizo. Unajua kuolewa na lofa, ni sawa na kukaribisha ulofa katika familia. Hilo siwezi kuliruhusu likatokea katika familia yangu. Siwezi kabisa.”
“Ni kweli kabisa baba Levina...itakuwa aibu kwa familia,” akasema mama Levina akiunga mkono kauli ya mumewe.

***
Saa nane na dakika zake za usiku, Mzee Massamu aliamka kitandani na kutoka nje taratibu kabisa. Akaenda moja kwa moja hadi kwenye mlango wa chumba cha Levina. Akatega sikio kusikia kama Levina alikuwa akihema ndani, lakini hakusikia kitu. Kwakuwa taa ilikuwa haijazimwa, akaamua kuchungulia kupitia kwenye tundu la ufunguo kuangalia kama alikuwemo mle ndani.

Hakuwepo!
Akashtuka sana.
Akashika kitasa cha mlango na kukizungusha taratibu, mlango ukafunguka wenyewe. Mzee Massamu akaingia mpaka ndani na kuangalia kila kona, hakuona mtu! Ni kweli Levina hakuwemo ndani.
“Shiiiti, huyu mtoto amekwenda wapi?” Akawaza.

Papo hapo likaja wazo lingine, akahisi huenda alikuwa ameingia msalani, kwa bahati nzuri choo kilikuwa mle mle ndani. Kwahiyo akaamua kuita kwa sauti ya chini...
“Levina...Levina...we Levina...” lakini Levina hakuitika.
Hapo akaamua kuusogelea mlango wa chooni, akajaribu kuusukuma kwa nguvu! Ukafunguka!
Levina hakuwepo!

“Lazima atakuwa chumbani kwa Deo,” akawaza na kutoka chumbani kwa Levina haraka.
Akapiga hatua za taratibu hadi kufikia mlango wa Deo. Korido nzima ilikuwa kimya kabisa. Alipoufikia mlango wa Deo alitarajia kusikia kelele za mahaba chumbani, lakini hakusikia.

Chumba kilikuwa kimya kabisa. Hakujiuliza mara mbili, akajaribu kuusukuma ule mlango ambapo ulifunguka mara moja kwakuwa haukufungwa!
Alihisi kuchangikiwa!
Akahisi kuzimia!

Alichokiona mle chumbani, ilikuwa vigumu sana kuamini. Macho yake yaliona gauni la kulalia la mwanaye likiwa chini, huku nguo yake ya ndani ikiwa juu ya kiti! Deo alikuwa amelala na mwanaye wakiwa kama walivyozaliwa!
Alihisia harufu ya damu!
Akatamani kuua!

Lakini akajipa moyo!
“Deo unamfanya mwanangu hivi?” akajisemea moyoni mwake.
Haikuwa na maana kwao maana wote walikuwa wameishilia kwenye usingizi mzito, wakiwa kama walivyozaliwa. Busara ya Mzee Massamu ikatumika, akaamua kutoka mle chumbani taratibu na kurudi chumbani kwake. Akamkuta mkewe akiwa macho. Kwa hali aliyoingia nayo, mkewe akajua lazima kulikuwa na kitu kibaya kimetokea.

“Vipi mume wangu?”
“Nenda mwenyewe chumbani kwa Deo ukajionee.”
“Kuna nini?”
“Nenda mke wangu,” akasema Mzee Massamu akitoka jasho mwili mzima.
Je, nini kitatokea?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom