Hadithi: Usife Haraka Mpenzi Wangu

Hadithi: Usife Haraka Mpenzi Wangu

leopatra analia mbele ya kitanda cha Deogratius, ambaye alikuwa amelazwa baada ya kupigwa risasi. Zilibaki wiki tatu tu, kabla ya ndoa yao. Machozi machoni mwa Cleopatra yaligoma kabisa kufutika!
Dokta akamtoa nje, akimbembeleza na kumpa moyo kwamba asijali, mgonjwa wake angepona. Cleopatra haamini hilo, anazidi kulia kwa uchungu, mawazo tele kichwani mwake yakizidi kumzonga.
Alichowaza yeye ni ndoa tu! Atafungaje wakati mpenzi wake alikuwa amelazwa wodini? Endelea kufuatilia...

AKIWA katika mawazo ya kumuumiza moyo, simu yake ikaita. Akaangalia jina la mpigaji akakutana na jina lililoandikwa ‘My Mumy’. Alikuwa ni mama yake mzazi akimpigia. Kwa muda akaiangalia ile simu akijishauri kupokea, lakini alisita.

Alijua sababu ya simu ya mama yake, kwa vyovyote vile, angetaka kujua kuhusu Deo, jambo ambalo aliamini lingeweza kuamsha machozi upya, kitu ambacho hakutaka kabisa kitokee. Lakini baadaye akaamua kupokea...

“Patra uko wapi?” Ndiyo neno alilokutana nalo baada ya kupokea simu ya mama yake.
“Hospitalini!”

“Upo sehemu gani, maana na mimi tayari nimeshafika hapa Muhimbili!”
“Nipo huku MOI mama!”

“Nakuja!”
Muda mfupi baadaye, mama yake akatokea. Cleopatra alipokutanisha uso na mama yake, machozi kama maji yakaanza kumwagika machoni mwake. Akamkimbilia na kumkumbatia.

“Mama Deo wangu anakufa mama...” akasema kwa hisia za uchungu sana.
“Hapana mwanangu, hutakiwi kuwaza hayo mama...yupo wapi?”
“Wodini!”
“Twende...”

“Hawaruhusu kwenda sasa hivi, muda wa kuwaona wagonjwa umepita!”
“Tatizo ni nini hasa lakini?”
“Amepigwa risasi!”
“Na nani?”

“Hawajulikani mama.”
“Wapi?”
“Mjini. Daktari anasema aliletwa na wasamaria wema baada ya kumuokoa!”

“Maskini, ana hali mbaya sana?”
“Haongei mama, amepigwa risasi ya bega, lakini dokta anasema imekuwa vizuri maana haijatokeza upande wa pili.”
“Mungu ni mwema mwanangu.”

“Namuomba sana amponye ili tufunge ndoa yetu kwanza.”
“Sote ndiyo dua yetu!”
Kwakuwa muda ulikuwa umeshapita wakaondoka kwa ahadi ya kurudi jioni kumuona.

****
Saa 11:00 jioni, Cleopatra na mama yake walikuwa wanaingia katika wodi aliyolazwa Deo. Hawakuamini walipofika kitandani mwake na kumuona akiwa amefumbua macho yake. Cleopatra akalia kwa furaha.
“Pole sana sweetie!”

“Ahsante!” Deo akajibu kwa sauti ya taratibu sana.
“Shikamoo mama...” Deo akasalimia.

“Marahaba mwanangu, pole sana!”
“Ahsante mama!”
“Ilikuwaje?” Cleopatra akauliza akiketi kitandani kwa Deo.

“Hata sielewi, nakumbuka nilikuwa kwenye lifti, nilipofika ghorofa ya tatu lifti ikasimama, wakaingia wanaume watatu, tukaanza tena kushuka hadi ghorofa ya pili, ikasimama tena. Ghafla nikasukumwa nje, kilichofuata ilikuwa ni mlio wa risasi.

“Nikashtuka sana na kupoteza fahamu. Nilipozinduka, nikajikuta nipo hapa hospitalini.”
“Unaweza kumkumbuka kwa sura hata mmoja wao?”
“Hapana.”
“Pole sana, lakini unajisikiaje sasa?”

“Siwezi kujielezea, nahisi maumivu ya mkono na bega, lakini sielewi hali yangu hasa!”
“Pole sana, utapona usijali,” mama yake Cleopatra akasema.
“Nashukuru sana mama.”

Cleopatra akamlisha chakula huku akimwambia maneno matamu ya kumtia moyo! Kidogo Deo akaanza kujisikia vizuri baada ya kupata faraja kutoka kwa mpenzi wake. Muda wa kuwaona wagonjwa ulipopita wakaondoka zao.

“Ugua pole dear, kesho asubuhi nitakuja kukuona.”
“Ahsante sana mpenzi wangu, nakupenda sana. Ahsante kwa kujali kwako!”
“Ni wajibu wangu...utapenda kula chakula gani asubuhi?”
“Chochote tu baby!”

“Chagua mwenyewe mpenzi wangu!”
“Nadhani mtori utanifaa zaidi.”
“Ok! lala salama, ugua pole, you will be okay!”
“Thank you baby!”

Cleopatra na mama yake wakaondoka, wakamuacha Deo akiwa ametulia kimya kitandani, akisikilizia maumivu yake ya bega. Mpaka wakati huo, hakuelewa ni kwanini watu wale walimpiga risasi, maana hakuwa na fedha na wala hawakumwibia! Hilo liliendelea kuzunguka kichwani mwake bila kupata majibu.

***
Anahisi kama ameguswa na mkono wa mtu, anajaribu kuyafumbua macho yake kwa shida kidogo kutokana na mzigo wa usingizi aliokuwa nao! Alilala sana siku hiyo. Uchovu na usingizi ulisababishwa na mambo mawili; Deo alikuwa hajalala usiku mzima kwa maumivu ya bega, ndiyo kwanza asubuhi hiyo alianza kuhisi usingizi.

Dawa alizokunywa, zilikuwa kali na zilimchosha sana mwili wake. Hayo yalitosha kabisa kumfanya, saa moja hii ya asubuhi, macho yake yaendelee kuwa mazito. Anajaribu kuyafumbua kwa shida na kumtazama mtu huyo!
Akashtuka sana!

Hakutegemea kukutana na sura hii hospitalini. Nani amemwambia kwamba amelazwa? Ni jana tu, alipata matatizo, leo hii amejuaje? Nani amempa taarifa za yeye kuumwa? Yalikuwa maswali yaliyofumuka mfululizo kichwani mwake, bila kupata majibu stahiki!
Anazidi kumwangalia mwanamke huyu ambaye naye amesimama kama ameganda...

“Pole Deogratius...pole sana kwa matatizo!” Mwanamke huyo akatamka kwa sauti ya taratibu sana.
Deo hakuitika!

“Maskini Deo, najua ni kiasi gani unaumia, najua kwamba ni jinsi gani ndoa yako itakavyokuwa na ugumu wa kufungwa. Bila shaka mmebakiza wiki tatu tu, sidhani kama utaweza kupanda madhabahuni ukiwa katika hali hii...pole sana...ni majaribu tu ya shetani,” akatamka kwa yakini, akiongea kwa mpangilio mzuri sana.
Deo hakujibu neno!

“Huyu vipi? Amejuaje nipo hapa? Amejuaje natarajia kufunga ndoa? Amejuaje mambo yangu?...amejuaje?” Akazidi kujiuliza Deo, lakini majibu hakuwa nayo.

“Nakupa pole huitiki, kwanini? Au hujapenda mimi kuja hapa?” Mwanamke yule akasema, akionekana kusononeka na mapokeo ya Deo.

Kwa ghafla sana, macho ya Deo yakaanza kupatwa na unyevunyevu, baadaye machozi yakaanza kuchuruzika machoni mwake. Ubongo wake ukasafiri miaka kumi nyuma. Akayatupa macho yake juu ya dari, kisha kumbukumbu zote za maisha yake yaliyopita zikaanza kumjia kama anatazama sinema ya kusisimua...

Sinema ya maisha yenye kila aina ya machafuko na mataabiko. Mateso, dhiki na kuonewa. Masimango, kutukanwa na kudhalilishwa. Ilikuwa sinema mbaya, lakini yenye mwisho mzuri wa kupendeza, mwisho ambao baadaye uliingia shubiri.
Ikawa chungu!
Sinema ikaanza...
 
Cleopatra analia mbele ya kitanda cha Deo aliyelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, hali yake ni mbaya na anatamani sana kuona Deo wake akiamka ili waende wakafunge ndoa yao kanisani.

Baada ya saa kadhaa, Deo anazinduka, Cleopatra na mama yake walipoenda baadaye, walimkuta Deo akiwa ameshazinduka, hawezi kuzungumzia vizuri jinsi alivyopata ajali ile. Wanaondoka kwa ahadi ya kurudi tena asubuhi inayofuata.

Muda mfupi baada ya wao kuondoka, anaingia mwanamke mmoja na kumpa pole kwa matatizo aliyoyapata. Deo hajibu kitu muda wote mwanamke yule alipokuwa akizungumza. Lakini baadaye, Deo akaonekana kuwa na mawazo ya ghafla!

Akili yake ikasafiri miaka kumi iliyopita, akaanza kukumbuka matukio yote yaliyotokea katika maisha yake. Kila kitu kikaanza kuonekana kama sinema ya kusisimua.
Je, anakumbuka nini? Endelea....

Oktoba 22, 1999 – Dar es Salaam
Ni siku nyingine ya pilikapilika, kama ilivyokuwa kwa siku zilizotangulia, leo pia Deo ameamka saa 11:00 alfajiri kama kawaida yake. Alipoamka kitu cha kwanza kufanya ni kumwagilia maji maua, kufanya usafi wa mazingira na kuwapeleka watoto shule.

Aliporudi, alitoka nyumbani kwa bosi wake Mburahati, akaenda sokoni Tandale, kilometa zaidi ya kumi na tano kwa miguu. Hapo ndipo anapofanya kazi ya kuuza mchele hadi saa 11:00 jioni, anapoanza safari nyingine ya kurudi nyumbani kwa miguu.

Siku yake humalizika kwa kufunga mifuko ya barafu hadi saa sita za usiku anapopata muda wa kupumzika, kabla ya kukurupushwa tena alfajiri inayofuata.
Hayo ndiyo maisha yake!

Deogratius Mgana, kijana mchapakazi, hajawahi kupumzika hata siku moja tangu alipoanza kazi katika nyumba ya mzee Maneno, miaka mitatu iliyopita. Alikuja Dar es Salaam, akitokea nyumbani kwao Kiomboi Singida kwa lengo moja tu, kutafuta maisha. Mshahara wake ukiwa ni shingili elfu arobaini na tano tu, kwa kazi zote anazofanya.

Akiwa ametulia kwenye ubao wake sokoni, anatokea dada mmoja mrembo sana. Si mgeni machoni mwake, ni mteja wake wa kila siku, ambaye amekuwa akimhudumia mchele karibu mara mbili au tatu kwa wiki!
“Mambo kaka?” Dada yule akamsalimia.

“Poa, karibu!”
“Ahsante, nipimie kilo tano!”
“Usijali!”

Deo akampimia mchele aliohitaji na kumuwekea kwenye mfuko, kisha akampa. Yule msichana akalipa na kuondoka...baada ya hatua nne, akarudi tena.

“Samahani kaka, nimeshakuwa mteja wako wa kudumu sasa, nadhani ni vizuri kujua jina lako. Mimi naitwa Levina, wewe je?”
“Deogratius, lakini wengi wanapenda kuniita Deo!”
“Nashukuru kukufahamu, sasa nimeridhika, kwaheri!”
“Poa!”

Deo alimwangalia Levina hadi alivyoishilia, namna alivyokuwa akitembea, namna alivyokuwa akiongea vilimpa picha ya tofauti sana. Alianza kuhisi eti huenda Levina anampenda, lakini alijishangaa, maana lilikuwa jambo gumu kidogo!

Levina ampende yeye?
Muuza mchele?
Mbona alikuwa anawaza mambo makubwa sana? Lakini bado hakutaka kuuhakikishia ubongo wake moja kwa moja juu ya hilo. Aliamini kwamba lazima kulikuwa na kitukinaendelea. Kwanini atake kujua jina lake? Ana umuhimu gani hasa?

“Au zali la mentali nini? Si kawaida mteja kutaka kujua jina langu bila sababu za msingi. Lazima kuna kitu kinaendelea, lazima....” akawaza Deo akiwa anamwangalia mpaka anavyoishilia mbali.

Akabaki akiwa na mawazo mengi kichwani mwake, tayari hisia za mapenzi dhidi ya Levina zilianza kumuingia, lakini aliwaza sana namna ya kumuingia, hakuwa na hadhi ya kutoka na Levina.

****
“Mambo Deo?”
“Poa Levina, mzima?”
“Nipo poa!”
“Za nyumbani?”
“Salama kabisa.”

“Ngapi leo?”
“Pima kilo kumi!”
“Wewe kwani mna sherehe?”
“Hapana ni bajeti tu!”

Deo akapima mchele alioagizwa, akamimina kwenye mfuko na kumkabidhi Levina, aliyeupokea huku akiachia tabasamu mwanana kabisa.
“Ahsante sana Deo!”
“Nashukuru pia!”
“Samahani Deo, naweza kupata namba zako za simu?” Levina akamwuliza.

“Simu?”
“Ndiyo!”
“Mimi sina, labda nikupe namba za nyumbani!”
“Hapana, nataka namba zako mwenyewe!”
“Sina.”

“Kwanini?”
“Maisha Levina!”
“Ok! basi chukua zangu...ukimaliza kazi zako nipigie kwenye kibanda cha simu, nahitaji kuzungumza na wewe!” Levina akasema akiandika namba na kumkabidhi Deo akiambatanisha na noti ya elfu tano.
“Ahsante sana Levina, nitakupigia!”
“Usiache tafadhali, ni muhimu sana!”
“Sawa.”

Levina ni nani hasa? Anataka kumwambia nini Deo? Fuatilia..
 
Samahani Deo, naweza kupata namba zako za simu?” Levina akamwuliza.
“Simu?”
“Ndiyo!”
“Mimi sina, labda nikupe namba za nyumbani!”

“Hapana, nataka namba zako mwenyewe!”
“Sina.”
“Kwanini?”
“Maisha Levina!”

“Ok! basi chukua zangu...ukimaliza kazi zako nipigie kwenye kibanda cha simu, nahitaji kuzungumza na wewe!” Levina akasema akiandika namba na kumkabidhi Deo akiambatanisha na noti ya elfu tano.
“Ahsante sana Levina, nitakupigia!”
“Usiache tafadhali, ni muhimu sana!”
“Sawa.”
ANZA SASA KUISOMA....

DEO alibaki na maswali mengi sana kichwani mwake bila kuwa na majibu, bado kitu kikubwa kilichokuwa kinamsumbua ni kwamba, ni kweli hisia zake zilikuwa sawa kwamba Levina alikuwa anampenda au zilikuwa hisia zake mwenyewe?

Hakujua hakika!
Lilikuwa suala gumu sana kichwani mwake kupitishwa moja kwa moja kuwa Levina alikuwa anampenda, hata hivyo ndani ya moyo wake alijua wazi kuwa kabisa yeye alimpenda sana Levina.
“Nitampataje jamani huyu msichana? Nahisi kabisa moyo wangu unaniambia kuna kitu fulani, ni kweli nampenda sana Levina,” akawaza Deo.

Siku nzima alishinda akiwa na mawazo, alitamani sana kumpigia simu Levina ili amsikilize alichokuwa akitaka kumwambia, lakini kwa sababu alikuwa na wateja wengi alishindwa kufanya hivyo, lakini kubwa zaidi kelele za pale sokoni zilimfanya ashindwe kumpigia kwakuwa alifahamu kwamba hawataweza kuelewana vyema!

Jioni alifunga biashara yake na kuanza kurudi zake nyumbani, kwakuwa alipewa pesa na Levina na pia alikuwa na haraka ya kuwahi kumpigia simu, akaona bora apande daladala.

Akachepuka kutoka sokoni Tandale hadi Manzese ya Agerntina, pale akapanda daladala iliyompeleka mpaka Magomeni ya Mwembechai, akashuka na kutafuta kibanda cha simu.
“Habari yako dada?” Deo akamsalimia mhudumu wa kibanda cha simu.
“Salama, karibu kaka’ngu!”

“Nahitaji kupiga simu.”
“Sawa, naomba namba.”
Deo akamtajia.

Yule dada akabonyeza zile namba kwenye simu, kisha akaweka saa yake ya kuhesabu muda tayari na kumpatia Deo simu.
“Hallow,” sauti laini ya kike ilisikika upande wa pili, baada ya kupokelewa.

“Hallow, habari yako?”
“Nzuri, bila shaka ni Deo?”
“Umejuaje?”
“Kwanza sauti yako, lakini pia wengi wanaonipigia simu namba zao nimezi-save!”
“Niambie Levina.”

“Poa!”
“Nimekupigia kama ulivyoniambia.”
“Hujakosea kitu Deo, tena umefanya vizuri sana, maana nilikuwa nawaza namna ya kukupata kama usingenipigia.”
“Sawa...sawa...nini kipya?” Deo akauliza.

Kimsingi hakuonekana kuwa na jambo lolote la kuzungumza zaidi ya kusubiri kumsikiliza Levina.
“Sikia Deo, kuna kitu cha muhimu sana nilitaka kuzungumza na wewe, lakini naona kama mazingira hayafanani kabisa.”
“Kivipi?”

“Nahisi upo kwenye kelele sana, kiasi kwamba hata hutakuwa na usikilizaji na uelewa mzuri wa nitakayokuambia.”
“Kwani unataka kuniambia nini?”

“Subiri Deo, usiwe na haraka kiasi hicho, huwezi kupata muda nikazungumza na wewe nje ya kazini kwako?”
“Kama lini?”
“Wewe off yako ni lini?”

“Jumapili, ingawa si mapumziko ya moja kwa moja!”
“Kivipi?”
“Huwa siendi sokoni, lakini kazi nyingine za nyumbani zinaendelea kama kawaida.”
“Sasa?”

“Naweza kujaribu kutoka mara moja, lini unataka tuonane?”
“Itakuwa Jumapili, lakini kesho nitakuja tena kuzungumza na wewe zaidi!”
“Sawa.”
“Haya usiku mwema mwaya Deo!”

“Ahsante,nawe pia ulale salama.”
Wakakata simu zao.
Deo akalipa na kuanza kutembea kwa miguu akienda Mburahati, nyumbani kwa bosi wake. Ndani ya moyo wake alijihakikishia kumpenda Levina, lakini ufukara wake ulimfanya ashindwe kuelewa namna ambavyo angeweza kumfanya Levina awe wake.

Alifika nyumbani nusu baadaye, kwanza alikabidhi mahesabu, akaingia bafuni kuoga. Aliporudi alifikia mezani kupata chakula cha usiku, kabla ya kwenda jikoni kuanza kazi ya kufunga mifuko ya barafu kama ilivyo kawaida yake.

***
Kama ni mateka, alikuwa mateka asiye na hali, ambaye pamoja na kutekwa kwenyewe, alikuwa tayari kufanywa mateka. Levina alijishangaa sana jinsi alivyotokea kumpenda Deo.

Hakika hakuwa hadhi ya mwanaume wa kuwa naye, uwezo wao kifamilia, heshima waliyonayo wazazi wake ni kati ya mambo ambayo yalimchanganya sana na kumfanya ashindwe kuwa na maamuzi ya moja kwa moja ya nini cha kufanya kwa ajili ya Deo.

Pamoja na yote hayo, moyo wake ulikuwa na kitu kimoja tu...
Mapenzi!
Alimpenda sana Deo, lakini alikuwa na changamoto nyingi sana kichwani mwake. Kwanza aliwaza juu ya wazazi wake...hakujua kama wangekubaliana na wazo lake la kuolewa na Deo, kijana fukara ambaye hana mbele wala nyuma.

Hilo lilimchanganya sana kichwa chake, lakini alijipa moyo kwamba siku moja lazima Deo angekuwa mikononi mwake, yeye akiwa mama na Deo akiwa baba.

“Hilo nitahakikisha nalitimiza, maadamu nimempenda, hayo mengine nitajua baadaye!” Akawaza Levina.

***
“Mambo Deo,” alikuwa ni Levina akimsalimia Deo, asubuhi ya siku iliyofuata alipokwenda sokoni.
“Poa, za nyumbani?”
“Salama.”
“Kilo ngapi?”

“Hapana, leo sihitaji mchele, nimekuletea zawadi yako,” akasema Levina akimkabidhi bahasha ya khaki.
Deo akapokea...
“Hiyo ni simu Deo, imebidi nikununulie ili kurahisha mawasiliano yetu.”

“Mh! Ahsante sana jamani, lakini kwanini umeamua kufanya hivi?”
“Kwa sababu sisi ni marafiki, unajua tunatakiwa kudumisha urafiki wetu kwa kuwasiliana mara kwa mara, au wewe hupendi tukiwa marafiki?”
“Napenda sana, nashukuru sana!”

“Usijali, line imo humo humo ndani, tayari nimeshakuwekea vocha za elfu ishirini, zikiisha nijulishe nikuongeze nyingine.”
“Ahsante sana,” Deo akashukuru tena.

Haikuwa rahisi kuamini jambo hilo, zawadi ile kwa Deo ilikuwa zaidi ya zawadi,ule ulikuwa uthibitisho tosha kwamba Levina alikuwa anampenda.
Levina hakukaa muda mrefu sana, akaaga na kuondoka.

***
Siku zilivyozidi kwenda na kuwasiliana, mapenzi kati ya wawili hawa yalizidi kuchipuka kwa kasi, lakini si Deo wala Levina aliyekuwa tayari kueleza hisia zilizokuwa ndani ya moyo wake.

Wote waliishi na siri nzito za mapenzi ndani ya nafsi zao, lakini leo Levina amepata wazo la kufanya ili aweze kumnasa Deo. Alitumia kila njia kumuonesha kwamba anampenda na alichokuwa akikisubiri siku zote ni Deo kumtamkia kwamba anampenda, lakini hilo halikutokea.

Deo naye alishangazwa na jinsi Levina alivyopenda kuwa naye karibu na kumsaidia mambo mbalimbali, lakini aliogopa kumwambia kwamba anampenda, akihofia kupoteza urafiki wao ambao kwake ulikuwa na manufaa makubwa sana.

Levina ameshapata njia za kumsogeza karibu Deo ili iwe rahisi kwake kutamka kwamba anampenda. Alipanga mpango hatari, haukuwa mwingine zaidi ya kufanya jitihada mfanyakazi wao wa kiume wa nyumbani atimuliwe ili amfanyie Deo mipango ya kupata kazi nyumbani kwao.

Hapo ndipo angempata Deo kwa urahisi zaidi, maana angekuwa anammiliki. Hilo alijihakikishia kulifanya.

Je, nini kitatokea? Levina atafanikiwa kumpata Deo? Usikose kufuatilia ..........
 
Levina ametekwa kimapenzi na Deo. Kilichopo akilini mwake ni kumfukuzisha kazi kijana wao wa nyumbani ili nafasi hiyo ichukuliwe na Deo, hapo angempata kirahisi zaidi.
Je, itawezekana? Endelea...

LEVINA alikuwa mateka wa mapenzi, alimpenda sana Deo na alitaka kuhakikikisha anakuwa wake wa maisha yake yote. Kitu pekee kilichokuwa kichwani mwake ilikuwa ni namna gani angeweza kumwondoa Rashid nyumbani kwao na kufanya jitihada za kumwingiza haraka sana Deo nyumbani, hapo lengo lake lingeweza kutimia bila mushkeli kabisa.

“Mimi ndiye ninayejua thamani ya penzi langu kwa Deo, najua kama nikimwambia ghafla anaweza kunichukia na kuniona malaya, lakini nikimsogeza kwanza nyumbani, naamini itakuwa vyema zaidi maana hataweza kupindua,” akawaza kichwani mwake Levina.

“Lazima atakuwa wangu, lazima...” akazidi kujihakikishia ushindi.
Tayari alishakuwa na mbinu zake, mipango ilikuwa tayari kabisa, kilichobaki ilikuwa ni utekelezeji tu.

“Rashid hana ujanja wowote kwangu, mimi ndiye Levina na nitahakikisha namtoa nyumbani,” akazidi kupanga mipango ya kummaliza.

****
Ilikuwa Jumapili asubuhi, nyumba ikiwa kimya kabisa, wazazi wa Levina, mdogo wao mdogo pamoja na house girl wote walikuwa wamekwenda kanisani, nyumbani wakiwa wamebaki Levina na Rashid, kijana wa kazi.

“Rashidiiiiiii....” Levina akaita akiwa amekaa sebuleni akiangalia runinga.
“Naam dada...”
“Njoo!”
“Nakuja.”

Rashid akakimbia haraka hadi sebuleni alipokuwa akiitwa na Levina. Akamkuta akiwa ametulia kwenye sofa.
“Mambo kaka?” Rashid akasalimia.
“Poa,mzima?”
“Nipo poa, nina shida moja muhimu nataka unisaidie.”
“Nini?”

“Naomba uniazime simu yako mara moja, maana yangu imekufa display!”
“Haina pesa lakini.”
“Usijali, ninayo nitaongeza, kuna mtu nataka kuchat naye kidogo!”
“Hii hapa.”

“Poa basi, nikimaliza nitakushtua, unafanya nini nje?”
“Nakatia fensi, si unajua tena dingi akija akikuta sijakamilisha anaweza kuniletea muziki?”
“Poa bwana endelea.”

Levina akachukua ile simu na kuiangalia kwa dharau...
“Nakumaliza na simu yako hii hii,” akawaza kichwani mwake Levina.

Zoezi kubwa lililokuwa likiendelea ni kutuma meseji kutoka kwenye simu ya Rashid kwenda kwenye simu yake, huku akijibizana naye. Alipomaliza, akafuta meseji zote zilizoingia na kutoka kwenye simu ya Rashid, ili kuondoa ushahidi.

Baadaye akamrudishia Rashid simu yake.
“Umefanikiwa kuwasiliana naye?” Rashid akamwuliza Levina.
“Siyo kuwasiliana naye, ni kuwasiliana nao?”
“Kwani walikuwa wangapi?”
“Nilikuwa nachat na marafiki zangu kibao, si mmoja kama unavyodhani.”

“Poa, mi nipo nje.”
“Sawa kaka Rashid.”
Kwa alivyokuwa akizungumza, ni kama muungwana mwenye roho nzuri na upendo, lakini kikubwa alikuwa amepanga kumfukuzisha kazi Rashid.

Ni kijana aliyefanya kazi kwao kwa muda mrefu sana, akiaminiwa sana na wazazi wake, isingekuwa rahisi kumtoa nyumbani kwao kienyeji kutokana na utendaji wake kuwa bora kwa miaka mitatu aliyoishi kwa uaminifu mkubwa katika nyumba ile.

****
“Samahani kwa kukusumbua Deo, naamini wewe ni rafiki yangu, ni kweli?” Levina alimwambia Deo, jioni moja alipomsubiri Magomeni Mwembechai, ambapo Deo alikuwa anarudi nyumbani Mburahati.
“Naamini hivyo, sisi ni marafiki.”

“Kweli?”
“Naamini hivyo au?”
“Hata mimi pia, lakini nilitaka kupata uhakika kutoka kwako.”
“Sisi ni marafiki Levina.”
“Bila shaka huwezi kunificha chochote katika maisha yako.”
“Hilo halina ubishi.”

“Ulisema unaitwa Deo, ukoo wako ni nani na wewe ni kabila gani?”
“Mh! Jamani, kwanini?”
“Nataka tu, kujua.”
“Niite Deogratius Mgana, ni mwenyeji wa Kiomboi, Singida, nikimaanisha kwamba mimi ni Mnyiramba.”

“Ok! nimefurahi sana kukufahamu kwa uzuri Deo, mimi ni Levina Masamu, ni Mchaga wa Old Moshi.”
“Oh! Ahsante sana kukufahamu zaidi, lakini kwanini umeniuliza yote hayo?”

“Nina maana yangu, utaijua baadaye kidogo. Samahani, mshahara wako ni shilingi ngapi kwa mwezi?”
“Nalipwa elfu arobaini na tano.”
“Jamani zinakutosha kweli?”
“Nitafanyaje Levina, maisha...”
“Elimu yako ikoje?”

“Mimi?”
“Ndiyo!”
“Darasa la saba tu, nilifaulu lakini wazazi wangu wakakosa fedha za kuniendeleza.”

“Usijali, vipi utakuwa tayari nikikutafutia mahali pengine utakapolipwa fedha nyingi zaidi?”
“Ndiyo, hata sasa hivi.”

“Kweli?”
“Ndiyo!”
Levina akafurahi sana, mpango wake ulikuwa unanukia kukamilika.
 
Mpango wa kumtoa Rashid nyumbani kwao unaendelea, nia hasa ya Levina ni kumwingiza Deo nyumbani kwao.
Lakini moyoni aliumia sana, maana machozi ya Rashid yalikuwa yanamuuma sana!
Ni kweli alimsingizia. Nini kitatokea? Endelea kuisoma...

LEVINA aliumia ndani kwa ndani, alikiri kabisa kwamba Rashid hakuwa anahusika na chochote katika mchezo ule. Kitu pekee kilichomsukuma kufanya vile ni mapenzi yake ya dhati pekee, hakuwa na kitu kingine ndani yake zaidi ya hivyo.

Tangu Rashid alipoondoka kwenda chumbani kwake kukusanya mizigo yake, alijisikia mkosaji sana.
Mwenye roho mbaya sana!
Alijihisi kama si binadamu kabisa!
Sifa zote mbaya akajipa yeye!

Mama yake aliweza kugundua tofauti aliyokuwa nayo mwanaye, akaona njia pekee ya kugundua kilichokuwa kikimtatiza mwanaye ni kumuuliza tu!
“Nini tatizo tena mwanangu?”
Levina akabaki kimya!
“Levina...” mama yake akaita.

“Abee...” Levina akaitikia kwa kushtuka kidogo.
Ni kama alikuwa amegutuka kutoka katika usingizi mzito, lakini ukweli haukuwa huo. Levina alikuwa na mawazo ya usaliti. Kusema uongo na kumnyanyasa Rashid kwa sababu ya mapenzi.
“Una nini mama?!!”

“Inaniuma sana mama...” Levina akasema machozi yakidondoka machoni mwake, ni kama alikuwa akiumizwa na meseji za Rashid, lakini ukweli halisi haukuwa huo.
Ndani ya nafsi yake alikuwa akiumizwa na kitendo cha kumsingizia na si kufanyiwa kama ambavyo alitaka kutengeneza.

“Lakini ndiyo nimemtimua hivyo.”
“Amekosa adabu kabisa, yaani siku zote hizo naishi naye kama kaka yangu halafu anakuja kuniambia maneno machafu kiasi hicho? Hana adabu kabisa...” akasema Levina lakini kichwani mwake kukiwa na kitu kingine.

Moyoni mwake alihifadhi kitu tofauti kabisa, alikuwa na siri nzito sana, ambayo hakutakiwa kumwambia mtu yeyote, ilikuwa ni siri ambayo alitakiwa kuijua yeye na moyo wake pekee.

“Potelea mbali, kama ni kazi anaweza kupata mahali pengine, lakini nitapata wapi mwanaume kama Deo, lazima nifanye hivi, sina namna!” Akazidi kuwaza kichani mwake.

“Usijali mwanangu, nimeshamtimua huyu mwanaharamu. Hutakiwi kuwa na mawazo mwanangu na mimi mama yako nipo. Tena subiri...wewe Rashid, unasubiri nini? Kwani una mizigo gani mingi ya kuchukua muda mrefu kiasi hicho?” Akasema mama Levina akisimama kumfuata chumbani kwake.

Mama Levina alikuwa amevimba kwa hasira, akafika chumbani kwa Rashid na kumwita kwa sauti kubwa...
“Si naongea na wewe, hebu toka haraka nyumbani kwangu.”

“Natoka mama,lakini siku moja utakuja kugundua ukweli, siwezi kufanya mambo ya ujinga kiasi hicho mama, lakini kwakuwa wewe umeamua kumuamini Levina sawa!”

“Tena funga domo lako kabisa wewe mwanaharamu, inaonekana unataka kunigombanisha na mwanangu, unataka kuniambia mwanangu anaongopa?”
“Ndiyo mama!”
“Kwa lipi hasa?”

“Sijui mama, lakini ukichunguza utagundua ukweli.”
“Tena ishia hapo hapo kuniita mama, anayeruhusiwa kuniita mama ni yule anayeheshimu wanangu na kuwachukulia kama dada zake, si wewe mpumbavu!”
“Hapana mama!”

“We’ mwendawazimu, sina muda wa kubishana zaidi na wewe. Paki vitu vyako, nakwenda kukuchukulia pesa zako uondoke!”
Rashid akabaki kimya.
Mama Levina akaenda ndani haraka na kuchukua fedha alizokuwa akidaiwa na Rashid kisha akarudi na kumkuta tayari ameshajiandaa.

“Chukua pesa zako, tena nimekuongezea na elfu thelathini zikusaidie, ondoka kwangu!”
“Ahsante mama, lakini Mungu mwenyewe ndiye anayejua ukweli wa haya yote!”

“Hayo mahubiri yako huwa nakutana nayo kanisani, sasa sioni kama hata hapa nyumbani kwangu panafaa kuhubiriwa!”
“Siyo mahubiri mama, ni ukweli kabisa kutoka ndani ya moyo wangu!”
“Ukweli wa nini?”

“Sijamtumia zile meseji mimi mama.”
“Hivi wewe una akili? Zile namba ni zako au za nani?”
“Zangu.”

“Sasa kama ni zako, kwanini unaruka?”
“Unajua mama...juzi...” mama Levina hakumpa nafasi ya kumalizia utetezi wake.

“Hebu toka kwangu haraka tafadhali, sidhani kama bado nina nafasi ya kuendelea kuusikiliza utumbo wako, ondoka tafadhali!”
Rashid alikuwa anataka kumweleza mama Levina kwamba kuna siku alimuazima simu yake, lakini hakupewa nafasi hiyo.

Rashid akaondoka analia, mama Levina akiendelea kufoka huku akirusha mikono. Alikuwa amekasirika sana. Pamoja na utendaji kazi wake kuwa mzuri kwa muda mrefu aliokuwa akikaa naye, lakini siku aliyasahau yote hayo kwa meseji iliyoonekana kutumiwa mwanaye.

****
Mto wote ulikuwa umelowana kwa machozi, Levina alikuwa na uchungu sana ndani ya moyo wake. Usiku huo ulikuwa mgumu sana kwake, aliteswa na watu mawili; DEO NA RASHID!

Alifanya dhambi ya kumsingizia Rashid kwamba amemtongoza na akafukuzwa kazi. Hilo lilimuuma, lakini lingepoa kama kweli Deo angekubali kuwa naye. Lakini aliteseka sana, akiwa hana uhakika kama kweli Deo atamkubalia.

Tabu yote ya nini? Usiku ule ule, akachukua simu na kumpigia Deo.
Je, nini kitatokea?
 
Zoezi la kwanza la Rashid kuondoka nyumbani kwao, linakamilika. Zoezi lililokuwa linafuata kwa Levina ilikuwa ni kuhakikisha Deo anaingia nyumbani kwao. Pamoja na mafanikio yale makubwa, moyo wake haukuwa na amani kabisa kutokana na fitna alizomfanyia Rashid.

Hata hivyo, kikubwa zaidi kwake ilikuwa ni Deo kukubali kwenda nyumbani kwao na baadaye alitamani sana Deo mpenzi wake wa maisha yake yote. Hiyo ndiyo ilikuwa ndoto yake kubwa. Akiwa katika lindi la mawazo, akaamua kumpigia simu Deo.
Je, nini kitaendelea? Endelea kuisoma...

LEVINA aliumia sana ndani ya moyo wake, akaona ni vyema kama angenyanyua simu yake na kumpigia Deo. Alitaka kujua hisia zake zina nini juu yake. Hakutaka kufanya mambo kwa hasara!

Akachukua simu na kwenda moja kwa moja kwenye Menu, akabonyeza Contacts kisha akaanza kutafuta jina la Deo, alipolipata akabonyeza kwenye kitufe cha kijani ili kuruhusu upigwaji simu.

Punde tu, sauti ya Deo ikasikika...
“Vipi Levina mbona usiku sana?”
“Nina matatizo Deo!”
“Matatizo gani?”
“Naomba nikuulize kwanza maswali yangu!”

“Uliza.”
“Mimi ni rafiki yako?”
“Ndiyo!”
“Unaniamini?”
“Ndiyo!”

“Unanipenda?” Levina akauliza kwa sauti ya taratibu, lakini iliyochanganyikana na kilio cha kwikwi kwa mbali.
Deo hakupata shida sana kugundua kwamba Levina alikuwa analia. Pengine hilo si neno sana, lakini kwanini amemuuliza kama anampenda? Hata kama anampenda, ndiyo alie?
Kwanini analia?

Hakujua!
Kimya cha muda mfupi kikapita, Deo akiwa ametulia kwenye simu na Levina akiendeleza kilio chake cha chini chini huku kwikwi zikisikika kwa mbali.
“Levina,” baadaye Deo akaita.
“Bee!”
“Nini tatizo?”

“Si tatizo, napenda kusikia ukinijibu!”
“Uliuliza nini?”
“Nilikuuliza kama unanipenda?”
“Ni kweli nakupenda Levina, wewe ni rafiki yangu na umekuwa msaada kwangu kwa kila kitu, lazima nieleze ukweli, nakupenda, kwani wewe hunipendi?”
“Swali gani hilo Deo?”

“Samahani kama nimekuudhi, lakini ndani ya moyo wangu natambua kwamba tunapendana, mimi nafahamu hilo, naamini hata wewe ni kama mimi.”
“Kweli.”
“Lakini ni kwanini unalia?”
“Silii ila sauti yangu leo haipo vizuri sana.”
“Unakohoa?”

“Ndiyo!”
“Pole sana.”
“Ahsante.”
“Nina swali lingine kwako Deo!”
“Uliza.”

“Lakini kabla sijauliza, nataka unihakikishie kwamba utajibu ukweli wako wote na hutanidanganya jambo lolote.”
“Hilo kabla hujauliza, naamini unatambua kabisa jinsi nilivyo mkweli.”
“Umewahi kuona mtu akilia?”

“Mara nyingi sana, hata leo kuna mtoto nimemuona akilia.”
“Siyo mtoto, nazungumzia mtu mzima.”
“Ndiyo, kwenye misiba huwa wanalia sana, nimeshaona mara nyingi, kwani kuna nini, mbona unaniacha na maswali?”
“Lakini vipi kama ukiona mtu mzima analia?”
“Nitajisikia vibaya sana.”

“Umeshawahi kumuona mtu akilia kwa ajili yako?”
“Hapana.”
“Utapenda siku moja hilo likitokea?”
“Hapana.”
“Basi usiku mwema.”

“Kwanini?”
“Nimekutakia usiku mwema Deo.”
“Lakini sijakuelewa kabisa. Mbona leo maneno yako yamekuwa magumu sana kuingia kichwani mwangu? Kwani kuna nini kimetokea?”
“Hakuna...nilitaka kujua tu unachowaza kichwani mwako!”
“Nikuambie kitu Levina?”

“Nakusikiliza.”
“Nitalala nikiwa na mawazo sana leo. Maneno yako yananiacha na maswali mengi yasiyo na majibu kabisa. Mpaka sasa sijajua maana ya kauli yako.”
“Siku moja utajua....”
“Usiku mwema.”

“Na wewe pia!”
Wakakata simu zao.
Deo akapata wakati mgumu sana wa kuwaza mambo kichwani mwake bila kupata majibu. Alikuwa katika wakati mgumu sana wa kujaribu kuwaza kilicho kichwani mwa Levina kitu ambacho kwa hakika kisingekuwa rahisi kuelewa.

“Sijajua anamaanisha nini? Anyway itajulikana baadaye!” Akawaza na kujifunika shuka kisha akaishilia usingizini.

****
Siku nzima ilikuwa kama wiki kwa Levina, kichwa kilikuwa kinamuuma mawazo mengi yakimsumbua. Hakuwa na kitu kingine kilichomtesa zaidi ya Deo, aliendelea kuwaza namna ya kumsogeza karibu yake.

“Nampenda sana Deo, ni kweli kwamba nampenda sana, lazima nitumie kila njia, nihakikishe anakuwa wangu. Hilo lazima nitalifanya,” akawaza Levina akiwa kazini kwake Posta.

Levina baada ya kumaliza kidato cha sita, wazazi wake walimkabidhi moja ya maduka yao yaliyopo mjini, Levina alipewa duka la simu lililopo Posta Mpya jijini Dar es Salaam.
Alichojua yeye ni kwamba alikuwa msimamizi wa duka lile kubwa, lakini wazazi wake walipanga kumwachia moja kwa moja kama lake. Walimfanya msimamizi mkuu, akishughulikia kila kitu, mpaka mishahara ya wafanyakazi, walichokifanya wao ni kukagua mahesabu ya fedha zinazoingia na kutoka benki.

Mali ikipungua dukani, ilikuwa ni kazi ya Levina kuagiza au kwenda nje ya nchi kununua mzigo mwingine wa dukani.
Akionekana mwenye mawazo tele kichwani mwake, simu yake ikatoa mlio wa ujumbe mfupi wa maneno, mara moja akaufungua na kusoma.

Ilikuwa meseji kutoka kwa mama yake, alijikuta anarudia kusoma zaidi ya mara mbili ile meseji akiwa haamini kabisa alichokiona.
Ujumbe ule ulisomeka; “Levina ni wiki moja sasa tangu Rashid ameondoka, hatuna house boy, sasa kama unaweza ni vizuri ukashughulikia hilo, tukapata mtu mwingine haraka.”
Levina akatabasamu.

Ilikuwa nafasi nzuri kwake ya kumwingiza Deo nyumbani kwao.
“Yes, mambo yanakwenda kama nilivyopanga, afadhali,” akasema kwa sauti ya taratibu akiachia tabasamu.

***
Jioni Levina aliwahi sana kurudi nyumbani, akamkuta mama yake sebuleni, baada ya kumsalimia akamwambia...
“Mama nilipata sms yako ya mchana, nimeanza kuifanyia kazi, ndani ya siku tatu tutapata mtu mwingine.”

“Oh! Usijali binti yangu, ameshapatikana kijana mwingine kutoka Bagamoyo, atakuja kuanza kazi kesho.”
Uso wa Levina ukasawagika kwa huzuni.

Itaendelea,..........
 
Jioni Levina aliwahi sana kurudi nyumbani, akamkuta mama yake sebuleni, baada ya kumsalimia akamwambia...
“Mama nilipata sms yako ya mchana, nimeanza kuifanyia kazi, ndani ya siku tatu tutapata mtu mwingine.”

“Oh! Usijali binti yangu, ameshapatikana kijana mwingine kutoka Bagamoyo, atakuja kuanza kazi kesho.”
Uso wa Levina ukasawagika kwa huzuni.
Sasa endelea...

KWA sekunde kumi na tano, Levina alikuwa ameganda akimwangalia mama yake, ni kama hakusikia vyema maneno yale, hata kama aliyasikia vizuri lakini yalionekana kuwa magumu sana kupenyeza kwenye ngoma za masikio yake.

Anamwangalia mama yake kwa macho yanayozungumza jambo fulani, ingawa haijulikani moja kwa moja kuwa anazungumza nini. Mama yake aliweza kugundua tofauti aliyonayo mwanaye haraka sana.

“Vipi Levina mwanangu, mbona kama hujafurahia?”
“Siyo hivyo mama?”
“Bali nini tena?”
“Nimeshangaa, maana tayari nilishaanza taratibu za kumpata huyo mtu.”

“Kwani umeshampata?”
“Kuna dada mmoja ameniambia kwamba jioni ya leo atakwenda kuzungumza naye. Yupo kaka mmoja amesema anaishi Mburahati, kwahiyo akionana naye atajaribu kumweleza.”
“Ni mfanyakazi au yupo tu, nyumbani?”

“Anafanya kazi!”
“Sasa atawezaje kutoka?”
“Kasema atamshawishi, maana hata pale halipwi mshahara mkubwa, lakini pia atamwambia mazingira ya kazi ni mazuri.”
“Sawa, ngoja tuone.”

“Na huyo mwingine uliyesema?”
“Huyo kila kitu kipo tayari, nimeshafanya naye mawasiliano na tumekubaliana aje kesho!”
“Sasa itakuwaje? Maana sitaki kuonekana mwongo kwa rafiki yangu.”

“Kesho tutapata majibu kamili, kama akija huyo wa Bagamoyo sawa, asipokuja basi utanijulisha makubaliano ya huyo kijana mwingine atakayezungumza na rafiki yako leo usiku.”
“Sawa mama, mimi nipo ndani,” akasema Levina.
“Sawa mama.”

Levina akajikongoja mpaka ndani akionekana kuwa na uchangamfu kidogo, bado alikuwa akiomba sana huyo kijana wa Bagamoyo asitokee ili Deo apate nafasi ya kuingia kwao.
“Itawezekana tu, maadamu moyo wangu umempenda, naamini itakuwa hivyo,” akawaza Levina.

Baada ya kubadili nguo, aliingia bafuni kuoga, alipotoka alionekana kuwa na nguvu kidogo, akachukua simu na kumpigia Deo.
“Uko wapi?”
“Nipo njiani naelekea nyumbani.”

“Umefika wapi sasa hivi?”
“Ndiyo nakaribia kushuka Mwembechai!”
“Ok! ukishuka naomba unisubiri!”
“Kwani wewe uko wapi?”
“Nipo home, lakini natoka sasa hivi nachukua taxi nakuja.”

“Basi jitahidi ufanye haraka!”
“Usijali, sina muda mrefu sana nitakuwa hapo.”
“Poa.”
Levina akabadili nguo haraka na kutoka. Alipopita sebuleni alimkuta mama yake akiwa amekaa pale pale!

“Haya wapi tena?”
“Natoka kidogo mama!”
“Ila saa hizi ni usiku na baba yako hapendi kabisa utoke usiku.”
“Mama siendi mbali, nakwenda hapo Mwembechai mara moja.”
“Unatoka na gari?”

“Hapana, sitaki baba ajue nimeenda mbali kama akirudi mapema, ni bora alione gari atajua nipo jirani!”
“Kumbe hutakuwa jirani siyo?”
“Mama...!!! Mwembechai si mbali, lakini ni mbali pia mama. Kwa baba kule ni mbali!”

Mama Levina akacheka.
“Uwahi kurudi,” akasema mama Levina akiendelea kutabasamu.
“Nakuahidi mama.”
Levina akaondoka zake.

***
Levina alifurahi sana kukutana na Deo, moyo wake ulikuwa ukisisimka sana kila alipokutanisha macho yake na Deogratius.
Alikuwa mwanaume pekee ambaye aliweza kuutetemesha moyo wake.
“Nina habari njema Deo!”
“Juu ya nini?”

“Unakumbuka mara ya mwisho nilizungumza nini na wewe?”
“Ndiyo, nakumbuka vizuri sana.”
“Ilikuwa ni nini?”
“Kuhusu kazi nyingine!”
“Halafu?”
“Kusoma.”

“Safi sana, kumbe unakumbuka vizuri sana, sasa tunaanza na kimoja baada ya kingine. Kama nilivyokuambia sisi ni marafiki na nitakuwa tayari kutumia kila njia nihakikishe nakufurahisha!”
”Nimefurahi kusikia hivyo.”
“Nimekupatia kazi, tena nyumbani kwetu kabisa.”

“Unasema kweli?” Deo akauliza akiwa haamini kabisa alichoambiwa na Levina.
“Kwanini isiwe kweli?” Levina akauliza akitabasamu.

Tabasamu lililomchoma Deo moyoni, kwa mara ya kwanza alikiri kumuona Levina akiwa ameachia tabasamu zuri zaidi kuliko siku zote!
Uzuri wa Levina ukawa hadharani!
Je, nini kitaendelea......
 
Pamoja na taarifa kutoka kwa mama yake kwamba alishapata kijana mwingine wa kazi, bado Levina hakukata tamaa kuhusu Deo. Usiku ule ule akatoka na kwenda kukutana naye Mwembechai.

Levina akamweleza kwamba amempatia kazi nyumbani kwao, Deo akafurahi sana. Furaha iliyosababisha Levina aachie tabasamu mwanana! Uzuri wake ukawa hadharani!
Nini kitatokea? Endelea kuisoma...

DEOGRATIUS akagundua kitu kipya kabisa kutoka kwa Levina, aligundua kwamba alikuwa msichana mzuri kupindukia! Tabasamu lake lililoacha sehemu kubwa ya meno yake nje, lilisababisha aone vijishimo vidogo mashavuni mwake na hivyo kuzidisha urembo wake.

Alihisi moyo wake kama umepigwa na shoti ya umeme, alikuwa amesimama mbele ya mwanamke mrembo sana tofauti na matarajio yake. Levina alikuwa mzuri zaidi ya alivyofikiria.
Kwanini anamsaidia sana?

Kwanini anakuwa naye karibu sana? Hayo yaliendelea kuwa maswali ambayo hayakuwa na majibu ya moja kwa moja kichwani mwake. Alibaki ameganda akimwangalia Levina ambaye sasa aliamua kucheka kabisa. Furaha ya Levina ilikuwa ni kuona jinsi Deo anavyomkubali yeye.

Hakujali umasikini wake, alichojua yeye ni mapenzi tu. Moyo wake ulianguka kwake, alitamani sana awe mpenzi wake wa dhati ndani ya moyo wake.

“Deo!” Levina akaita kwa sauti tamu sana.
“Naam!”
“Vipi?”
“Poa.”

Levina akacheka.
“Mbona unanicheka?”
“Sijakucheka Deo!”
“Bali!”

“Nimecheka. Unajua kuna tofauti kubwa sana kati ya kucheka na kumcheka mtu. Mimi nimecheka, sijakucheka. Umeona tofauti hiyo?”
“Haya mama wa Kiswahili, siwezi kushindana na wewe, hapo umenishinda.”
“Enhee stori nyingine?”

“Sina!”
“Basi poa, acha mimi nirudi zangu home, si unajua tena dingi hajaingia, sasa akija na kunikuta sijafika nyumbani mpaka saa hizi haitakuwa sawa!”

“Sawa basi. Enhee niambie, naanza lini kazi?”
“Una hamu eeh!”

“Sasa kumbe ningefanyaje?”
“Subiri kidogo, mpaka kesho nitakupa jibu kamili la lini utaanza kazi rasmi.”

“Sawa.”
“Usiku mwema.”
“Nawe pia!”

Deo akaondoka, Levina akaendelea kumkazia macho mpaka alipoondoka. Baada ya hapo akavuka upande wa pili, akachukua taxi nyingine na kurudi zake nyumbani. Kwa bahati nzuri, baba yake alikuwa bado hajafika nyumbani.
“Una bahati, baba yako hajafika!”

“Acha tu mama!”
“Enhee vipi, mambo yanaendaje?”
“Huyo kijana yupo mama, hata kesho anaweza kuja!”

“Sawa basi, lakini naomba tusubiri hadi kesho, kama yule wa Bagamoyo hatakuja basi atakuja huyo, unajua tayari nilishamuahidi na huyo mtu alimuhangaikia sana!”
“Sawa mama,” Levina akasema kwa sauti ya chini lakini ndani ya moyo wake akiumia sana.

Alitamani sana huyo kijana asitokee ili Deo wake aweze kwenda nyumbani kwao. Hiyo ilikuwa dua yake kubwa.
“Mimi naingia chumbani mama.”

“Sawa, bado nipo hapa naendelea kuangalia taarifa ya habari.”
Muda mfupi baada ya Levina kuingia chumbani kwake, simu ya Mama yake ikaita. Namba hakuzijua, lakini mara moja akapokea!
“Nani mwenzangu?” Ndiyo neno la kwanza mama Levina kutamka mara baada ya kupokea simu.

“Mama Happy wa Bagamoyo...samahani mama Levina, nimekupigia na namba ya kibandani, simu yangu haina chaji!”
“Usijali, vipi za huko?”
“Bwana wangu, si salama.”

“Kuna nini tena?”
“Yule kijana amefiwa na mama yake, kwahiyo anatakiwa kwenda kwao Morogoro kesho, kurudi ni baada ya wiki mbili!”
“Duh!”

“Ndiyo mwenzangu, matatizo yamemfika kijana wa watu, kwa jinsi alivyokuwa na hamu na hiyo kazi, yaani amechanganyikiwa kabisa!”
“Poleni mwaya, umpe pole na yeye, hakuna jinsi, maana nilikuwa na shida ya haraka sana na kijana wa kazi, sasa nalazimika kutafuta mwingine.”

“Hakuna shida, haikuwa riziki yake!”
Wakakata simu zao. Muda ule ule mama Levina akamwita binti yake, ambaye alifika baada ya muda mfupi sana.

“Levina nimepigiwa simu na Happy sasa hivi, yule kijana amepatwa na matatizo. Amefiwa na mama yake, kwahiyo hataweza tena kuja labda mpaka baada ya wiki mbili, nimemwambia mama Happy kwakuwa nina haraka, nalazimika kutafuta mwingine kwahiyo basi zungumza na huyo rafiki yako, yule kijana aje kesho aanze kazi mara moja!”

“Sawa,” Levina akajibu kwa sauti ya chini sana, akionekana kuwa na huzuni lakini ndani ya moyo wake alikuwa akishangilia kwamba Deo wake alikuwa anakwenda kuwa karibu naye.

****
Levina alivyoingia tu chumbani kwake, kitu cha kwanza ilikuwa kuchukua simu yake na kumpigia Deo haraka sana.
“Vipi?”

“Habari njema zaidi ya zile za saa ile!”
“Zipi tena Levina?”
“Unatakiwa kuanza kazi kesho, vipi utaweza?”
“Nitaweza!”
“Kweli?”

“Kweli kabisa.”
“Basi fanya juu chini, kesho tukutane saa 3:00 asubuhi!”
“Sawa.”
Wakaagana.

****
Kama walivyokubaliana, siku iliyofuata walikutana Mwembechai, Deo akiwa na begi lake, tayari alikuwa ameshaacha kazi alipokuwa akifanya mwanzoni na akawa tayari kwenda kuanza kazi kwa akina Levina.

Wakaingia sebuleni na kukutana na mama yake Levina akiwa anamsubiria kwa hamu...

“Karibu mwanangu!” Mama Levina akamwambia Deo.
“Ahsante mama!”
“Jisikie uko nyumbani!”

“Ahsante mama.”
“Nina imani maelekezo yote umeshapewa na Levina, kama bado atakupa. Acha mimi niwahi kazini, nawatakieni siku njema,” akasema mama Levina akisimama na kupiga hatua za kuondoka.

“Ahsante!” Deo akajibu akiona haya.
Mama Levina akaondoka zake, akawaacha Deo na Levina tu nyumbani. Levina aliposikia muungurumo wa gari la mama yake nje, akajua tayari ameshaondoka. Akamkazia macho Deo, aliyekuwa amesimama kama mlingoti!

Mara ghafla akamsogelea na kumkumbatia kwa nguvu! Kilikuwa kitendo cha haraka na ghafla sana, kilichomshtua sana Deo. Akabaki ameduwaa akimwangalia bila majibu!
Je, nini kitatokea? Usikose kufuatilia
 
Levina anafanikiwa kumsogeza Deo karibu yake, baada ya kumtafutia kazi ndani mwao. Nini kitaendelea? Songa nayo...

Levina alimshangaa Deo kwa kutoonesha furaha kwa kupata kazi.
“Jamani Deo mbona huoneshi furaha?”
“Levina mbona nipo happy.”
“Muongo, au hukupenda kuja kufanya kazi hizi?”
“Kwa nini nisipende.”

“Basi Deo nakwambia achana na mshahara utakao lipwa nitahakikisha nakuongezea pesa zaidi ya mshahara wako.”
“Nitashukuru Levina.”
“Basi twende nikakuoneshe chumba chako.”

Levina alichukua begi la Deo na kumpeleka kwenye banda la uani kulikokuwa na chumba kimoja. Baada ya kuingia chumbani alitoka na kurudi na ufagio na shuka za kumtandikia. Deo alishangaa mtoto wa tajiri yake kumuhangaikia vile, baada ya usafi wa chumba alimtandikia kisha alimkaribisha.

“Deo karibu hiki ndicho chumba chako.”
“Asante.”
“Vipi umekipenda?’
”Nimekipenda.”

Baada ya kumuonesha kile chumba alimuelekeza kazi zote alizotakiwa kuzifanya kisha alimuacha aendelee na majuku ya siku ile. Levina alirudi hadi sebuleni kutaka kujiandaa kwenda mjini kwenye duka.

Lakini roho haikumpa alisogea hadi dirishani kumtazama Deo aliyekuwa katika vazi la bukta na singland, alijikuta akitabasamu mwenyewe jinsi moyo wake ulivyofurahi kuwa na Deo mwanaume aliyeutesa moyo wake.

Kuwa mbali na Deo aliona kama kuinyima uhuru nafsi yake, aliamini muda ule ambao wazazi wake hawapo ni muda mzuri wa kujisogeza karibu na Deo. Alitoka hadi uani ambako Deo alikuwa ameanza kazi ya kupunguza majani, alisogea karibu yake huku kidole kikiwa mdomoni kujipa ujasiri.

“Deo,” alimwita huku akiachia tabasamu pana.
“Levina si umesema unawahi kazini?”
“Ndiyo Deo lakini bado nina muda, Deo,” Levina alimwita Deo huku akimtoa majani kichwani.
“Unasemaje Levina?”
“Kazi unaionaje?”

”Ndiyo naianza lakini siyo mbaya.”
“Leo kuna kitu nataka kukueleza.”
“Kipi hicho?” Deo aliuliza bila kumuangalia.
“Deo acha kwanza kukata majani nisikilize.”

“Levina hii ndiyo kazi iliyonileta acha niifanye, we wahi kazini jioni tutazungumza nitakuwa nimepunguza kazi si unajua leo ndiyo siku ya kwanza nitaonesha picha mbaya.”
“Deo ufanye kazi usifanye kazi mimi ndiye mwenye mamlaka, na kukuleta hapa si kufanya kazi hii.”

“Si kazi hii, kwa kazi gani?”
“Ili uwe karibu na mimi”.
“Kivipi?”
“Deo lazima usome alama za nyakati kila ninachokifanya lazima ujiulize kina maana gani.”

“Levina mimi na wewe tumefahamiana kitambo umekuwa msichana ambaye umeonesha kunijali, nimekuwa nikivunia upendo wako na kujikuta nikikosa cha kukulipa.”
“Deo cha kunipa unacho hakihitaji pesa wala nguvu.”
“Kipi hicho?”

“Deo lazima leo nikueleze ukweli...na..na..ku...,” Levina hakumalizia aliweka kidole mdomoni huku mkono ukitetemeka baada ya kupoteza ujasiri wa kulitamka neno toka moyoni mwake.
“Levina unasemaa!”

Levina aliona aibu na kukimbilia ndani huku akimwacha Deo akijiuliza maswali yasiyo na majibu, alijiuliza Levina alimaanisha anampenda. Kama ni kweli ulikuwa mtihani ambao aliamini kabisa mapenzi ni kikohozi kamwe wasingeyaficha. Kwa muonekano wa haraka ilionekana familia yake ilikuwa ikimpenda sana na kumjali.

Aliamini kama wazazi wake wakigundua lazima wangemfukuza kazi, alijua lazima atataabika kutokana na kuacha kazi iliyokuwa ikimuingizia riziki. Pia alikuwa na mtihani mwingine kama atamkatalia Levina lazima atamfukuzisha kazi, lakini hakutaka kuingilia sana mawazo ya Levina.

Levina alikimbia hadi chumbani kwake na kuanza kulia kutokana na kukosa ujasiri kuwasilisha uju mbe wake. Alichukua kitambaa cha mkononi na kufuta machozi. Mara simu ya mama yake iliingia, aliipokea na kuzungumza.
“Haloo Mamy.”

“Levina upo wapi?” Alimuuliza kwa ukali kidogo.
“Mbona hivyo mama?”
“Hujanijibu upo wapi?”
“Mamy nipo njiani nakwenda mjini.”

“Jitahidi uwahi kuna mteja wa jana mlikubaliana afuate simu dukani amefika muda, bado duka halijafunguliwa.”
“Namjulisha sasa hivi.”

Alikata simu na kukimbia bafuni kuoga kisha alibadili nguo haraka haraka kuwahi dukani, alitoka hadi uani alipokuwa Deo akikata majani alitembea kwa mwendo wa kunyata alipomkaribia alimgusa begani, Deo alipogeuka alikutana na busu la mdomoni.
“Deo bai, nawahi kazini kazi njema.”
“Na wewe pia.”

Levina alitembea kwa haraka kuelekea kwenye gari lake ili awahi kwenye mihangaiko yake. Nyuma alimuacha Deo na maswali mengi juu ya vitendo vya kimahaba vya Levina, Levina alibadilika kwa muda mfupi hakuwa yule mpole na mnyenyekevu muda wote, alikuwa ni mtu aliyeonekana kuchizika kimahaba.

Kauli ya Levina ilimfumbulia fumbo zito moyoni mwake la muda mrefu la huduma zote zilizoelekezwa kwake na Levina haikuwa bure na ukweli wake ulikuwa umedhihirika muda mfupi uliopita. Deo alicheka na kuendelea kupunguza majani huku umbile la Levina msichana mrembo tena anayetoka katika familia tajiri lilitawala katika ubongo wake.

Nini Kitaendelea?
 
ILIPOISHIA:
Kauli ya Levina ilimfumbulia fumbo zito moyoni mwake la muda mrefu la huduma zote zilizoelekezwa kwake na Levina haikuwa bure na ukweli wake ulikuwa umedhihirika muda mfupi uliopita. Deo alicheka na kuendelea kupunguza majani huku umbile la Levina msichana mrembo tena anayetoka katika familia tajiri likiwa limetawala katika ubongo wake.
SASA ENDELEA...

Mbinu za Levina kumuingiza ndani ya jumba lao lilimfanya Deo acheke peke yake kwa kicheko cha chini chini huku akitikisa kichwa, kama alikuwa akizungumza na mtu alisema kwa sauti ya chini.

“Kweli Levina kiboko, mbinu zake mwenyewe sina hamu.”
Baada ya kumaliza kukata majani aliyakusanya na kuyapeleka kwenye shimo la takataka lililokuwa nyuma ya banda la ng’ombe.
***
Levina akiwa ndani ya gari lake akielekea kwenye duka lao la simu, macho yake yalikuwa yametazama mbele huku akikanyaga mafuta taratibu kutokana na foleni ya jijini. Pembeni ya barabara alimuona mvulana mmoja na msichana wakitaniana katika hali ya mapenzi.

Aliwakazia macho mpaka alipowapita, alitabasamu na kuchukua simu yake iliyokuwa kwenye dash boad na kuifungua upande wa picha. Aliifungua na kuijaza picha ya Deo kwenye kioo cha simu, picha ambayo alipiga kwa siri bila yeye kujijua.

Aliibusu simu na kusema kwa sauti ya chini.
“Lazima Deo atanielewa si mtoto mdogo.”
Kutokana na foleni ya barabarani kila gari liliposimama aliiangalia picha ya Deo na kutabasamu. Aliikumbatia simu kifuani katika mahaba mazito na kufumba macho huku akisindikizwa na muziki mtamu wa kizazi kipya wa Suma Usemao Mapenzi ni sumu.

Alirudia maneno ya kiitikio kimoyomoyo, kumbe wakati huo foleni ilikuwa imeshasogea lakini Levina alikuwa amejisahau na mahaba mazito ya picha ya Deo kwenye simu yake. Hata kelele za honi hakuzisikia kutokana na kujifungia ndani ya gari huku akipulizwa na kiyoyozi. Sauti ya kugongwa dirisha ndiyo iliyomshtua alipofumbua macho aligundua foleni imefika mbele ambapo alibadili gia na kukanyaga mafuta akiwaacha watu wakimsindikiza na matusi mazito ya nguoni lakini hakuyasikia.

Hata alipofika dukani muda wateja walipopungua alitumia muda huo kuzungumza na Deo huku akimpigia simu mfanyakazi wa ndani ampatie Deo chakula kizuri na kila kitu ambacho baba yake alikitumia wakati wa chakula. Kingine alimuonya mfanyakazi wa ndani kuwa mbali na Deo bila kufanya utani wowote.

“Haloo Deo.”
“Ooh, Levina za kazi?”
“Zimezidi kuwa nzuri baada ya kusikia sauti yako.”
“Nashukuru kusikia hivyo.”

“Vipi unafanya nini sasa hivi?”
“Mmh, nimepumzika ndiyo nimemaliza kula.”
“Umekula nini Deo?”
“Chakula.”

“Chakula gani?”
“Ndizi na nyama.”
“Matunda je?”
“Nimepata.”

“Juisi?”
“Nimepata.”
“Umeshiba?”
“Nimeshiba.”

“Muongo, usione aibu wewe kwa sasa ni zaidi ya baba yangu mzazi.”
“Kivipi?”
“Umekuwa mtu muhimu sana maishani mwangu, kuwa nawe karibu nimefarijika. Nilijihisi ufahari siku uliyonikubalia kuja kufanya kazi kwetu.”

“Mh!”
“Usigune Deo, lazima niseme ukweli, Deo nakupenda sana.”
Maneno yale yalimfanya Deo anyamaze kwa muda kitu kilichomnyima raha Levina na kuona mbegu yake huenda hakuipanda muda muafaka. Lakini kwa upande mwingine alijiona yupo sawa kutokana na moyo wa kupenda ulivyo.

Siku zote macho yakiona moyo unapenda na moyo ukipenda subira hakuna tena na subira ikitoweka aibu hukimbia. Aliamini mchuzi wa mbwa ulitakiwa kunywewa ungali moto.

Hakujutia kauli yake kumueleza ukweli Deo kuwa anampenda, ulikuwa ujumbe sahihi toka moyoni mwake ambao aliamini kupitia njia ya simu kidogo ujasiri ulikuwepo. Lakini kimya cha Deo kilimfanya akose raha moyoni kwake aliamini kama Deo hataafiki ombi lake lilikuwa sawa na kutwanga maji kwenye kinu.

“Deo,” Levina alimwita baada ya kupita ukimya mfupi.
“Levina.”
“Mbona hunijibu, kujivua nguo mbele yako si umalaya Deo, usinihukumu kwa jinsia yangu bali kwa upendo wangu mzito moyoni mwangu. Deo sikuwa na njia yoyote ya kukueleza kuwa nakupenda, naomba uheshimu hisia zangu.”
“Levina,” Deo alimwita Levina kisha alishusha pumzi nzito.

“Deo,” Levina aliitikia upande wa pili na sauti yenye dalili za kilio.
“Levina naogopa sana mimi kuwa sehemu ya matatizo yako katika furaha zako za kila siku.”
“Deo kunikubalia ni kuniingiza kwenye matatizo?”

“Sina maana hiyo!”
“Muongo Deo, unataka kuongopa nini?”
“Levina wewe ni mtu muhimu sana kwangu, nilikuwa na maana kutokana na kujitoa kwangu na mimi kuniona ni sehemu ya furaha yako. Nami najitoa kwako kwa nguvu zote ili kukuhakikishia zile raha ulizokuwa ukizitafuta kwangu unazipata.”
“Kweli Deo?”

“Siwezi kukudanganya.”
“Waooo, I can’t beleave my dear, Thanks God thanks Deo I love you soooo much.”
Levina alishangilia kukubaliwa ombi lake na kujisahau kama yupo dukani na kuwashangaza wateja waliokuwa dukani wakisubiri amalize kuzungumza kwa simu.
Nini kitaendelea?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom