Hadithi: Tatoo, ajichora mchoro mwilini akiona cha moto

Hadithi: Tatoo, ajichora mchoro mwilini akiona cha moto

X_INTELLIGENCE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2014
Posts
10,700
Reaction score
14,769
kuna msichana mmoja anaitwa Valentina alimpenda sana kijana mmoja anaeitwa mshana jr mahusiano yao yalidumu kwa muda mrefu sana na kila mtu alipenda sana kuwaona mshana jr na Valentina jinsi wanavyopendana mithiri ya watoto mapacha.

mshana jr alikuwa anapenda sana kufuga njiwa hivyo mara nyingi alipenda sana kuwahudumia njiwa wake ambao alikuwa anajitahidi awapatie vyakula mbali mbali kama mchele, mtama, punje za mahindi n.k.

Lyme-Regis-pigeon-pair-April-2015-1-600-px-tiny-June-2015-Darren-Naish-Tetrapod-Zoology.jpg


kutokana na mapenzi mazito aliyo nayo Valentina kwa mshana jr , Valentina aliamua kumfuata sunola ambaye alikuwa mchoraji tatoo {michoro ya kwenye mwili}. Valentina alimwambia sunola amchore mchoro mzuri wa njiwa begani mwake,

sunola hakuwa na hiyana alichokuwa anaitaji yeye ni fedha tu. walipatana kisha sunola akamwambia Valentina kuwa tatoo hii ninayo kuchora haitafutika nitakuchora vizuri sana. Valentina hakuwa na hiyana kwani aliamua kufanya hivyo ili kumuonyesha mshana jr kuwa anampenda sana.

flying-pigeon-tattoo-on-left-back-shoulder.jpg


Valentina alipatwa na maumivu makali sana pindi alipokuwa anachorwa uo mchoro adi alijuta kwa uamuzi huo lakini hakuwa na jinsi kwani maji alisha yavulia nguo hivyo ilikuwa budi yake kuyaoga. mchoro ulipendeza sana na akaona fahari sana kuwa na ule mchoro mwilini mwake. kipindi chote hicho Valentina alikuwa ameliza chuo hivyo alikuwa katika harakati za hapa na pale kutafuta ajira,

siku moja Valentina alikutana na Papushikashi ambaye walimaliza wote chuo Papushikashi akamwambia Valentina kuwa kuna nafasi za jeshi zimetoka na watu wenye sifa kama zao wanahitajika. Valentina alipenda sana kazi ya jeshi hivyo alijiandaa kwenda kufanya usahili.

siku ya usahili ilipofika Valentina aliwakuta Th Name ambaye alikuwa mgambo mkuu, na xavia jr pamoja na Kilemachocho ambao walikuwa ni maafisa wa jeshi kutoka makao makuu. watu wengi waliohudhuria usahili ule walipoteza kigezo kutokana na elimu yao kuwa ndogo lakini Valentina na Papushikashi walishinda kuendelea na usahili ambapo atua iliyofuata ilikuwa ni kupimwa afya ili waende wakasajiliwe kuanza rasmi mafunzo ya kijeshi.

flying-pigeon-tattoo-on-left-back-shoulder.jpg


TATOO YAWA KIKWAZO
baada ya vipimo vya afya vya Valentina kuwa safi aliamliwa Nifah amfanyie ukaguzi wa mwili kuona kama anazo alama zozote mwilini. bahati ikawa mbaya kwa Valentina baada ya ile tatoo kuonekana, Nifah akamwambia Valentina kuwa tatoo ni miongoni mwa vitu ambavyo mwanajeshi hatakiwi kuwa navyo hivyo Valentina huo ukawa ndio mwisho wa kukosa ajira ndani ya jeshi.

Valentina alirudi nyumbani akiwa na hasira sana alitamani iyo tatoo aifute lakini ikawa haiwezekani. ilibidi amtafute mpenzi wake mshana jr ili angalau aende akapunguze mawazo walikutana wakumbatiana kisha mshana jr akauvunja ukimya kwa kumwambia Valentina kuwa amepata safari kwenda USA kusoma.

Valentina alichanganyikiwa maradufu maana faraja pekee iliyokuwa imebaki kumfariji ni mshana jr, naye mshana jr alipata safara muhimu ya masomo, walihaidiana mengi ikiwa ni pamoja kuwa mara mshana jr atakaporejea wataoana.

PrecisionAir-656x351.jpg


MADHARA YA TATOO YAANZA KUONEKANA
siku ya safari ilipowadia ilikuwa ya huzuni kwa wote mshana jr na Valentina. waliagana kisha mshana jr akapanda ndege kuelekea masomoni. Valentina alikubari matokeo lakini ghafra kwenye mdomo wa ile tatoo ya njiwa pakatokea kipere cha kawaida.

Valentina akakitumbua kile kipere lakini kadri siku zilivyokuwa zinaenda mara kile kipere kikawa kidonda, kidonda kilikuwa kikubwa kukiziba kichwa cha yule njiwa Valentina alipata maumivu sana alitumiwa dawa mbali mbali za vidonda lakini hakupata nafuu kabisa wazo la kuifuta ile tatoo likamjia.

akakutana na Gobe ambaye alimwambia Valentina kuwa ata yeye Gobe alikuwa na tatoo kama hiyo ila aliifuta kwa kutumia asidi furani ivi. Gobe alimletea Valentina hiyo asidi ili apake tatoo hiyo iondoke kabisa. Valentina alipaka hiyo asidi kwenye tatoo alipata maumivu makari sana alishindwa kuvumilia machozi yalianza kumtiririka kwenye mashavu yake laini ya kirembo. alilia sana.

zombie_shoulder_wound_by_nighteffects07-d6qkmii.jpg


HATIMAE Valentina APATA KANSA
matokeo ya ile tatoo ya njiwa yalikuwa mabaya sana kwa Valentina kwani alipata kidonda kikubwa sana alipoenda hospitali wakamwambia amepata kansa hadi leo bado Valentina anauguza kidonda chake ambacho ajui kitapona lini......... itaendeleaaaaaa ......

{ndugu zangu tuache tabia ya kuiga mambo, kuna vitu ni bora kuviacha vipite madhara ya tatoo ni makubwa sana acha kujichora michoro ya ajabu ajabu. story hii aihusiani na maisha harisi na watu wenye majina yaliyotumika humu, vile vile naomba mniwie radhi sana kwa kutumia majina yenu bila ridhaa yenu sijatumia ili niwachafue bali nilikuwa naiasa jamii.}
 
Somo zuri sana natunai wadau watakuwa wamekuelewa na kujifunza!
Maana siku hizi wanaume wanachora tatoo mpaka usoni wawe Kama lil wyne,wanawake huko kwenye viuno n'a makalio ndy usiseme....
Amazing-Tattoo-Ideas-for-Men.jpg

kama hiyo ebu angalia hii si laana hii
 
enh ni alama kubwa sana na mwanzo wake ni vikundi vya kijasusi. na ndio maana wanausalama wote hawaruhusiwi kujiweka alama kama hizo mwilini
 
enh ni alama kubwa sana na mwanzo wake ni vikundi vya kijasusi. na ndio maana wanausalama wote hawaruhusiwi kujiweka alama kama hizo mwilini
 
enh ni alama kubwa sana na mwanzo wake ni vikundi vya kijasusi. na ndio maana wanausalama wote hawaruhusiwi kujiweka alama kama hizo mwilini
Watu wapo mazabe hapo Sao,ilifanyikaa opération kubwa ndani walikuwa wanatafutwa watu wenye alama fulani .....ilikuwa sooooo
Kuna mambo mtu hupitia n'a kukutana navyo
Ila tatoo Noma sana,siku hzo watu wanajichoraaa msimu mzimaaa....
Lakini zamani tatoo walikuwa mabaharia n'a makundi ya uhalifu.....
 
Dah mimi nilicho jifunza ni mshana jr kasafiri sasa story za miujiza nani atatupa humu ndani maana atakua bize na masomo halafu hiv jamii forums na huko uko ulaya ipo kweli?
SIJUI ITAKUWAJE AISEEE...
 
Back
Top Bottom