KASHAMBURITA
JF-Expert Member
- Mar 27, 2021
- 201
- 631
- Thread starter
- #21
Hadithi fupi!
SITOSAHAU ALICHONIFANYA DAKTARI WA SARATANI YA MATITI
SEHEMU YA KUMI
TULIPOISHIA
Nilimtumia ujumbe “Mbona hutaki kupokea simu yangu, nisamehe mume wangu” nilimuita kimahaba hivyo. Kweli haikuchukua muda akapiga.
Nilipopokea simu nilimuita kwa hisia “Mume wangu” lakini cha kushangaza nilisikia nimejibiwa na sauti ya kike ikiniuliza
“Wewe nani???” niliishiwa nguvu
ENDELEA
“Mhh” ilibidi nigune kidogo nikasikilizia na kumuambia “Samahani labda nimekosea namba” nilikata simu kwa haraka nikaiangalia namba vizuri ili kujua kama ni ya kwake au nilikosea.
Nilipoiangalia ile namba niligundua ndiyo ile ile, nilikasirika, nilijaribu kujifosi kutokuumia lakini kadri dakika zilivyokuwa zinasogea ndivyo moyo wangu ulivyokuwa unauma na kujisikia vibaya zaidi na zaidi.
Nilijikuta namchukia kabisa Hemed, nikafuta namba yake na kuamua kukaa kwa amani.
Kiukweli sikujua penzi limeshaniingia sana, niliwaza siku nzima, pia nilijuta kumuambia mama yangu kuhusu yeye maana mimi nilikuwa nahitaji mume halafu yeye alionekana kuwa na wanawake tofauti tofauti.
Nilikumbuka kauli ambayo nilishawahi kuiona kwenye mtandao kwamba usimwamini mwanaume mwenye ndevu nyingi, na hilo ndilo lililonifanya nikahisi ni kweli.
Nikaanza kujitia moyo “Kwanza ni mkubwa kwangu, sikupaswa kuoana na mtu kama huyo…nitatafuta wa rika langu na hata wa dini yangu….Eeh Mungu niletee” nilisema huku nikipanga nguo zangu taratibu.
Ilipofika jioni ndipo niliona ujumbe kutoka kwa Hemed ukisema hivi “Hello mke wangu, leo mbona umenisusa hivi?” nilipoitazama namba ni ya kwake, nikaufuta ule ujumbe bila hata kumjibu halafu nikasonya lakini akanipandia hewani.
Niliitazama simu kwa muda mrefu bila kupokea lakini almashauri ya ubongo wangu ikaniambia nipokee ili nimuambie ukweli, nikapokea
“Hallo” nilisema
“Poa vipi mbona leo umekuwa kimya sana?” aliniuliza
“Embu niache bwana” nilisema
“Nikuache kivipi? Hivi nimekukosea au?”
“Hemed, niache na maisha yangu, sitaki mawazo ya haraka haraka tu hivi, nilipokuwa zangu bila mwanaume nilikuwa na furaha ya ajabu….naona stress zimeshaanza”
“Stress??? How???” aliniuliza
“Una mke wako, mimi sihitaji kuwa na wewe”
“Acha mambo yako, kila kitu si nilikueleza Pendo? Sina mwanamke, ila kuna mwanamke ambaye tumepanga kuoana, si nilikuambia haya tangu jana??” aliniuliza
“mimi sio mtoto”
“Nini sasa”
“Asubuhi nimekupigia, aliyepokea simu ni mke wako….ananifokea”
“Mke wangu? Simu yangu saa ngapi?” aliniuliza
“Saa mbili….mbona unakuwa muongo, embu angalia call logs za asubuhi acha kunidanganya bhana aah” nilisema na kukata simu kwa hasira nikaiweka pembeni na kujilaza kidogo kwenye kiti cha dukani
Baada ya dakika moja alinipigia, nikapokea, na nilipopokea tu alikuwa anacheka sana ndipo nikamuuliza “Vipi mbona unanicheka?”
“Hahahahaa…lazima nikucheke, sasa wewe hiyo simu amepokea nani? Huyo si ndio mdogo wangu nilikuambia anakaa na binti yangu mamy??” aliniambia
“Mmmh…” niliguna huku nikijikuta naelekea kumuamini “Hivi kwanini uwe muongo, simu mnashirikiana na mdogo wako?”
“Mara nyingi simu yangu ni ya kazi, nilikuwa bafuni kuna appointment nilikuwa nayo, nikamuambia kwamba akipiga mtu apokee”
“Khaa….sijui”
“Ndio, au kama vipi ngoja usiku nije nikuchukue tuende nyumbani kabisa ukamuone” alisema Dr Hemed
“Mh”
“Ndio hivyo…..namalizia jukumu hapa, halafu nakufuata ofisini kwako sawa?”
“Ok” nilisema.
***
Ilipofika saa moja usiku nilitaka kufunga nikaona nimtafute nimuulize kama ananifuata au niondoke zangu, akanijibu
“Nakuja hapo soon….usiwe na wasiwasi”
“Saa ngapi?”
“Sasa hivi”
“Ok fanya haraka mimi sitaki kuchelewa nyumbani kama jana, au niache niondoke nije kesho mapema”
“No baby, unajua kabisa nia yangu kukuoa” alisema
“Mh…kunioa tena?”
“Ndio kwani sijakuambiaga?”
“Mh”
“Nakuja” alisema na kukata simu yake nikabaki nawaza huyu mwanaume anamaanisha au la, may be nilihisi yuko serious, nilikuwa nimeshampenda kidogo lakini niliona kabisa navyoelekea kutumbukia kwenye mapenzi na mtu ambaye hata hatujuani vizuri.
Nilisubiri dakika kama kumi na tano kweli alikuja yule kaka na siku ile alikuwa na gari yake, nikafunga duka na kupanda ndani ya gari na kuondoka kuelekea kwake nyumbani.
Tukiwa barabarani, kuna msichana alisimama katikati ya barabara akawa amenyoosha mikono kwa ishara ya kutaka kugongwa lakini Hemed alishika break na kushasha kioo akamchungulia yule msichana anacheka.
“Nitakugonga” alisema Hemed
“Ungenigonga uone kitakachokukuta” alisema binti huku akitabasamu na kuchungulia ndani ya gari. Ilionekana watu hawa wanafahamiana kwa kiasi kikubwa.
“Hahaha….vipi unafanya nini hapa?” Hemed aliuliza
“Nilikuwa nakusubiri wewe”
“Oh…basi sawa mi niko na mgeni nampeleka home” alisema Hemed
“Mh…” alisema yule msichana kisha akaniangalia na kuniambia “Mambo”
“Poa” nilijibu
“Basi, tutachat au?” aliuliza binti
“Hamna noma” alisema Hemed
Hemed aliendesha gari kwa mwendo wa taratibu, mimi sikumuuliza chochote, ila tulipofika getini kwenye nyumba aliyokuwa anaishi pia alikuja jirani mmoja wa kike, akampatia kitu fulani kwenye mfuko, na kumuuliza “Baadaye tutaonana au?”
Hemed akajibu “Kwa leo sidhani ila nitakuambia kwenye simu”
Niliweka mikono kifuani tu nashangaa mwanaume amezoeana sana na wanawake halafu wote ni wazuri nilijisikia vibaya ila sikutaka kumuonyesha kwamba nimekasirishwa. Alifungua geti kisha tukaingia ndani…..ITAENDELEA
SITOSAHAU ALICHONIFANYA DAKTARI WA SARATANI YA MATITI
SEHEMU YA KUMI
TULIPOISHIA
Nilimtumia ujumbe “Mbona hutaki kupokea simu yangu, nisamehe mume wangu” nilimuita kimahaba hivyo. Kweli haikuchukua muda akapiga.
Nilipopokea simu nilimuita kwa hisia “Mume wangu” lakini cha kushangaza nilisikia nimejibiwa na sauti ya kike ikiniuliza
“Wewe nani???” niliishiwa nguvu
ENDELEA
“Mhh” ilibidi nigune kidogo nikasikilizia na kumuambia “Samahani labda nimekosea namba” nilikata simu kwa haraka nikaiangalia namba vizuri ili kujua kama ni ya kwake au nilikosea.
Nilipoiangalia ile namba niligundua ndiyo ile ile, nilikasirika, nilijaribu kujifosi kutokuumia lakini kadri dakika zilivyokuwa zinasogea ndivyo moyo wangu ulivyokuwa unauma na kujisikia vibaya zaidi na zaidi.
Nilijikuta namchukia kabisa Hemed, nikafuta namba yake na kuamua kukaa kwa amani.
Kiukweli sikujua penzi limeshaniingia sana, niliwaza siku nzima, pia nilijuta kumuambia mama yangu kuhusu yeye maana mimi nilikuwa nahitaji mume halafu yeye alionekana kuwa na wanawake tofauti tofauti.
Nilikumbuka kauli ambayo nilishawahi kuiona kwenye mtandao kwamba usimwamini mwanaume mwenye ndevu nyingi, na hilo ndilo lililonifanya nikahisi ni kweli.
Nikaanza kujitia moyo “Kwanza ni mkubwa kwangu, sikupaswa kuoana na mtu kama huyo…nitatafuta wa rika langu na hata wa dini yangu….Eeh Mungu niletee” nilisema huku nikipanga nguo zangu taratibu.
Ilipofika jioni ndipo niliona ujumbe kutoka kwa Hemed ukisema hivi “Hello mke wangu, leo mbona umenisusa hivi?” nilipoitazama namba ni ya kwake, nikaufuta ule ujumbe bila hata kumjibu halafu nikasonya lakini akanipandia hewani.
Niliitazama simu kwa muda mrefu bila kupokea lakini almashauri ya ubongo wangu ikaniambia nipokee ili nimuambie ukweli, nikapokea
“Hallo” nilisema
“Poa vipi mbona leo umekuwa kimya sana?” aliniuliza
“Embu niache bwana” nilisema
“Nikuache kivipi? Hivi nimekukosea au?”
“Hemed, niache na maisha yangu, sitaki mawazo ya haraka haraka tu hivi, nilipokuwa zangu bila mwanaume nilikuwa na furaha ya ajabu….naona stress zimeshaanza”
“Stress??? How???” aliniuliza
“Una mke wako, mimi sihitaji kuwa na wewe”
“Acha mambo yako, kila kitu si nilikueleza Pendo? Sina mwanamke, ila kuna mwanamke ambaye tumepanga kuoana, si nilikuambia haya tangu jana??” aliniuliza
“mimi sio mtoto”
“Nini sasa”
“Asubuhi nimekupigia, aliyepokea simu ni mke wako….ananifokea”
“Mke wangu? Simu yangu saa ngapi?” aliniuliza
“Saa mbili….mbona unakuwa muongo, embu angalia call logs za asubuhi acha kunidanganya bhana aah” nilisema na kukata simu kwa hasira nikaiweka pembeni na kujilaza kidogo kwenye kiti cha dukani
Baada ya dakika moja alinipigia, nikapokea, na nilipopokea tu alikuwa anacheka sana ndipo nikamuuliza “Vipi mbona unanicheka?”
“Hahahahaa…lazima nikucheke, sasa wewe hiyo simu amepokea nani? Huyo si ndio mdogo wangu nilikuambia anakaa na binti yangu mamy??” aliniambia
“Mmmh…” niliguna huku nikijikuta naelekea kumuamini “Hivi kwanini uwe muongo, simu mnashirikiana na mdogo wako?”
“Mara nyingi simu yangu ni ya kazi, nilikuwa bafuni kuna appointment nilikuwa nayo, nikamuambia kwamba akipiga mtu apokee”
“Khaa….sijui”
“Ndio, au kama vipi ngoja usiku nije nikuchukue tuende nyumbani kabisa ukamuone” alisema Dr Hemed
“Mh”
“Ndio hivyo…..namalizia jukumu hapa, halafu nakufuata ofisini kwako sawa?”
“Ok” nilisema.
***
Ilipofika saa moja usiku nilitaka kufunga nikaona nimtafute nimuulize kama ananifuata au niondoke zangu, akanijibu
“Nakuja hapo soon….usiwe na wasiwasi”
“Saa ngapi?”
“Sasa hivi”
“Ok fanya haraka mimi sitaki kuchelewa nyumbani kama jana, au niache niondoke nije kesho mapema”
“No baby, unajua kabisa nia yangu kukuoa” alisema
“Mh…kunioa tena?”
“Ndio kwani sijakuambiaga?”
“Mh”
“Nakuja” alisema na kukata simu yake nikabaki nawaza huyu mwanaume anamaanisha au la, may be nilihisi yuko serious, nilikuwa nimeshampenda kidogo lakini niliona kabisa navyoelekea kutumbukia kwenye mapenzi na mtu ambaye hata hatujuani vizuri.
Nilisubiri dakika kama kumi na tano kweli alikuja yule kaka na siku ile alikuwa na gari yake, nikafunga duka na kupanda ndani ya gari na kuondoka kuelekea kwake nyumbani.
Tukiwa barabarani, kuna msichana alisimama katikati ya barabara akawa amenyoosha mikono kwa ishara ya kutaka kugongwa lakini Hemed alishika break na kushasha kioo akamchungulia yule msichana anacheka.
“Nitakugonga” alisema Hemed
“Ungenigonga uone kitakachokukuta” alisema binti huku akitabasamu na kuchungulia ndani ya gari. Ilionekana watu hawa wanafahamiana kwa kiasi kikubwa.
“Hahaha….vipi unafanya nini hapa?” Hemed aliuliza
“Nilikuwa nakusubiri wewe”
“Oh…basi sawa mi niko na mgeni nampeleka home” alisema Hemed
“Mh…” alisema yule msichana kisha akaniangalia na kuniambia “Mambo”
“Poa” nilijibu
“Basi, tutachat au?” aliuliza binti
“Hamna noma” alisema Hemed
Hemed aliendesha gari kwa mwendo wa taratibu, mimi sikumuuliza chochote, ila tulipofika getini kwenye nyumba aliyokuwa anaishi pia alikuja jirani mmoja wa kike, akampatia kitu fulani kwenye mfuko, na kumuuliza “Baadaye tutaonana au?”
Hemed akajibu “Kwa leo sidhani ila nitakuambia kwenye simu”
Niliweka mikono kifuani tu nashangaa mwanaume amezoeana sana na wanawake halafu wote ni wazuri nilijisikia vibaya ila sikutaka kumuonyesha kwamba nimekasirishwa. Alifungua geti kisha tukaingia ndani…..ITAENDELEA