mizambwa
JF-Expert Member
- Oct 8, 2008
- 4,421
- 1,792
HADITHI: KIZUIZI
SEHEMU YA KWANZA
Majira ya saa tatu asubuhi waumini waliokuwa wanatarajia kuingia katika misa ya pili walikuwa wameanza kujongea katika kanisa katoliki parokia ya mtakatifu Francis maeneo ya National jijini Mwanza. Ibada ya kwanza ilikuwa inakaribia kumalizika, kipengele cha matangazo mbalimbali ndio kilikuwa kinaimalizia hiyo ibada iliyokuwa inaongozwa na paroko wa kanisa hilo. Hali ya hewa ilikuwa ya ubaridi na waumini walikuwa wamejikunyata kila mmoja kwa namna yake huku wakiyapokea matangazo hayo.
Mwanamama mfupi sana, nadhifu alikuwa mbele ya kipaza sauti akifuatisha mpangilio wa matangazo, aliyamaliza yale ya kawaida na sasa akayafikia mengine.
Matangazo ya ndoa yalikuwa yanasomwa.
"Bwana James Syaga wa parokia ya mtakatifu Kalolilwanga jijini Mwanza anatangaza kufunga ndoa na Bi. Emmy John wa parokia ya mtakatifu Joseph wilayani Kahama, hili ni tangazo lao la pili. Kwa yeyote mwenye kizuizi afikishe ofisini kwa paroko kabla ya tangazo la tatu" sauti ya mwanamama aliyekuwa anasoma matangazo ilisikika. Umri wake ulikuwa unafaa kuitwa bibi lakini alisoma kwa makini sana ukilinganisha na vijana ambao walikuwa na tatizo la kuchanganya herufi r na l. Huyu hakukosea.
Kanisa zima lilikuwa kimya, vilio vya watoto na vikohozi vya hapa na pale pekee ndio viliweza kuvuruga utulivu kiasi fulani. Ndege waliokuwa wamejenga viota vyao katika kanisa hilo pia walikuwa wanaruka hapa na pale huku wakiimba nyimbo zao nzuri za kuvutia.
Mwanamama yule aliendelea kusoma matangazo mengine ya ndoa huku umakini ukiwa kwa hali ya juu kwa wale waliokuwa wanasikiliza, kwa wale wasiokuwa na ndoa wakawa wanajisikia aibu huku wenye ndoa wakijisikia fahari kuwa mfano kwa wengine.
Tofauti na vilio vya watoto, kuna watu wazima wawili walikuwa wananong'ona kwa tahadhari ili wasiweze kusikiwa na mtu mwingine kuwa na wao wanachangia kuvunja utaratibu ndani ya kanisa, hasahasa padri aliyekuwa anaongoza ibada hii ya misa. Maana hakuwa na dogo, akikugundua unanongona alikuwa anakusema hapohapo.
Wawili hawa mwanamke na mwanamume walikuwa katika mjadala mkubwa sana.
"Ni Jimmy huyohuyo...haiwezekani Bibiana haiwezekani" Mwanaume alikuwa akimwambia mwenzake wa kike aliyeitwa Bibiana.
"Wewe Deo, ndiye James huyo au watakuwa wamefanana majina?" Mwanamke ni kama hakuwa na uhakika bado.
"Ni yeye bwana, mi namfahamu hadi huyo msichana anayetaka kumuoa...anachofanya sio sahihi." Deo alimjibu Bibiana kwa manunguniko makubwa sana.
"Kama ni yeye kweli, kesho naenda kwa Paroko, sikubali." alimaliza mazungumzo Bibiana huku uso wake ukitangaza chuki dhidi ya James Syaga.
Chuki aliyoijua yeye na nafsi yake.
Labda alitaka aolewe yeye? Labda ni chuki binafsi. Nani anayejua?
Deo akamuunga mkono.
****
Mazungumzo ya kunong'ona kati ya Bibiana na Deo ndani ya kanisa wakati matangazo ya ndoa yakiendelea yalimshtua kijana Joseph Boniphace ambaye alikuwa anaanza kupitiwa na usingizi baada ya kuwa amejikunyata kwa muda mrefu, mazungumzo hayo yalianza kama kero kwake, kwani yalikuwa yakimzuia kusinzia kwa amani, lakini kutajwatajwa jina la James na watu hawa kulichangia mshtuko wake wa pili. Kwa nini wanamtaja James?? Alijiuliza. Lazima kuna kitu hapa.
Kwa tabia ya kupenda kujua yasiyomuhusu alitumia fursa hiyo kujitendea haki. Aliukemea ule usingizi nao ukamtii. Akayaamuru masikio yake kuwa makini, nayo pia yakamtii. Akaifurahia hali ile. Akayafumba macho yake kama vile amesinzia kumbe yu macho!!
Tabia yake hii ya kupenda kujua mengi tena yasiyomuhusu ilimfanya apate umaarufu fulani usiokuwa na tija wala malipo, umaarufu wa kijinga katika vikundi vikundi alikuwa muongeaji mkuu, jambo gani limpite Jose asilijue? Skendo gani litapita mtoto huyu wa Boniphace pembeni na asilijue mwanzo hadi mwisho wake?? Kwa maisha yake hayo ya kujua kila kitu hatimaye akafupishwa jina lake kuwa Jose kwani kumuita Joseph ilionekana ni kupoteza muda lakini ili kumkumbuka mzazi aliyemzaa kijana huyu jina la Boniphace likafupishwa na kuwa B yaani Jose B.
Jose B licha ya kujifanya kujua mengi, hakuwa muongo kila mara alikuwa na taarifa za uhakika, kwa hali hiyo watoto wa mjini wakawa wanamuitawa ukweli na hatimaye likaunganika jina tamu kutamka lililoyapendeza masikio ya kila mtu kusikia Joseph Boniphace akawa Jose B Waukweli.
Jina alilolipenda na kulitendea haki. Jose akawa Jose kweli.
Jose alijifanya amesinzia kabisa lakini masikio yake yalikuwa wazi yakisikiliza kwa makini minong'ono hiyo kama yalivyokuwa yameamurishwa. Machale yakamcheza kuwa hayo mazungumzo hayakuwa tu ya kimbea ambayo yanaweza kumuongezea umaarufu bali yangeweza kutumika pia kama biashara kwake.
Jose kwa mara ya kwanza katika maisha yake ya kupenda kujua kila kitu akawaza kuyatumia mazungumzo hayo ya siri kujipatia chochote kitu. Jose akawaza pesa!!
Japo hakuwa akimfahamu vyema huyo muhusika anayezungumziwa lakini aliamini akiweka jitihada atamfahamu.
Kizuizi!! Alijiuliza, wanataka kumwekea kizuizi gani? Alikosa majibu. Na hata kama angekuwa na jibu bado hakumjua muhusika.
Roho ilimuuma sana baada ya wawili hawa kukatisha maongezi yao. Aliumia kwa kuwa bado alikuwa hajapata stori iliyokamilika, lawama zake zilienda moja kwa moja kwa padri aliyeamuru waumini wasimame kwa ajili ya sala ya mwisho ya kufunga ibada. Jose B akahisi padri hakuwa ametenda haki.
Lakini alifurahi kwa kuwa alipata vitu vitatu, jina la James Syaga, pili majina ya waliokuwa wakimteta (Deo na Bibiana) na tatu KIZUIZI!!
"Hata hayo yanatosha!'' Alijisemea Jose B huku akiyakariri vyema majina hayo matatu kama vile anaenda kuweka majibu hayo katika mtihani darasani.
Sasa alitamani misa imalizike aanze kuitumia taarifa hiyo, alihofia kuwa maneno mengi ya kukariri aliyokuwa akiyataja padri kwa kutumia kinasa sauti yangeweza kumuathiri na kumsahaulisha yale majina. Hivyo kila padri alivyokuwa akiwaamrisha kusema maneno fulani. Deo alijibu kwa sauti ya chinichini, Deo, James, Bibiana na Kizuizi. Kwa mtindo huu hakuna lililompotea kichwani.
Jose B, alijiona mwenye bahati sana kuwa wa kwanza kupata habari. Nitazidi kuwa maarufu!!! Aliwaza.
Na pia nitapata pesa ikibidi.
***
Maandalizi ya harusi yalikuwa yamepamba moto, simu ya James Syaga ilikuwa bize kila mara, vikao vilikuwa vinaendelea jijini Dar es salaam. Marafiki wa James hawakutaka kumwangusha kila mmoja alishughulika ipasavyo, jambo zuri kila mmoja alikuwa vyema kiuchumi.
Milioni thelathini zilizuwa zimechangwa tayari katika vikao vitatu vya harusi. Na bado ahadi zilikuwa nyingi sana, na zilikuwa ahadi za uhakika. Kwani zilitolewa na watu wa uhakika.
Emmy John alikuwa amechukua likizo ya majuma mawili kazini, sasa alikuwa ni mtu wa kujifungia ndani tu akisubiri kwa hamu kubwa kutimiza ndoto yake, ndoto ya kuolewa huku akiwa na usichana wake (bikra), ahadi aliyowahi kuwahaidi wazazi wake tangu akiwa katika umri wa balehe. Na kubwa zaidi ndoto ya kuolewa na James, mwanaume wa maisha yake.
Emmy na James wote waliona kama siku hazisogei. Sasa tangazo la pili lilikuwa limepita, na lilikuwa limebaki tangazo moja waweze kuhalalishwa.
James Syaga na Emmy John kuwa mtu na mke wake.
Hiyo ndoto kila mtu aliyewafahamu wawili hawa alitamani itimie.
Na kwa nini isitimie? Pesa zilikuwepo. James alikuwa na biashara zake na Emmy alikuwa mfanyakazi, tena anayelipwa mshahara mkubwa.
Pande mbili za familia hazikuwa na vikwazo vyovyote juu ya ndoa hii. Familia ya Emmy ilimpenda sana James. Sasa nini cha kuzuia ndoto hii kutimia?? Hapakuwa na chochote!!!
Wakati kila upande ukiamini kuwa hakuna kitakachoharibika. Kinaibuka kizuizi katika tangazo la tatu na la mwisho, kizuizi kipo maili nyingi sana kutoka jiji la Dar es salaam, Kizuizi kipo jijini Mwanza.
Hakuna anayejua.
Je? Ni kizuizi kipi Bibiana na Deo wanataka kumwekea James Syaga?
Je? Jose B atafanikiwa KUKIGEUZA KIZUIZI biashara??
NINI KITATOKEA?
Usikose sehemu inayofuata. Huenda yakakukuta siku moja na wewe!!!!
ITAENDELEA
SEHEMU YA KWANZA
Majira ya saa tatu asubuhi waumini waliokuwa wanatarajia kuingia katika misa ya pili walikuwa wameanza kujongea katika kanisa katoliki parokia ya mtakatifu Francis maeneo ya National jijini Mwanza. Ibada ya kwanza ilikuwa inakaribia kumalizika, kipengele cha matangazo mbalimbali ndio kilikuwa kinaimalizia hiyo ibada iliyokuwa inaongozwa na paroko wa kanisa hilo. Hali ya hewa ilikuwa ya ubaridi na waumini walikuwa wamejikunyata kila mmoja kwa namna yake huku wakiyapokea matangazo hayo.
Mwanamama mfupi sana, nadhifu alikuwa mbele ya kipaza sauti akifuatisha mpangilio wa matangazo, aliyamaliza yale ya kawaida na sasa akayafikia mengine.
Matangazo ya ndoa yalikuwa yanasomwa.
"Bwana James Syaga wa parokia ya mtakatifu Kalolilwanga jijini Mwanza anatangaza kufunga ndoa na Bi. Emmy John wa parokia ya mtakatifu Joseph wilayani Kahama, hili ni tangazo lao la pili. Kwa yeyote mwenye kizuizi afikishe ofisini kwa paroko kabla ya tangazo la tatu" sauti ya mwanamama aliyekuwa anasoma matangazo ilisikika. Umri wake ulikuwa unafaa kuitwa bibi lakini alisoma kwa makini sana ukilinganisha na vijana ambao walikuwa na tatizo la kuchanganya herufi r na l. Huyu hakukosea.
Kanisa zima lilikuwa kimya, vilio vya watoto na vikohozi vya hapa na pale pekee ndio viliweza kuvuruga utulivu kiasi fulani. Ndege waliokuwa wamejenga viota vyao katika kanisa hilo pia walikuwa wanaruka hapa na pale huku wakiimba nyimbo zao nzuri za kuvutia.
Mwanamama yule aliendelea kusoma matangazo mengine ya ndoa huku umakini ukiwa kwa hali ya juu kwa wale waliokuwa wanasikiliza, kwa wale wasiokuwa na ndoa wakawa wanajisikia aibu huku wenye ndoa wakijisikia fahari kuwa mfano kwa wengine.
Tofauti na vilio vya watoto, kuna watu wazima wawili walikuwa wananong'ona kwa tahadhari ili wasiweze kusikiwa na mtu mwingine kuwa na wao wanachangia kuvunja utaratibu ndani ya kanisa, hasahasa padri aliyekuwa anaongoza ibada hii ya misa. Maana hakuwa na dogo, akikugundua unanongona alikuwa anakusema hapohapo.
Wawili hawa mwanamke na mwanamume walikuwa katika mjadala mkubwa sana.
"Ni Jimmy huyohuyo...haiwezekani Bibiana haiwezekani" Mwanaume alikuwa akimwambia mwenzake wa kike aliyeitwa Bibiana.
"Wewe Deo, ndiye James huyo au watakuwa wamefanana majina?" Mwanamke ni kama hakuwa na uhakika bado.
"Ni yeye bwana, mi namfahamu hadi huyo msichana anayetaka kumuoa...anachofanya sio sahihi." Deo alimjibu Bibiana kwa manunguniko makubwa sana.
"Kama ni yeye kweli, kesho naenda kwa Paroko, sikubali." alimaliza mazungumzo Bibiana huku uso wake ukitangaza chuki dhidi ya James Syaga.
Chuki aliyoijua yeye na nafsi yake.
Labda alitaka aolewe yeye? Labda ni chuki binafsi. Nani anayejua?
Deo akamuunga mkono.
****
Mazungumzo ya kunong'ona kati ya Bibiana na Deo ndani ya kanisa wakati matangazo ya ndoa yakiendelea yalimshtua kijana Joseph Boniphace ambaye alikuwa anaanza kupitiwa na usingizi baada ya kuwa amejikunyata kwa muda mrefu, mazungumzo hayo yalianza kama kero kwake, kwani yalikuwa yakimzuia kusinzia kwa amani, lakini kutajwatajwa jina la James na watu hawa kulichangia mshtuko wake wa pili. Kwa nini wanamtaja James?? Alijiuliza. Lazima kuna kitu hapa.
Kwa tabia ya kupenda kujua yasiyomuhusu alitumia fursa hiyo kujitendea haki. Aliukemea ule usingizi nao ukamtii. Akayaamuru masikio yake kuwa makini, nayo pia yakamtii. Akaifurahia hali ile. Akayafumba macho yake kama vile amesinzia kumbe yu macho!!
Tabia yake hii ya kupenda kujua mengi tena yasiyomuhusu ilimfanya apate umaarufu fulani usiokuwa na tija wala malipo, umaarufu wa kijinga katika vikundi vikundi alikuwa muongeaji mkuu, jambo gani limpite Jose asilijue? Skendo gani litapita mtoto huyu wa Boniphace pembeni na asilijue mwanzo hadi mwisho wake?? Kwa maisha yake hayo ya kujua kila kitu hatimaye akafupishwa jina lake kuwa Jose kwani kumuita Joseph ilionekana ni kupoteza muda lakini ili kumkumbuka mzazi aliyemzaa kijana huyu jina la Boniphace likafupishwa na kuwa B yaani Jose B.
Jose B licha ya kujifanya kujua mengi, hakuwa muongo kila mara alikuwa na taarifa za uhakika, kwa hali hiyo watoto wa mjini wakawa wanamuitawa ukweli na hatimaye likaunganika jina tamu kutamka lililoyapendeza masikio ya kila mtu kusikia Joseph Boniphace akawa Jose B Waukweli.
Jina alilolipenda na kulitendea haki. Jose akawa Jose kweli.
Jose alijifanya amesinzia kabisa lakini masikio yake yalikuwa wazi yakisikiliza kwa makini minong'ono hiyo kama yalivyokuwa yameamurishwa. Machale yakamcheza kuwa hayo mazungumzo hayakuwa tu ya kimbea ambayo yanaweza kumuongezea umaarufu bali yangeweza kutumika pia kama biashara kwake.
Jose kwa mara ya kwanza katika maisha yake ya kupenda kujua kila kitu akawaza kuyatumia mazungumzo hayo ya siri kujipatia chochote kitu. Jose akawaza pesa!!
Japo hakuwa akimfahamu vyema huyo muhusika anayezungumziwa lakini aliamini akiweka jitihada atamfahamu.
Kizuizi!! Alijiuliza, wanataka kumwekea kizuizi gani? Alikosa majibu. Na hata kama angekuwa na jibu bado hakumjua muhusika.
Roho ilimuuma sana baada ya wawili hawa kukatisha maongezi yao. Aliumia kwa kuwa bado alikuwa hajapata stori iliyokamilika, lawama zake zilienda moja kwa moja kwa padri aliyeamuru waumini wasimame kwa ajili ya sala ya mwisho ya kufunga ibada. Jose B akahisi padri hakuwa ametenda haki.
Lakini alifurahi kwa kuwa alipata vitu vitatu, jina la James Syaga, pili majina ya waliokuwa wakimteta (Deo na Bibiana) na tatu KIZUIZI!!
"Hata hayo yanatosha!'' Alijisemea Jose B huku akiyakariri vyema majina hayo matatu kama vile anaenda kuweka majibu hayo katika mtihani darasani.
Sasa alitamani misa imalizike aanze kuitumia taarifa hiyo, alihofia kuwa maneno mengi ya kukariri aliyokuwa akiyataja padri kwa kutumia kinasa sauti yangeweza kumuathiri na kumsahaulisha yale majina. Hivyo kila padri alivyokuwa akiwaamrisha kusema maneno fulani. Deo alijibu kwa sauti ya chinichini, Deo, James, Bibiana na Kizuizi. Kwa mtindo huu hakuna lililompotea kichwani.
Jose B, alijiona mwenye bahati sana kuwa wa kwanza kupata habari. Nitazidi kuwa maarufu!!! Aliwaza.
Na pia nitapata pesa ikibidi.
***
Maandalizi ya harusi yalikuwa yamepamba moto, simu ya James Syaga ilikuwa bize kila mara, vikao vilikuwa vinaendelea jijini Dar es salaam. Marafiki wa James hawakutaka kumwangusha kila mmoja alishughulika ipasavyo, jambo zuri kila mmoja alikuwa vyema kiuchumi.
Milioni thelathini zilizuwa zimechangwa tayari katika vikao vitatu vya harusi. Na bado ahadi zilikuwa nyingi sana, na zilikuwa ahadi za uhakika. Kwani zilitolewa na watu wa uhakika.
Emmy John alikuwa amechukua likizo ya majuma mawili kazini, sasa alikuwa ni mtu wa kujifungia ndani tu akisubiri kwa hamu kubwa kutimiza ndoto yake, ndoto ya kuolewa huku akiwa na usichana wake (bikra), ahadi aliyowahi kuwahaidi wazazi wake tangu akiwa katika umri wa balehe. Na kubwa zaidi ndoto ya kuolewa na James, mwanaume wa maisha yake.
Emmy na James wote waliona kama siku hazisogei. Sasa tangazo la pili lilikuwa limepita, na lilikuwa limebaki tangazo moja waweze kuhalalishwa.
James Syaga na Emmy John kuwa mtu na mke wake.
Hiyo ndoto kila mtu aliyewafahamu wawili hawa alitamani itimie.
Na kwa nini isitimie? Pesa zilikuwepo. James alikuwa na biashara zake na Emmy alikuwa mfanyakazi, tena anayelipwa mshahara mkubwa.
Pande mbili za familia hazikuwa na vikwazo vyovyote juu ya ndoa hii. Familia ya Emmy ilimpenda sana James. Sasa nini cha kuzuia ndoto hii kutimia?? Hapakuwa na chochote!!!
Wakati kila upande ukiamini kuwa hakuna kitakachoharibika. Kinaibuka kizuizi katika tangazo la tatu na la mwisho, kizuizi kipo maili nyingi sana kutoka jiji la Dar es salaam, Kizuizi kipo jijini Mwanza.
Hakuna anayejua.
Je? Ni kizuizi kipi Bibiana na Deo wanataka kumwekea James Syaga?
Je? Jose B atafanikiwa KUKIGEUZA KIZUIZI biashara??
NINI KITATOKEA?
Usikose sehemu inayofuata. Huenda yakakukuta siku moja na wewe!!!!
ITAENDELEA