Hadithi: Bruno the Fisherman

Hadithi: Bruno the Fisherman

Inabidi tupitishe sheria mtu akituma uzi wake uwe mwanzo mpaka mwisho hii nikuzizarau Mb zetu tuazotumia kuingia humu kila muda tunakuta hola
 
BRUNO THE FISHERMAN

Mtunzi .Nyemo


Episode 13

“Today is the day,” (leo ndiyo siku yenyewe) alisema Tim huku akiwaangalia wenzake.
Walikaa nchini Kenya kwa siku kadhaa wakisubiri kufanya mipango ya kumteka Sharifa na kuondoka naye. Kwao, kazi hiyo haikuonekana kuwa ngumu tena kwa kuwa waliaminika na kila mtu aliyekuwa akiwaangalia aliwaamini kwamba walikuwa madaktari kutoka nchini Marekani.
Siku hiyo ambayo ndiyo waliyotaka kufanya tukio wakamwambia Sharifa kwamba lingekuwa jambo jema kujiunga nao kwani kesho yake wangeweza kuondoka kurudi nchini Marekani kuendelea na kazi zao nyingine.
Hilo lilimshtua Sharifa kwani kitu alichojua ni kwamba watu hao wangeendelea kukaa nchini Kenya kwa siku kadhaa. Kuhusu kuungana nao na kula chakula cha mchana halikuwa tatizo hata kidogo, akakubali na hatimaye kwenda sehemu fulani iliyokuwa na hoteli na kuanza kunywa.
Kichwa cha Sharifa hakikuwaza ubaya wowote ule, aliwaamini watu hao kwamba walikuwa wema kwa kuwa tangu walipofika nchini humo na kutoa msaada wa kuwasimamia wagonjwa wengine katika vituo vya afya walivyokuwa wamevianzisha.
Walikula na kunywa, walizungumza mambo mengi, walifurahia mno na kugongesheana mikono lakini vichwa vyao vilikuwa vikifikiria kitu kimoja tu, kumteka msichana huyo na kuondoka naye kuelekea Tanga.
Walipomaliza, wakaingia ndani ya gari. Humo ndipo Sharifa akagundua kwamba watu aliokuwanao hawakuwa wa kawaida, walibadilika, vile vicheko walivyokuwa wakicheka, vikapotea, sura zao zikawa na muonekano mwingine na kuanza kumtia hofu.
“Kuna nini?” aliuliza.
“Tulia hivyohivyo,” aliambiwa na kutolewa kisu, Tim akakishika na kumwamuru anyamaze kwani vinginevyo angemchoma tumboni, msichana huyo akafanya kama alivyoambiwa.
Gari likawashwa mahali hapo na kuanza kuondoka kuelekea katika barabara inayoelekea nchini Tanzania. Njiani, Sharifa alitakiwa kunyamaza kwani vingine angeuawa kama alivyoambiwa.
Hakukuwa na tatizo lolote lile barabarani, waliendelea na safari yao huku kila mmoja akitarajia kufika nchini Tanzania pasipo kupata kipingamizi chochote kile njiani.
Muda wote huo Sharifa alikuwa na hofu, hakujua kilichokuwa kikiendelea, aliwaamini watu hao lakini ghafla walibadilika na kuwa watekaji.
Kila alichokuwa akijiuliza juu ya kile kilichokuwa kimetokea alikosa majibu. Kila alipotaka kuuliza kitu, aliambiwa kunyamaza, hakutakiwa kuzungumza jambo lolote lile kwani kama angekaidi basi angechomwa kisu kama alivyokuwa ameambiwa. Hivyo akanyamaza.
***
Muda ulikuwa ukienda, kila mmoja nyumbani alijua kwamba muda wowote ule Sharifa angerudi nyumbani hapo na kuendelea na majukumu lakini msichana huyo hakutokea.
Nyumbani kwake, wafanyakazi walikuwa na hofu, wakahisi kwamba alipitia sehemu fulani hivyo kuendelea kumsubiri lakini kitu cha ajabu kabisa msichana huyo hakutokea mahali hapo.
Mpaka inafika majira ya saa mbili usiku, bado hakuwa amefika. Hilo likawatia wasiwasi na kuhisi kwamba kulikuwa na jambo lilikuwa limetokea, haikuwa kawaida na mbaya zaidi kila walipokuwa wakimpigia simu haikuwa ikipatikana.
Walichokifanya ni kumpigia Bruno na kumwambia kilichotokea. Alipoambiwa hivyo, hakutaka kuendelea kubaki jijini Nairobi, ni kweli alikuwa bize lakini kwake, familia ilikuwa ni zaidi ya pesa na mali hivyo akarudi haraka sana Mombasa ili kuangalia ni kitu gani kilikuwa kikiendelea.
Njiani, alijaribu mara kadhaa kumpigia simu Sharifa, hazikuwa zikipatikana, Hilo lilimtisha na kumfanya kuogopa, akahisi kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea, akapiga simu zaidi na zaidi lakini majibu yaliendelea kuwa yaleyale.
Hakutaka kuchelewa, alichokifanya ni kuripoti polisi na kuwaambia kile kilichokuwa kimetokea. Kila polisi alishangaa, hawakuamini kama Wazungu waliokuwa wametajwa wangeweza kushirikiana kumtena msichana huyo.
Wakamuuliza maswali kadhaa kuhusu Wazungu hao, akawaambia kwamba walitoka nchini Marekani na walifika huko kwa kuwa walitaka kuwasaidia wagonjwa waliokuwa wakiteseka na magonjwa mbalimbali nchini humo.
“Mh! Sasa Wazungu wamemteka au kuna watu wamewateka na hao Wazungu?” aliuliza polisi mmoja huku akionekana kushangaa.
“Hatuna jibu. Naomba mfuatilie,” alisema Bruno huku akionekana kuchanganyikiwa.
Hilo ndilo lililofanyika, mtu ambaye mchumba wake alikuwa ametekwa alikuwa Bruno, mwanaume aliyeibuka ghafla na pesa na kuwa mtu mwenye heshima kubwa mno.
Polisi hawakutaka kusubiri, hawakutaka kuona suala hilo likifika mbali zaidi mpaka rais kujua, ili kuwe na amani, waokoe vibarua vyao ilikuwa ni lazima kupambana kuhakikisha msichana huyo anapatikana mara moja.
Simu zikapigwa katika vituo vya polisi na kuambiwa kilichokuwa kikiendelea, walitakiwa kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha Sharifa na Wazungu wale wanapatikana haraka iwezekanavyo.
Bruno hakuwa na furaha tena, moyo wake ulinyong’onyea na kuona kabisa kwamba asingeweza kumuona tena mpenzi wake. Hakulala, usiku mzima alikuwa akiongea na wakubwa wa vituo kuhusu mpenzi wake kama alikuwa ameonekana sehemu au la.
Wakati hayo yote yakiendelea, zilikuwa zimebaki siku mbili kabla ya kesi ya mzee Todd kuendelea nchini Marekani. Akiwa katika hali hiyo, akapigiwa simu kutoka moja kwa moja nchini Marekani na kuambiwa kwamba alikuwa akihitajika nchini Marekani kwa ajili ya kutoa ushahidi katika kesi ya mzee Todd.
Alipoambiwa hilo tu, akaanza kupata picha, akaunganisha tukio lililotokea la kutekwa kwa mchumba wake na kesi ile ya mzee Todd, akahisi kabisa vitu hivyo vilikuwa vimepangwa, kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea.
Huku akiendelea kuwa katika hali hiyo, akapigiwa simu tena, akaichukua na kuangalia kioo, mpigaji hakuwa mwingine bali ilikuwa ni namba ya mchumba wake, muda huo ulikuwa ni saa sita usiku.
“Halo! Sharifa upo wapi?” aliuliza mara baada ya kuipokea simu ile.
“Unatakiwa kufanya kitu kimoja tu,” ilisikika sauti ya mwanaume mmoja kutoka upande wa pili, alikuwa Tim.
“Unasemaje?”
“Sikiliza maelezo yetu kwanza,” alisikika Tim.
Akamwambia kilichokuwa kikiendelea, alikuwa akihitajika nchini Marekani kwa lengo la kwenda kutoa ushahidi katika kesi ya mzee Todd, hapo, Tim alimwambia kwamba alitakiwa kutokwenda nchini humo kwani kama angekwenda, mchumba wake angeuawa kwa kuchomwa visu kwa kuwa alikuwa mikononi mwao.
Bruno aliposikia maneno hayo, akaogopa, akahisi kabisa mwanaume huyo hakuwa akitania kwani hata sauti yake ilivyokuwa ikitoka, ilionyesha ni kwa jinsi gani alikuwa siriazi kwa kile alichokuwa akikizungumza.
“Naomba msimuue mpenzi wangu,” alisema Bruno huku machozi yakianza kumtiririka mashavuni mwake.
“Hatutomuua kama tu hautokwenda nchini Marekani, vinginevyo, tutamuua yeye na hata hicho kiumbe kilichopo tumboni mwake,” alisikika Tim, maneno aliyokuwa ameyazungumza yalimfanya Bruno kuogopa kupita kawaida.
***
Mzee Bruno alitulia huku masikio yake yakiwa kwa wakili wake, Harris. Mwanaume huyo hakumwambia kitu chochote kuhusu kutekwa kwake, alijua kwamba kama angemwambia ukweli basi hali ingekuwa mbaya zaidi na inawezekana watu wale wangemrudia tena na kumteka kama walivyofanya.
Alizungumza naye kwa utaratibu, hakutaka kumuonyeshea dalili kwamba kulikuwa na kitu kilichokuwa kimetokea, alimpa matumaini kwamba angeshinda kesi ile pasipo kumwambia kuwa mashahidi waliokuwa na nguvu ya kumtoa walikuwa njiani kuuawa.
Yeye ndiye aliyekuwa akimwambia hali ilivyokuwa ikiendelea. Hakumficha, alimwambia kuwa Wamarekani walimchukia na kila mmoja kwa kipindi hicho alikuwa akitaka kuona akihukumiwa kifo kama watu wengine.
Hilo lilimuhuzunisha mzee huyo kwani hakuwa amefanya jambo lolote baya, hakuwa ameua wala yale madawa ya kulevya yaliyokutwa ndani ya nyumba yake hayakuwa yake.
Kila alipokuwa akimuuliza kuhusu mashahidi wake kama walipigiwa simu, Harris alikuwa akijiumauma kana kwamba kulikuwa na jambo baya sana ambalo mzee huyo hakutakiwa kulijua.
“Waliwasiliana nao,” alisema.
“Ikawaje?”
“Waliniambia kwamba watakuja!”
“Watakuja? Washaanza safari? Serikali ndiyo inatakiwa kuwasafirisha! Wameanza hiyo safari?” aliuliza.
“Hata sijajua!”
“Harris! Inakuwaje usijue na wakati wewe ndiye wakili wangu ninayekutegemea?” aliuliza mzee Todd.
Harris hakuwa na cha kujibu, hofu ilimtanda moyoni mwake. Mpaka kufikia hatua hiyo, tayari mzee Todd akahisi kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea ambacho mtu huyo aliyemtegea hakutaka kumwambia ukweli.
Siku hazikuwasubiri, zikaendelea kukatika kama kawaida. Mpaka siku ya kupanda tena mahakamani, bado mashahidi hawakuwa wamefika mahakamani na kwa taarifa ambazo zilianza kuzagaa ni kwamba mtu aliyetajwa kama shahidi namba mbili, Innocent alipotea katika mazingira ya kutatanisha, na hakukuwa na mtu aliyejua mahali alipokuwa.

Je, nini kitaendelea?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom