Unafikiri Gwajima anachochote cha maana? Hana cheti wala kitu chochote kinachofanana na Cheti, haiwezekani Gwajima adai ufeki wa vyeti na kutofaulu kwa Makonda na madai kuwa alitumia vyeti vya watu wengine nakutaja jina halisi la Makonda, iweje leo ataje taarifa za Makonda baada tu ya yeye Gwajima kutajwa kuhusika na Madawa ya kulevya? Makonda alianza kuwa Mkuu wa Wawilaya, na baadaye Rc, na alipoanza kushughulika na mihadarati, na kumtaja Gwajima, ghafla ikaja hoja ya vyeti, pia ikumbukwe kuwa kabla ya tuhuma za mihadarati kwa Gwajima, Gwajima mwenyewe aliwahi kumkaribisha Makonda kwenye kanisa lake, sasa aliwezaje kumkaribisha Makonda mwenye vyeti feki,tena akatumia mimbari ambapo ni mahali patakatifu. Gwajima ni Muongo mkubwa.