Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 22,494
- 33,052
GWAJIMA NA SIASA ZA UBUNGE
Mchungaji Gwajima alipotangaza nia ya kugombea ubunge kupitia CCM video zake nyingi ziliwekwa mitandaoni akizungumza mambo mbali mbali lakini mbili ndiyo zilionekana kupendwa zaidi.
Video ya kwanza kwa umaarufu ni ile anayoahidi kugeuza madrasa zote za Waislam kuwa Sunday schools.
Video ya pili ni hii ambayo anasema yeye kama mtumishi wa Mungu hawezi kutamani kushika nafasi kama ya ubunge au uwaziri.
Ile kauli yake ya kwanza ya kugeuza madrasa za Waislam kuwa Sunday Schools ukitaka kuielewa uzito wake kimantiki inabidi uigeuze iwe maneno yale kayasema sheikh kuwa anataka kubadili Sunday Schools zote makanisani ziwe madrasa.
Sasa hapo simama na utulie tuli uwaze nini kingefuatia kwa sheikh huyo.
Jaribu kufikiri kurasa za mbele za magazeti siku ya pili yangekuwaje?
Mimi naogopa hata kufikiri ingekuwaje.
Je, unaweza kufikiri Jeshi la Polisi lingesema nini na kuchukua hatua gani?
Hakuna kilichofanyika.
Magazeti yote yalikuwa kimya.
Jeshi la Polisi lilikuwa kimya.
Waislam walikuwa kimya.
Na hadi leo Waislam bado wako kimya na wataendelea kuwa kimya.
Lakini si kama kweli Waislam wako kimya.
Kuwasikia Waislam inahitaji uwe na masikio.
Waislam tumesema kwa ule ukimya wetu.
Kwani ukimya una sauti.
Ukiwa na masikio mazuri utasikia sauti ya ukimya.
Mchungaji Gwajima alipotangaza nia ya kugombea ubunge kupitia CCM video zake nyingi ziliwekwa mitandaoni akizungumza mambo mbali mbali lakini mbili ndiyo zilionekana kupendwa zaidi.
Video ya kwanza kwa umaarufu ni ile anayoahidi kugeuza madrasa zote za Waislam kuwa Sunday schools.
Video ya pili ni hii ambayo anasema yeye kama mtumishi wa Mungu hawezi kutamani kushika nafasi kama ya ubunge au uwaziri.
Ile kauli yake ya kwanza ya kugeuza madrasa za Waislam kuwa Sunday Schools ukitaka kuielewa uzito wake kimantiki inabidi uigeuze iwe maneno yale kayasema sheikh kuwa anataka kubadili Sunday Schools zote makanisani ziwe madrasa.
Sasa hapo simama na utulie tuli uwaze nini kingefuatia kwa sheikh huyo.
Jaribu kufikiri kurasa za mbele za magazeti siku ya pili yangekuwaje?
Mimi naogopa hata kufikiri ingekuwaje.
Je, unaweza kufikiri Jeshi la Polisi lingesema nini na kuchukua hatua gani?
Hakuna kilichofanyika.
Magazeti yote yalikuwa kimya.
Jeshi la Polisi lilikuwa kimya.
Waislam walikuwa kimya.
Na hadi leo Waislam bado wako kimya na wataendelea kuwa kimya.
Lakini si kama kweli Waislam wako kimya.
Kuwasikia Waislam inahitaji uwe na masikio.
Waislam tumesema kwa ule ukimya wetu.
Kwani ukimya una sauti.
Ukiwa na masikio mazuri utasikia sauti ya ukimya.